Polisi waua raia

Polisi waua raia

Kama kawaida yao nguvu nyingi akili kidogo.
Polisi wilayani Kaliua mkoani Tabora wamempiga risasi na kumuua raia mmoja aliekua miongoni mwa kundi la wananchi waliokua wanakabiliana na polisi hao.
Wananchi walikua wanawataka kuwaadhibu wezi wa mifugo waliokua mikononi mwa polisi.

Note-kama unajipenda kaa mbali na polisi ukirusha mchanga wanarusha risasi.

Ama kweli hii nchi ujinga unaongezeka
 
Kumbe jiwe haliuwi enhee? Wacheni kuharibu amani kwa kuendekeza ujinga

Kwanini Polisi nao wasiokote mawe wawapige hao waliobeba mawe? Siku wananchi wakipata silaha (kama za polisi), amani itatoweka nchini. Hali itakuwa kama ya Congo, Sudani, CRA n.k.
 
Kwa hyo ulitaka muue kisha mseme polisi wamesimamia mauaji? Kwa nini walipotaka kumwokoa nyie mkaamua kukabiliana na polisi? Pumb. Vu zenu

Kwa akili zako,kufa jambazi na kufa raia mwema kipi kina afadhari? Crazy typ.
 
Mimi na wewe hatukuwepo, lkn melezo ya mleta mada yanaashiria principle hyo ilitumika. We mtu anadiriki kuandika "tunakabiliana na polisi". Mpaka kukabiliana tayari tayari wamepewa onyo

Polisi huwa na vifaa vingi sana na mbinu za kukabiliana na Raia. Sioni sababu yao kutumia silaha moto. Kwanza wanakuwa wamevaa vifaa vya kujilinda kimwili. Pia raia anakuwa hawana silaha moto.
 
Polisi sikuhizi wanafundishwa kulinda wahalifu na kuua raia na sio kudhibiti uhalifu.
 
Polisi sikuhizi wanafundishwa kulinda wahalifu na kuua raia na sio kudhibiti uhalifu.

raia kuua raia mwenzake kwa tuhuma ambazo hazijathibitishwa naye ni mhalifu.

na kwa mjibu wa viapo vya askari, ukiangalia sheria iliyounda jeshi hilo, kulinda watu na mali zao, kulinda watuhumiwa na wahalifu wenyewe ni kazi ya polisi kufanya hivyo, kuhakikisha watu wote wanakuwa salama.

Na sheria zinaruhusu matumizi ya nguvu katika kuokoa maisha.
 
Polisi huwa na vifaa vingi sana na mbinu za kukabiliana na Raia. Sioni sababu yao kutumia silaha moto. Kwanza wanakuwa wamevaa vifaa vya kujilinda kimwili. Pia raia anakuwa hawana silaha moto.

unasema unayoyajua au unasema ili mradi tu umesema? kidhana wanatakiwa kuwa na vifaa vyote mhimu vya kujilinda lkn ukweli uliopo vifaa vilivyopo ni vichache ndio maana tunawaona wanafanya kazi wakiwa hawajavivaa. hata leo ukikatizza mtaani, utawakuta wanapiga kazi bila vifaa hivyo. nimekutana nao wengi tu.

Halafu hata kama una vifaa vya kujilinda, mwananchi anapokabiliana na wewe, lengo lake unalijua? tujifunze kuheshim kazi za watu wengine, la sivyo sote tutalia. polisi watalia na raia tutalia
 
Watasema huyo mwananchi alikuwa na Silaha na alitishia usalama wa polisi.

Yaani raia mwenye jiwe anatishia usalama wa askari mwenye mguu wa kuku!

sijui tunakwenda wapi majuzi basi limegonga bodaboda bila kujua mwenye kosa ni nani huko singida wanachi wakaamua kuchoma basi moto....sasa hili nalo sahihi mambo mengine tujiangalieni jamani
 
Kwa akili zako,kufa jambazi na kufa raia mwema kipi kina afadhari? Crazy typ.

hivi hujawahi kuona mtu anauwawa kwa tuhuma za uongo? hujawahi kusikia mtu anapigiwa mwano wakati si yeye ametenda kosa na anaadhibiwa kwa kosa ambalo hajafanya? nani kathibitisha kuwa yule jambazi? usipende kujichukulia sheria mkononi, ipo siku utajibu kesi ambayo haikuwa lazima. kwani wewe hakimu?
 
Kwanini Polisi nao wasiokote mawe wawapige hao waliobeba mawe? Siku wananchi wakipata silaha (kama za polisi), amani itatoweka nchini. Hali itakuwa kama ya Congo, Sudani, CRA n.k.

kwani wananchi hawana silaha hizo? si polisi kila siku wanauwawa kwa risasi? halafu chukulia wako polisi wawili, ndio wanataka kuokoa maisha ya mtu anayetuhumiwa kufanya kosa, lakini wananchi wanaotaka kuua mtuhumiwa wapo 20 hadi 50. polisi atachukua mawe mangapi kukabiliana na watu 50? tumia akili wewe
 
raia kuua raia mwenzake kwa tuhuma ambazo hazijathibitishwa naye ni mhalifu.

na kwa mjibu wa viapo vya askari, ukiangalia sheria iliyounda jeshi hilo, kulinda watu na mali zao, kulinda watuhumiwa na wahalifu wenyewe ni kazi ya polisi kufanya hivyo, kuhakikisha watu wote wanakuwa salama.

Na sheria zinaruhusu matumizi ya nguvu katika kuokoa maisha.

uko sahihi mku ila tatizo hapo kila mmoja kakosa imani na mwenzake. lkn pia raia hujichukulia sheria mkononi hasa pale wanapowapeleka wahalifu polisi kisha wanaachiliwa na kuanza kuwatishia maisha wale waliowapeleka polisi. hali hii huwakatisha tamaa wananchi au raia na kuamua kujichukuliaa sheria mkononi. Kiukweli haukutakiwa kuwa hivyo.
 
uko sahihi mku ila tatizo hapo kila mmoja kakosa imani na mwenzake. lkn pia raia hujichukulia sheria mkononi hasa pale wanapowapeleka wahalifu polisi kisha wanaachiliwa na kuanza kuwatishia maisha wale waliowapeleka polisi. hali hii huwakatisha tamaa wananchi au raia na kuamua kujichukuliaa sheria mkononi. Kiukweli haukutakiwa kuwa hivyo.
tuanzie hapo, kwa nini mtuhumiwa anakamatwa na baadae kuachiwa?
 
kwani wananchi hawana silaha hizo? si polisi kila siku wanauwawa kwa risasi? halafu chukulia wako polisi wawili, ndio wanataka kuokoa maisha ya mtu anayetuhumiwa kufanya kosa, lakini wananchi wanaotaka kuua mtuhumiwa wapo 20 hadi 50. polisi atachukua mawe mangapi kukabiliana na watu 50? tumia akili wewe

Usitetee uovu wa polisi wewe.
Polisi risasi siku hizi wanapiga risasi ovyo hata sehemu isipohitajika kufanya hivyo.
 
Rushwa ndio tatizo.

inaweza kuwa ni hoja, lkn si yenye mashiko. tatizo kubwa tulilonalo, tunapenda kuwapeleka watuhumiwa wa uhalifu polisi kama kuwahifadhi. hakuna anayejitokeza kudai kafanyiwa uhalifu, hakuna aliyetayari kutoa ushahidi mahakamani na hakuna anayefuatilia kujua mtuhumiwa aliyefikishwa kituo cha polisi ana kesi gani ya kujibu. tunachokosea, tukiwafikisha kituoni, tayari tunajua tumeshamaliza kila kitu.

mara nyingi polisi huabika mahakamani, pale hakim anapohitaji kumwona mlalamikaji dhidi ya mtuhumiwa. akikosekana mlalamikaji, mtuhumiwa hana kesi ya kujibu, hivyo anaachiwa huru, anarudi kitaa.

Hii haijaanza leo, ipo tangu enzi na enzi, ndio maana huwa nakataa hoja ya kuwa wananchi wamepoteza imani na wananchi, ni hoja ambayo ukiichambua haina ukweli wowote.
 
Back
Top Bottom