Mangaline
JF-Expert Member
- May 19, 2012
- 1,045
- 222
Raia mmoja mwenyeji wa Kata ya Heru - Ushingo Wilayani kasulu, ameuwawa na Polisi kwa kupigwa risasi, baada ya fujo iliyotokana na tofauti za njia ya malipo ya huduma ya kinywaji katika kusherehekea Krismas.
Marehemu awali alikuwa anamdai Askari polisi. Marehemu huyo akaamua kwenda kupata kinywaji kwenye grocery inayomilikiwa na Askari polisi huyo.
Baada ya Kupata kinywaji, Askari huyo aliomba kulipwa, na kwa kuwa marehemu alikuwa anamdai Askari yule, Marehemu akamwambia Askari akate pesa yake kwenye Deni alilokuwa anamdai. Hapo ndipo mwanzo wa tatizo, lililopelekea kichapo, hadi matumizi ya silaha yaliyopelekea kifo.
Sakata hili analifuatilia kwa karibu Mbunge wa eneo hilo Mh. Agripina Buyogera (NCCR).
Chanzo: Radio Kwizera
Marehemu awali alikuwa anamdai Askari polisi. Marehemu huyo akaamua kwenda kupata kinywaji kwenye grocery inayomilikiwa na Askari polisi huyo.
Baada ya Kupata kinywaji, Askari huyo aliomba kulipwa, na kwa kuwa marehemu alikuwa anamdai Askari yule, Marehemu akamwambia Askari akate pesa yake kwenye Deni alilokuwa anamdai. Hapo ndipo mwanzo wa tatizo, lililopelekea kichapo, hadi matumizi ya silaha yaliyopelekea kifo.
Sakata hili analifuatilia kwa karibu Mbunge wa eneo hilo Mh. Agripina Buyogera (NCCR).
Chanzo: Radio Kwizera