Nimesoma maoni ya watu wengi kuhusu mada hii, nimegundua watu wengi hatufahamu ubaguzi huu wa vyombo vya ulinzi na usalama, umetokanatokanaje!
Kwa macho ya kawaida na kauli za makusudi za viongozi wa siasa zinaendeleza kujenga "ukuta" na ubaguzi wa makusudi katika vyombo vya ulinzi na usalama kwa uzembe wao wa kutozibadilisha sheria za majeshi zenye harufu ya ukoloni.
Ubaguzi huu wa kujiona nani bora katika vyombo hivi, haujaanza leo. Ubaguzi huo ulitengenezwa na sheria za kikoloni kwa makusudi ya matakwa na mahitaji ama malengo maalumu ya wakati huo.
Wakati Bunge linakaa kutunga sheria ya jeshi mwaka kama sikosei 1967/8, inavyoonekana hawakutunga, bali walibariki sheria ya majeshi ya kikoloni iendelee kutumika ileile, isipokuwa kuifanyia amendments ndogondogo, mf: majina ya nchi kijiografia nk, lakini mambo ya msingi kuachwa vilevile.
Jeshi la taifa katika vitabu vyao vya sheria ambavyo wao wanaviita volumes 1,2,3 vimefafanua bila kuacha neno kuhusu stahiki zao za majukumu, nidhamu na malipo.
Hii inayoitwa posho na duty free kwenye vitabu vya sheria yao ipo kisheria, wanastahili kulishwa,kunyweshwa na kuvishwa siku ya kwanza hadi ya mwisho ya utumishi wao pia upendeleo katika manunuzi ya bidhaa.
Haya mambo ya kuwaona polisi na magereza si wanajeshi, yapo katika sheria zao(jwtz) vol 1. Inavyofafanua jinsi linapotokea jambo la hatari ama vita namna ya kuwashirikisha vyombo vingine vinavyofanana na jeshi.
Pia katika lugha za jeshi(jwtz), polisi na magereza zinatajwa kama ni taasisi za kiraia kama zilivyo taasisi zingine za kiraia, ambapo wanajeshi kwa masuala ya kinidhamu hawaruhusiwi kuwakamata na kuwatupa jela za kijeshi ama kuwafungulia mashitaka nje ya makambi ya kijeshi. Kwao polisi na magereza cjui Tiss ni raia.
Haya mambo unayoyaona hivi sasa polisi, magereza na Tiss kupokea posho ni baraka za wanasiasa, lakini hakuna sheria iliyowazi inayoeleza polisi ama magereza atalishwa chakula, vinywaji ama duty free shop, vituhivyo hakuna kisheria.
Kwa mtizamo wangu, vyombo vyote vya ulinzi na usalama vipo sawa kutokana na majukumu jinsi taifa lilivyopanga.
Kuna haja sasa kupitia upya sheria za majeshi yote ya serikali, kuyatungia sheria zinazoondoa ubaguzi katika maslahi, kuwakweza baadhi na kuwatweza wengine.
Hii kauli ya kusema kwanini wanajeshi(jwtz) wanapendelewa, ni kauli inayotoka kwa watu wasiofahamu kwamba, upendeleo huu upo katika sheria za majeshi ambazo kiukweli ni za kiupendeleo zinazostahili kubadilishwa.
Tuige mfano wa Uganda. Waganda walishaliona hili siku nyingi kuwa ni tatizo. Wao vijana wao wote huingizwa jeshi la taifa mfano kwetu jwtz na wakimaliza mafunzo ya awali, ndipo hugawiwa jeshi,polisi,magereza nk. Na yeyote popote katika utumishi wake atakapokwenda kinyume na maadili hukabiliwa na sheria za kijeshi, maana atakuwa ni mwanajeshi kimsingi na maslahi yao hayana ubaguzi.