RUBERTS
Senior Member
- Apr 5, 2012
- 136
- 50
Jeshi la Polisi nchini ndilo linahusika na kuratibu usafirishaji haramu wa Wasomari na Waethopia nchini kupitia maeneo mbalimbali ya nchi yetu, licha ya Rais Kikwete juzi kuwamwagia sifa kuwa wanashughulika sana kukabiliana na uhalifu huo.
Ushahidi ninao.
Katika maeneo yote ya bahari kuanzia Feri Kigamboni hadi Kimbiji ambapo ni eneo la wilaya ya Kipolisi Kigamboni, kazi ya kuingiza wahamiaji haramu inaratibiwa na mtu mmoja yuko Kigamboni anaitwa Maafudhi/Maabubu.
Mtu huyu anashirikiana kwa karibu sana na Mkuu wa Kituo cha Polisi Kigamboni anayeitwa Mlasani. Wasomali wanaingilia maeneo ya ufukwe wa Kigamboni kuanzia Minazi Mikinda hadi Kimbiji.
Wasomali hawa wanaletwa na maboti hadi ufukweni na polisi kwa macho yetu tunaona wanawasindikiza kuwaingiza kwenye maroli yanayokuwa yameegeshwa barabarani yakisubiria.
Magari aina ya Canter au Fuso yakiwa yamefunikwa maturubai huwa yanatumika sana. Kama serikali inataka kujua ukweli wa jambo hili ifuatilie kwa wananchi na viongozi wa vijiji wa maeneo ya ufukwe wa Kigamboni.
Polisi wakibisha nitamwaga mambo zaidi hapa.
Ushahidi ninao.
Katika maeneo yote ya bahari kuanzia Feri Kigamboni hadi Kimbiji ambapo ni eneo la wilaya ya Kipolisi Kigamboni, kazi ya kuingiza wahamiaji haramu inaratibiwa na mtu mmoja yuko Kigamboni anaitwa Maafudhi/Maabubu.
Mtu huyu anashirikiana kwa karibu sana na Mkuu wa Kituo cha Polisi Kigamboni anayeitwa Mlasani. Wasomali wanaingilia maeneo ya ufukwe wa Kigamboni kuanzia Minazi Mikinda hadi Kimbiji.
Wasomali hawa wanaletwa na maboti hadi ufukweni na polisi kwa macho yetu tunaona wanawasindikiza kuwaingiza kwenye maroli yanayokuwa yameegeshwa barabarani yakisubiria.
Magari aina ya Canter au Fuso yakiwa yamefunikwa maturubai huwa yanatumika sana. Kama serikali inataka kujua ukweli wa jambo hili ifuatilie kwa wananchi na viongozi wa vijiji wa maeneo ya ufukwe wa Kigamboni.
Polisi wakibisha nitamwaga mambo zaidi hapa.