mtendaji wa kijiji
JF-Expert Member
- Jul 3, 2012
- 533
- 115
Hongera Jesh la polisi kwa kuendeleza mauaji. Nadhan The Heg inamwasubiria Said Mwema
Mkuu si unajua tena taarifa za kipolisi "UCHUNGUZI BADO UNAENDELEA","INAHISIWA NDIYO ILISABABISHA KIFO CHAKE"Sio wamesababisha kifo, hapana, bali wameua kwa kutumia "flying object"
Jeshi la polisi mkoani Kigoma,linawashikilia askari wake wawili kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mkazi mmoja wa kijiji cha Herushingo,tarafa ya Makere,wilaya ya Kasulu. Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na kamanda wa polisi mkoani humo,Fraisser Kashai,alisema tukio hilo lilitokea Decemba 25,mwaka huu,saa nne usiku katika kijiji hicho.
Aliwataja askari hao kuwa ni D.8622 CPL,Peter na G.1236 PC Sunday wa kituo kidogo cha Rerushingo ambapo wanadaiwa kumshambulia Bw.Gasper Mussa (36),ambaye ni mkulima katika baa waliyokuwa wanakunywa na baada ya kumpiga,walimfikisha kituoni hapo. Alisema Decemba 26 mwaka huu,mkuu wa kituo hicho alitoa taarifa kituo cha polisi kwa SP Sospeter kunguru kuwa mtuhumiwa alikuwa mgonjwa lakini alifariki muda mchache baada ya kufikishwa katika hospitali ya wilaya ya Kasulu.
"Chanzo cha ugomvi ni baada ya marehemu kushindwa kulipa vinywaji alivyokunywa ndipo askari walipoanza kumshambulia na kumsababishia maumivu yaliyosababisha kifo chake," Alisema kutokana na tukio hilo,askali hao wamekamatwa na wanashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi ili kubaini chanzo hasa cha ugomvi huo na kama itabainika walihusika moja kwa moja watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka ya mauaji.
Chanzo cha Habari:Gazeti la Majira la Desemba 28,2012,habari hii inapatikana ukurasa wa 3.
My Take Kadri siku zinavyozidi kwenda, mmomonyoko wa maadili kwa askari wetu unazidi kukuwa.Askari wetu wamejenga tabia ya kuchukua sheria mkononi (Instant justice).Hii pia imezoeleka hata kwa sisi raia,utasikia mtu anakwambia "unauliza makofi polisi" yaani anamaanisha askari ana haki na kuchukua sheria mikononi pale anapojisikia kufanya hivyo.Tabia hii ni mbaya na inaenda kinyume na kaki za binadamu.Kuna haja ya kufanya uchunguzi yakinifu, ili kujua kama askari wetu huwa wanafundishwa nini kwenye vyuo vya polisi,inawezekana huwa kuna mafunzo maalumu wanaopewa ambayo yanakinzana na haki za binadamu.
Mkuu hapo hakuna kitu ni sawa na kesi ya nyani apelekwe ngedere akaitolee maamuzi!Kwa hali hii ya police kujichukulia sharia mkononi sasa imechukua kasi ndani ya Nchi yetu inayodai ya Amani na utulivu!
Na kwa jinsi ilivyo hautaacha kusikia kesho kutwa askari hao wako huru!
Ndiyo maana wale wananchi wa mkoa wa Kagera waliamua kumalizana na wale askari wawili,kwani walijua watapigwa danadana na maneno ya kipolisi "UCHUNGUZI BADO UNAENDELEA".Kwa hali hii polisi hawaaminiki tena kwenye jamii yetu!Hakuna haja ya kuwakamata polisi. Badala yake wangewaachia na kuwauliza wananchi nini adhabu ya wauaji hawa. Simpo. Wananchi sasa wamechoka.
Ingekuwa ni huku kila kitu kinachunguzwa...hata kama mtu alikufa miaka 50 iliyopita ili mradi kaburi lake linapatikana...ni mambo ya "Carbon Fourteen"Mkuu si unajua tena taarifa za kipolisi "UCHUNGUZI BADO UNAENDELEA","INAHISIWA NDIYO ILISABABISHA KIFO CHAKE"
Huko wapi mkuu?Sisi bado tunaendelea na mambo yetu ya kibongobongo ya "UCHUNGUZI BADO UNAENDELEA HATA BAADA YA MIAKA KUMU BAADA YA TUKIO"Teh teh teh!Ingekuwa ni huku kila kitu kinachunguzwa...hata kama mtu alikufa miaka 50 iliyopita ili mradi kaburi lake linapatikana...ni mambo ya "Carbon Fourteen"
Huko wapi mkuu?Sisi bado tunaendelea na mambo yetu ya kibongobongo ya "UCHUNGUZI BADO UNAENDELEA HATA BAADA YA MIAKA KUMU BAADA YA TUKIO"Teh teh teh!
Mkuu karibu sana tulikarabati linchi letu!"An imminent disaster"(We acha tu)Mkuu TUKUTUKU maisha ni kutafuta ila kesho nitatua JKIA, NBO Kenya, na baadaye Arusha na Dar before kuondoka. Anyway maisha ndivyo yalivyo..Nina wadau wa kuonana nao.
Mkuu karibu sana tulikarabati linchi letu!
Policcm ni hatari, utaskia kesi inaisha kiaina, inabid tuwaroge tu.😛ainkiller:Raia mmoja mwenyeji wa Kata ya Heru - Ushingo Wilayani kasulu, ameuwawa na Polisi kwa kupigwa risasi, baada ya fujo iliyotokana na tofauti za njia ya malipo ya huduma ya kinywaji katika kusherehekea Krismas.
Marehemu awali alikuwa anamdai Askari polisi. Marehemu huyo akaamua kwenda kupata kinywaji kwenye grocery inayomilikiwa na Askari polisi huyo.
Baada ya Kupata kinywaji, Askari huyo aliomba kulipwa, na kwa kuwa marehemu alikuwa anamdai Askari yule, Marehemu akamwambia Askari akate pesa yake kwenye Deni alilokuwa anamdai. Hapo ndipo mwanzo wa tatizo, lililopelekea kichapo, hadi matumizi ya silaha yaliyopelekea kifo.
Sakata hili analifuatilia kwa karibu Mbunge wa eneo hilo Mh. Agripina Buyogera (NCCR).
Chanzo: Radio Kwizera