Kamanda wa Polisi (M) Iringa akiri juu ya utata wa abiria aliyeuawa na Polisi Mafinga: Inadaiwa risasi ilipigwa upande wa dirisha la abiria.

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
May 30, 2017
2,869
3,188
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire amekiri kupata taarifa za awali za tukio la kuuawa na Polisi kwa abiria aliyekuwa katika Gari lililokaidi Amri ya Polisi ya kusimama. Kamanda Bwire ameeleza kufuatilia tukio hilo ili apate taarifa kamili. Alisema kuwa: "Ni kweli nimepata taarifa hizo lakini nazifuatilia ili nijue kwa undani kwa sababu tukio lenyewe lina utata."

Shuhuda wa ajali hiyo ameeleza kuwa, dereva wa Gari aina ya Canter aliyekuwa akiendesha kwa zaidi ya spidi 50 kutokea Iringa, alisimamishwa na Polisi lakini alikaidi Amri ya kusimama ndipo askari hao wa usalama barabarani wakaanza kulifukuza. Alieleza kuwa, Polisi walipokuwa wakilifukuza Gari hilo walipiga risasi kwenye kioo cha ubavuni upande aliokaa abiria na inadaiwa ilimjeruhi kichwani na kufariki dunia.

Hata hivyo, Polisi walipifika maeneo ya Kinyanambo C walipiga risasi katika gurudumu la gari na kumlazimu dereva kusimama.
Baada ya marehemu na dereva kupakiwa kwenye gari la Polisi, dereva alikuwa akiwalalamikia askari polisi: kwa nini mmemuua ndugu yangu, kwa nini mmemuua ndugu yangu?

Wajuvi wa mambo ya ajali, hebu angalieni Picha ya gari na eneo lililoharibiwa kioo halafu ufikirie kuwa, risasi ilipigwa wakati wanakimbizana. Akili za kuambiwa?

IMG_7474.JPG
 
Labda polisi ndiyo walikuwa wanakimbizwa! Au hapo kwenye kioo ndipo risasi ilipotokea? Halafu gari kama Canter ni ya kuikimbiza kwa mabunduki kweli?au dereva/abiria nae alikuwa na bunduki? Haya bana,hongera kwa huyo polisi maana anaweza akapandishwa cheo,hii ndiyo tanzania
 
Labda polisi ndiyo walikuwa wanakimbizwa! Au hapo kwenye kioo ndipo risasi ilipotokea? Halafu gari kama Canter ni ya kuikimbiza kwa mabunduki kweli?au dereva/abiria nae alikuwa na bunduki? Haya bana,hongera kwa huyo polisi maana anaweza akapandishwa cheo,hii ndiyo tanzania
Hapa kuna utata maana inaonekana labda walikua sambamba ndio huyo polisi akamlenga abiria au askari walikua mbele gari ilipokarabia wakamlenga abiria.Polisi Watanzania walio wengi hawana akili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna kitu hakiko sawa humo Polisi, sasa hivi karbia kila Mkoa kuna Maiti zimesuswa na ndugu kwa kuuuliwa na Polis. Mbeya maiti ina siku 50, Temeke siku zaidi ya 20, Tabora vilevile, Tarime maiti mbili, Kinondoni kama kawa, Hiii ya Iringa ndiyo kali kabisaaaa hiyo silaha yenye Rivas sijui ni aina gani?
 
Hapa kuna utata maana inaonekana labda walikua sambamba ndio huyo polisi akamlenga abiria au askari walikua mbele gari ilipokarabia wakamlenga abiria.Polisi Watanzania walio wengi hawana akili.

Sent using Jamii Forums mobile app
That's my problem mzee coz ni ngumu kumpiga abiria kutokea dirishani. Nimejaribu theories, hypotheses na approaches mbalimbali za kisayansi naona zote zimenigomea.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire amekiri kupata taarifa za awali za tukio la kuuawa na Polisi kwa abiria aliyekuwa katika Gari lililokaidi Amri ya Polisi ya kusimama. Kamanda Bwire ameeleza kufuatilia tukio hilo ili apate taarifa kamili. Alisema kuwa: "Ni kweli nimepata taarifa hizo lakini nazifuatilia ili nijue kwa undani kwa sababu tukio lenyewe lina utata."
Shuhuda wa ajali hiyo ameeleza kuwa, dereva wa Gari aina ya Canter aliyekuwa akiendesha kwa zaidi ya spidi 50 kutokea Iringa, alisimamishwa na Polisi lakini alikaidi Amri ya kusimama ndipo askari hao wa usalama barabarani wakaanza kulifukuza. Alieleza kuwa, Polisi walipokuwa wakilifukuza Gari hilo walipiga risasi kwenye kioo cha ubavuni upande aliokaa abiria na inadaiwa ilimjeruhi kichwani na kufariki dunia. Hata hivyo, Polisi walipifika maeneo ya Kinyanambo C walipiga risasi katika gurudumu la gari na kumlazimu dereva kusimama.
Baada ya marehemu na dereva kupakiwa kwenye gari la Polisi, dereva alikuwa akiwalalamikia askari polisi: kwa nini mmemuua ndugu yangu, kwa nini mmemuua ndugu yangu?
Wajuvi wa mambo ya ajali, hebu angalieni Picha ya gari na eneo lililoharibiwa kioo halafu ufikirie kuwa, risasi ilipigwa wakati wanakimbizana. Akili za kuambiwa?

View attachment 853993
Wameua polisi tena kwa risasi wakati unajua ukipa risasi nini kitatokea, ishu itafunikwa funikwa yataisha,kaua mwalimu kwa ba
hati mbaya tena katoto kenyewe maskini kalikuwa kahanga ka mateso ya nyumbani kwao,na ripoti ya daktari inathibitisha,ila kila mtu anajifanya ana hasira na kutukana walimu wote na kazi wamefukuzwa huku raia wakishangilia.....very sad....chuki chuki chuki kwa walimu na
ndio maana bila shaka vizazi vya watanzania vinakua na ujinga mwingi laana ya kudharau walimu.
 
That's my problem mzee coz ni ngumu kumpiga abiria kutokea dirishani. Nimejaribu theories, hypotheses na approaches mbalimbali za kisayansi naona zote zimenigomea.
Inatia faraja kwamba na wewe leo umewashtukia PoliceCCM wenzako. Maana huwa hamkawii kusema amejeruhiwa na kitu chenye ncha Kali kilichorushwa toka mbinguni....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo kuna mawili au matatu
(1)polisi walipiga risasi hewahi ikakatiza kona ikamuua ndg wa dereva maana risasi zao zina uwezo wa kukatiza kona.
(2)Au dereva alikuwa na bunduki mfukoni akampiga ndugu yake risasi ili kulichafua Jeshi letu!!!walimsachi kweli!!
(3)itakuwa watu wasiojulikana ndio wameingilia kati makimbizano ya polisi na kenta!!!
(4)Ama kitu chenye ncha kali tusubiri report ya postmotum
 
Back
Top Bottom