Polisi wamshughulikie Mchange katika mambo haya 10...

Polisi wamshughulikie Mchange katika mambo haya 10...

kijana kama huyu ukimuangalua ni dhahili hakuwa na dira ya maisha na alikuwa in choka mbaya kabla hajajanjaruka....kweli mjini panawatoa watu ushamba...maana ukiangalia kila alichovaa ni dhahili ujanja kaupata baada ya kufika mjini.

Ushauri Vijana kama huyu Mchange wangeachiwa Vijana wa Mwamnyange wamhoji angalau dakika 15 wakiwa nae faragha basi wakimuachia utamkuta tayari karudi kijijini bila kupenda na bila kufahamu kafikaje kijijini nakuanza mradi wa kulima nyanya.
Maana kijana kama huyu akilelewa kijinga kama hivi na kuachia kuropoka vitu ambavyo ukivifuatilia kwa undani ni kama kuchezea akili za watz na jeshi zima la nchi ambalo ndo lenye dhamana ya kulinda amani ya nchi...basi ujue tabia yake itakuwa zaidi na baadae utasikia kama siyo kuunda kundi kama la Alshababu hapa Tz basi atajiunga na Alshababu wenyewe na kutekeleza mauaji hapa nchini.

Vyombo vikuu vya usalama muwe makini sana na Vijana kama hawa ambao wanaachiwa wanalopoka vitu hatarishi kisa kupata pesa .

Unajikumbuka ulivyokuwa kabla hujaanza secondary?
Ulizaliwa na ujanja?
 
Arudishe pesa za CCM maana ni tapeli kiasi cha Manifesto ya Uchaguzi mdogo Igunga anaita mpango wa Chadema kumteka Mussa Tesha na kummwagia tindikali. Hata kijana wa Chadema aliyeuliwa toka Dar hamkumbuki bali anabwabwaga ili Nape na wenzake wamkubali. Anathubutu kudanganya Mnyika alikuwa Igunga kumbe hakuwepo Bongo alikuwa safarini Zambia
 
Lengo ni kupoteza attention ya mchakato wa katiba lakini hawatafanikiwa
 
Nimekuwa nikafatilia malumbano kati ya Habibu Mchange na Madiwani wa CHADEMA kutuhumiana kesi za mauaji,Jeshi la polisi pia limeamua kuingilia kati swala hili.Naimani tuhuma na malumbano haya yamewagusa watanzania wengi,hasa wafuatiliaji wa siasa ya Tanzania.

Ni tuhuma za kushangaza na kushitua lakini hizi tuhuma si mara ya kwanza kutolewa cha kushangaza huibuliwa na huzimwa bila majibu kwa watanzania,kiasi ambacho kinatufanya tuamini ni mbinu au mkakati unaoandaliwa kwa masilahi ya watu Fulani huku wapuuzi Fulani wakitumika kufanikisha mkakati.

Kwa mtu makini anaweza kubaini kuwa nyuma ya jambo hili kuna mkakati umefichika,kwani tuhuma hizi pia zinakuja kipindi ambacho kuna mjadala mzito wa KATIBA na unaoelekea kuwaelemea baadhi ya watu lakini pia ni kipindi ambacho
CHADEMA wanajiandaa na uchaguzi wao wa ndani wa kupata viongozi katika chama,Lazima tulitafakari swala hili kwa umakini ikiwa pia na CHADEMA kuwatafakari hao madiwani walioibua tuhuma hizi,wasijekuwa ni miongoni mwa wapuuzi wanaotekeleza mkakati wa kuhamisha watanzania katika maswala ya msingi.

Ni jambo la kushangaza pia kuona Jeshi la polisi kuingilia swala hili katika sura ya kuegemea upande mmja,hapa ndipo inakuja shaka kuu na kuona kinachoendelea na kinachofanywa na Mchange ni upuuzi unaoratibiwa kwa masilahi ya watu Fulani.

Jeshi la polisi limesikika likitoa taarifa kuwa linafatilia mwenendo wa viongozi wa
CHADEMA,hapa swala si kufatilia,kwani hiyo ni sehemu ya wajibu wao,lakini kwa nini kama linania dhabiti halikufatilia tuhuma zilizotolewa na madiwani wa CHADEMA dhidi ya viongozi wa CCM,badala yake liliziita tuhuma hizo ni propaganda za kisiasa,kwa nini Jeshi la Polisi limeamini tuhuma za Mchange na kuanza kuzifatilia?

Na kwanini tuhuma nzito namna hiyo za ugaidi awenazo Mchange? Jeshi la polisi halioni kuwa Mchange na madiwani wanatakiwa wakamatwe wahojiwe vizuri na kama ni uongo wachukuliwe hatua kwa kupotosha na kuleta uchochezi unaoweza kuvunja amanin ya nchi yetu?

Lakini tuhuma zingine za mauaji (Ugaidi) zinazotolewa na Mchange,ambazo pia zilifanywa hadharani kama mauaji ya Mwandishi wa Habari Daudi Mwangosi,zinashindwa kugunduliwa na Jeshi la polisi lenye wapelelezi waliosomea na wanaolipwa mishahara kwa kodi za watanzaniana kumbaini muuaji au kutolewa ufafanuzi wa kuridhisha mpaka leo na zinatolewa na Mchange,

Je jeshi la polisi linajidhihirishia kwa watanzania kuwa haliwezi kazi yake na linazidiwa intelejensia na mtu kama Mchange? Jeshi letu la polisi lazima liwe makini kwa sababu limebeba dhamana kubwa katika nchi yetu,litafakari kwa umakini kabla halijatoa matamko na kuingilia baadhi ya maswala ya kisiasa yanayoweza kulidharirisha,kwa namna hii tutaamini kuwa baadhi ya viongozi wa jeshi letu wanatumikia watawala na wanatumika kudhoofisha vyama vya upinzani Nchini katika maswala yanayogusa masilahi ya Nchi yetu.

Tuhuma kama hizi za mauaji hazijaanza kutolewa leo,watanzania tunakumbuka alivyokamatwa Mkurugenzi wa usalama CHADEMA Lwakatare akibambikisiwa kesi kama anazositoa Mchange za Ugaidi lakini mahakama ikafutilia mbali tuhuma hizo,lakini cha kushangaza jeshi la polisi limekuwa likiendelea kuingia katika mtego huu wa wapuuzi wachache kwa kuwabambikizia kesi viongozi wa upunzani ambao ni tishio kwa wanasiasa wanaotaka kuendelea kufanya upuuzi katika nchi hii,Kwa nini jeshi la polisi linaendekeza mambo haya?

Na kwanini linaingia kwenye upuuzi wa Mchange na kumuunga mkono badala ya kumkamata na kumhoji juu ya tuhuma nzito namna hii za Ugaidi, ni kwa nini tuhuma zinazotolewa kuelekezwa kwa baadhi ya viongozi wa CCm na viongozi wa Serikali hazifanyiwi kazi kwa namna kama ambavyo tuhuma zinazotolewa kwa viongozi wa Upinzani? je ni nani asiyejua madhara ya Ugaidi Duniani na ni nan yuko tayari kuona magaidi wanaendelea kufanya madhara?

Watanzania tunaanza kuamini kuwa Jeshi letu linatumika vibaya,Kama kweli Jeshi la polisi halitumiki basi ni wakati mwafaka kuwakamata wahusika wote na kuutafuta ukweli,kama litaendekeza kutoa matamko na kukaa kimya basi jeshi letu lazima liangaliwe na watu wanaolichafua wawajibishwe.Watanzania tunataka kujua ni hatua gani zitafuaata baada ya tuhuma hizi na kama Mchange na madiwani wanatudanganya basi wachukuliwe hatua za kisheria kwani wanahatarisha usalama na amani ya Nchi yetu. Upendeleo wa namna hii wa vyombo vya dola kama hautadhibitiwa mapema unaweza kuleta athari katika Nchi yetu.

Mchange jitafakari upya na utueleze nia yako hasa ni nini katika hili,watanzania makini wanakuona unafanya upuuzi na tunatafakari hata Elimu uliyonayo inakusaidia nini katika maisha yako,leo huruma hii unayoionesha imetoka wapi? Na kwa nini ije katika kipindi ambacho nchi yetu inasongwa na mambo mazito ya kujadili?

Mbona siku zote hizo hukuamua kuyasema haya unayoyasema? Na kwa nini usipeleke katika vyombo vinavyohusika ili wahusika wa Ugaidi wachukuliwe hatua sitahiki badala yake unatapatapa kutumia vyombo vya habari kutangaza Ugaidi wa viongozi wako?

Waswahili wanasema Simba akizidiwa hula Nyasi,hiki ndicho ninachokiona kwa Mchange,anaamua mpaka kujidharilisha kwa sababu ya kuwatumikia watu anaowajua yeye,kwani kama hawatumikii yeye pia atueleze na ajitangaze alivyohusika katika ugaidi aache unafiki lakini pia asitenganishe ugaidi huo na viongozi wasaliti kwani kama ugaidi upo nao pia wamehusika kwa namna Fulani kwani walikuwa viongozi CHADEMA,Mchange atueleze watanzania wote vizuri ili tusiamini anafanya upuuzi kuua upinzani na kutuhamisha watanzania katika mijadala ya msingi,kama nia yako ni kuibomoa CHADEMA na kuwapotosha watanzania,hata kama vyombo vya dola havitakushughulikia hakika Mungu atakushughulikia na laana itakufata,na wale wale unaowatumikia watakutafuna tena wewe,watakukaanga kwa upuuzi wako mwenyewe. "Mwiba hutokea ulipoingilia".

Ex-Vice president Ditso.
Costantine R Bandiho
0762421085-cbandiho@yahoo.com
 
Bado Mnyika,Lissu,Mbowe.
Na hayo Maswali wataulizwa wao.
Mchange kaenda kutoa melezo tuu!

Kwa hiyo bavicha mna imani na jeshi letu la polis I? Litapochukua hatua ambazo hazitokufurahisha usisahau kulipongeza jeshi letu La polisi.

Nashukuru kuona bavicha mnaanza kuliamini jeshi letu la polisi na usisahau kumshauri mbowe kupeleka hule mkanda wa mauji ya Soweto.

Nakutakia kila LA kheri kwenye kugombea uenyekiti wa bavicha.

Akiambiwa athibitishe??
 
huyu kijana kajitakia makubwa asiyoyaweza,,,hata kama anayoyasema ni ya kweli basi na yeye yumo kwenye kundi hilo hilo so hata yeye hawezi kupona...he is also a culprit...pili hao aliowataja ni politicians trena wenye wafuasi wengi zaidi ..ebu imagine leo mbowe anakamatwa au lisu asilaa mnyika hata kama ni kweli itajulikana ni njama ya serikali so mimi naona huyu kijana kajitakia ya ludovick
 
Frankly speaking....hivi kuna mtu anayeamini hayo anayoyasema huyu jamaa?
mimi siamini labda wale wenye mahaba na chama kile cha kijani na kile chama kilichoanzishwa juz kati...aka chama cha mwandiga
 
huyu kijana kajitakia makubwa asiyoyaweza,,,hata kama anayoyasema ni ya kweli basi na yeye yumo kwenye kundi hilo hilo so hata yeye hawezi kupona...he is also a culprit...pili hao aliowataja ni politicians trena wenye wafuasi wengi zaidi ..ebu imagine leo mbowe anakamatwa au lisu asilaa mnyika hata kama ni kweli itajulikana ni njama ya serikali so mimi naona huyu kijana kajitakia ya ludovick
 
Kuna wanasiasa wachache sana wanaofanya watanzania waichukie siasa,,siasa sio mbaya ila ,,wanasiasa ndio wabaya,,,TANGU MH MBOWE ALIPOSEMA ANAVIDEO YA MAUWAJI YALIYOTOKEA SOWETO ARUSHA....lakini mpaka leo imekuwa kitendawili,,SINA IMANI KABISA NA CHADEMA,,,na yote aliyosema MCHAGE YANAUKWELI,,,maana kimekuwa chama cha uwongo uwongo tuuu....chama chenye maneno ya hovyo hovyo,,,,
 
Alinishangaza sana aliposema eti Mwangosi aliuawa na chadema, bila ile picha sijui cdm wangekuwa na hali gani sasa hivi- Lakini, kwa kuwa Mungu hakupenda mwana wake aonewe, alimtuma mtumishi wake, akamuelekeza achukue picha ile muhimu. Hata walipoanza kutunga uongo, akamuelekeza mtumishi wake atoe picha ile kwa wakati muafaka.

Ghafla uongo wa adui ukashindwa. Sasa iweje kijana mwenye mtindio wa ubongo anayeitwa Habibu Mchange apindue ukweli wa kuiita nyeupe kuwa nyeusi na sisi tumkubali wakati tunajua ubongo wake umevia? Penginepo na sisi bongo zetu ziwe na walakini hilo linaweza kutokea!
 
Nilishasema, Siasa za Tanzania kutupiana vijembe, nani kafumaniwa, nani kauawa, nani tumwue na nani afanye vipi, shida moja moja kwa moja, Mtanzania ulijua jambo la miaka na ukalinyamazia, Wewe mtuhumiwa namba moja wa kusimama mahakamani, No way to escape......Mchange una kesi ya kujibu
 
Hivi kwa nini jeshi la polisi halioni aibu kujitanabaisha hadharani kwamba halina misingi ya kazi na maamuzi zaidi ya kufuata matakwa na ccm? Kwa nini liliogopa kuwahoji madiwani walotoka ccm na kuwafuatilia waliotajwa wote, halafu bila haya linaunga mkono maneno ya mchange?

Mauaji ya Mwangosi hayakufanywa hadharani na polisi wenyewe?

Baada ya taarifa za kifo cha mwangosi polisi Iringa walisema mwangosi ameuawa na wa fuasi wa CDM waliovaa mavazi ya kipolisi wamemtupia bomu ili kuichafua serikali.

Wakati ule anauawa mwangosi, kulitolewa agizo watafutwe wote waandishi waliopiga picha na wanyang'anywe chips. Wapiga picha hao walikimbia kwenye mashamba ya mahindi nyororo ili kujiokoa na hatimaye kukimbiza picha zao mtandaoni. Kusudi kama serikali innawakamata na kuwaua taifa lijue ukweli wa yaliyotokea.

Picha zilipotoka, zikiwaonyesha polisi na Kamuhanda akiwa kakumbatiwa na Mwangosi ili alindwe, na yule kijana polisi aliyetoka dodoma akitafuta mwanya wa kumrenga hadi akamuua mwangosi, Jeshi la polilis likasema, askari hakuwa na weledi wa kutumia ilie silaha. Alitakiwa kupiga juu lakini akalenga degrees zisizo sawa na hivyo kumpiga Mwangosi. Wakati polisi wanasema hayo, picha ziko wazi kijana anamlenga mwangosi makusudi na askari wengine wamemshambuliwa kwa , marungu na hadi utumbo wa Mwangosi umemwagika pale kati kati yao ndipo walipoondoka eneo la tukio.

Inafahamika yule kijana alilyempiga mwangosi alikuwa kituo kimoja dodoma na ameandaliwa makusudi kufanikisha mauji ya serikali. Habari za kuaminika huyo kijana hata Morogoro alikuwepo. UKitafakari sana, kwa nini jeshi la polisi lisafirishe askari kutoka dodoma kwa ajili ya kuzuia ufunguzi wa ofisi za cdm nyororo wakati Iringa nzima imejaa askari?

Kijana yule amekuwa akipelekwa mahakamani kwa ulinzi kwa usiri mkubwa kutoka jeshi la polisi ili watu wasimwone suraNi nini hatima ya ile kesi? BAADA ya haya yote, leo Jeshi hilohill oa polisi lililokiri kufanya mauaji baada ya kuanikwa hadharani, linajidai kutofahamu undani wa mauaji hayo, na kununua hadithi za Mchange kwamba aliuliwa na CDM waliowavalisha magwanda watu na kuwapa silaha za polisi. Kinatatufwa nini hapa?

JESHI LA POLISI KWA NINI MNATAKA KUWA CHANZO CHA MACHAFUKO TANZANIA? HUO NI UNAFIKI TU KWA SERIKALI AMA KUNA KITU KINGINE MNATAFUTA? WATANZANIA SI WAPUMBAVU. HILI MLIELEWE.
 
Mkuu habibu yupi unayemwongelea wewe aliyelizidi akili jeshi la polisi? - huyu hapa????

attachment.php
 
Jeshi la polis kama litaingia mkenge kwa huu uzushi wa huyu mchange nitalipuuza mara moja. Mchange anatoa tuhuma faki baada ya kufukuzwa cdm, hizi ni chuki za wazi, hakuna jipya hapo.
 
Tanzania kikwazo cha mabadiliko ni vyombo vya dola kunyong'onyeza upinzani. Mfano polis!
 
Back
Top Bottom