POLISI kanda maalumu Tarime/Rorya wanachunguza tukio la askari wake wawili kulimiminia risasi basi la abiria lenye namba za usajili T 928 BWK likiwa limeegeshwa baada ya wao kulisimamisha.
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya, Sebastian Zakaria wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi aliyetaka kujua sababu za milipuko ya risasi katika mtaa wa Mawasiliano, Tarime mjini jana asubuhi.
Watu walioshuhudia tukio hilo wamesema kwamba basi hilo ambalo hufanya kazi ya daladala lilisimamishwa na askari polisi wawili waliokuwa wakitaka dereva alipeleke basi hilo kituo cha polisi kwa ukaguzi.
Imeelezwa kuwa dereva huyo anayetambuliwa kwa jina la Robert Merengo (31) alipouliza sababu ya kupeleka basi lake hilo dogo la abiria aina ya Toyota Double Coaster polisi, askari mwenye bunduki alifika na kumtoa katika kiti chake cha udereva huku akiwa amemshikia mtutu shingoni.
Akisimulia mkasa huo, Merengo alisema akiwa nje ya sehemu ya kuuzia mbao mjini hapa Mtaa wa Mawasiliano alikopita baada ya kushuka abiria stendi ya mabasi Walimfuata askari wawili pale alipoegesha, mmoja trafiki na mwingine wa kawaida akiwa na bunduki na kuamuru aligeuze gari na kulipeleka Kituo cha Polisi.
Alisema alipowauliza gari hilo lina kosa gani, askari aliyekuwa na bunduki akamwambia ashuke kutoka ndani ya gari huku akimuelekeza bunduki.
Nilitii amri kwa kuteremka, huku nikiacha gari ikiunguruma. Nilipoteremka chini walitaka kunipiga ndipo mama mwenye duka alipoingilia kati na kuhoji kwanini wanipige badala ya kuchukua namba za gari na kumtafuta mmiliki wake.
Kabla mama yule hajamaliza kuwaeleza walifyatua risasi saba kwenye mlango wa kushoto na kusababisha watu pale mtaani kukimbia ovyo.
Naye mmiliki wa basi hilo, Mohere alipoulizwa kuhusiana na basi lake kuwa huenda halina nyaraka muhimu zinazoliruhusu kutembea barabarani, alisema lina vibali vyote. "Gari langu lina vibali vyote, nasikitika kwa askari huyu kuniharibia gari na kutaka kuua dereva, alilalamika.
Pamoja na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya, Sebastian Zakaria kusema kwamba hakuna mtu aliyejeruhiwa na kwamba uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea, ikiwa ni pamoja na kuwahoji askari waliohusika na tukio hilo, wananchi walisema kwamba lilileta kizaazaa kikubwa.
Mara baada ya tukio, mmiliki wake Boniface Mohere alifika eneo la tukio na kuamuru lipelekwe makao makuu ya polisi wilayani hapa akitaka aelezwe sababu za kuharibiwa kwa gari lake.
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya, Sebastian Zakaria wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi aliyetaka kujua sababu za milipuko ya risasi katika mtaa wa Mawasiliano, Tarime mjini jana asubuhi.
Watu walioshuhudia tukio hilo wamesema kwamba basi hilo ambalo hufanya kazi ya daladala lilisimamishwa na askari polisi wawili waliokuwa wakitaka dereva alipeleke basi hilo kituo cha polisi kwa ukaguzi.
Imeelezwa kuwa dereva huyo anayetambuliwa kwa jina la Robert Merengo (31) alipouliza sababu ya kupeleka basi lake hilo dogo la abiria aina ya Toyota Double Coaster polisi, askari mwenye bunduki alifika na kumtoa katika kiti chake cha udereva huku akiwa amemshikia mtutu shingoni.
Akisimulia mkasa huo, Merengo alisema akiwa nje ya sehemu ya kuuzia mbao mjini hapa Mtaa wa Mawasiliano alikopita baada ya kushuka abiria stendi ya mabasi Walimfuata askari wawili pale alipoegesha, mmoja trafiki na mwingine wa kawaida akiwa na bunduki na kuamuru aligeuze gari na kulipeleka Kituo cha Polisi.
Alisema alipowauliza gari hilo lina kosa gani, askari aliyekuwa na bunduki akamwambia ashuke kutoka ndani ya gari huku akimuelekeza bunduki.
Nilitii amri kwa kuteremka, huku nikiacha gari ikiunguruma. Nilipoteremka chini walitaka kunipiga ndipo mama mwenye duka alipoingilia kati na kuhoji kwanini wanipige badala ya kuchukua namba za gari na kumtafuta mmiliki wake.
Kabla mama yule hajamaliza kuwaeleza walifyatua risasi saba kwenye mlango wa kushoto na kusababisha watu pale mtaani kukimbia ovyo.
Naye mmiliki wa basi hilo, Mohere alipoulizwa kuhusiana na basi lake kuwa huenda halina nyaraka muhimu zinazoliruhusu kutembea barabarani, alisema lina vibali vyote. "Gari langu lina vibali vyote, nasikitika kwa askari huyu kuniharibia gari na kutaka kuua dereva, alilalamika.
Pamoja na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya, Sebastian Zakaria kusema kwamba hakuna mtu aliyejeruhiwa na kwamba uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea, ikiwa ni pamoja na kuwahoji askari waliohusika na tukio hilo, wananchi walisema kwamba lilileta kizaazaa kikubwa.
Mara baada ya tukio, mmiliki wake Boniface Mohere alifika eneo la tukio na kuamuru lipelekwe makao makuu ya polisi wilayani hapa akitaka aelezwe sababu za kuharibiwa kwa gari lake.