Huko CCP sasa hivi kunamafunzo mapya?
![]()
![]()
Mwalimu mmoja wa shule ya sekondari kitulo wilayani makete aliyefahamika kwa jina la casto sote kawamba ameuawa kwa kupigwa risasi na askari wa jeshi la polisi Makete
Akizungumza na mtandao huu wawww.francisgodwin.blogspot.com mkuu wa polisi wilaya ya Makete SP Peter Kaiza kuhusu tukio hilo lililotokea eneo la benki ya NMB tawi la Makete jana majira ya saa moja na robo alisema kuwa mwalimu huyo alikuwa anakwenda kupata huduma za kibenki kupitia mashine ya kutolea pesa ya ATM akiwa na pikipiki ndipo alipo uwawa na askari mmoja aitwae Jose Msukuma na kukutwa na umauti huo .
Inadaiwa kuwa kisa cha mauwaji yake ni madai kutovaa kofia hiyo na baada ya kuitwa na askari hao alikaidi amri na kutaka kumgonga askari huyo aliye kuwa lindo.
Nae mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Makete Idd Nganya ambaye ndie mwajiri wa marehemu amesema kuwa mwili wa marehemu bado umehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya makete wakati utaratibu wakusafirisha mwili huo kwenda kwao mbeya kwa ajili ya mazishi ukiendelea
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye jina lake limehifadhiwa amesema kuwa askari hao walikuwa wakiomba fedha kwa mwalimu huyo na baada ya kukataliwa ndipo walipo anza kumshushia kichapo na alipo wazidi walilazimka kutumi asilaha na kumpiga begani kwa risasi
Walimu wenzake na marehemu ambao walifika hospitali kujua kuhusina na kifo cha mwalimu mwenzake wameeleza kusikitishwa na tukio hilo na kulifananisha na tukio la kikatili machoni pao.
Mganga mkuu mfawidhi ambaye ni msemaji wa hospitali ya wilaya ya makete Dr Michael Gulaka amesema kuwa wao walipokea mwili wa marehemu na sio majeruhi.
[TABLE="align: center"]![]()
[TR]
[TD]Askari wa FFU mkoani Iringa wakimwadhibu kwa kipigo
aliyekuwa mwandishi wa Chanel Ten mkoa wa Iringa
marehemu Daudi Mwangosi (wa pili kushoto) kabla ya
kuuwawa kwa bomu septemba 2 mwaka 2012 katika
kijiji cha Nyololo Mufindi.(picha na maktaba ya mtandao huu)
[/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
.....................................................................................................................................................................
WAKATI mtuhumiwa wa mauwaji ya aliyekuwa mwandishi wa kituo cha runinga cha Chanel Ten mkoani Iringa Daudi Mwangosi Daudi Mwangos, askari wa FFU mwenye namba G2573 Pasificus Cleophace Simoni (23) akitarajiwa kufikishwa tena mahakamani leo kwa kesi hiyo kutajwa ,askari wilaya ya Makete mkoa wa Njombe wadaiwa kufanya mauwaji ya kinyama kwa kumpiga mteja wa benki ya NMB kwa risasi. Huku askari askari mmoja nayetuhumiwa kufanya unyama huo akishikiliwa na jeshi la polisi kufuatia mauwaji hayo ya kinyama.
Tukio hilo limekuja huku bado watanzania hasa wakazi wa mikoa ya Iringa na Njombe wakiwa bado hawajasahau mauwaji ya kinyama yaliyomkuta mwanahabari Daudi Mwangosi ambapo kesi hiyo bado ikiendelea kutajwa na wanahabari waliokuwepo eneo la tukio siku ya mauwaji wakisubiri kuchukuliwa maelezo yao kama mashahidi wa kesi hiyo pindi itakapoanzwa kusikilizwa.
Mwandishi wa wetu wa mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com kutoka Makete Njombe anaeleza kuwa tukio hilo wamedai kuwa mauwaji hayo ya kinyama yametokea jana jumatano majira ya saa 1.20 usiku baada ya mteja huyo aliyekuwa na usafiri wa boda boda kufika eneo hilo la benki kwa lengo la kuchukua fedha .
Imedaiwa kuwa aliyepigwa risasi anatambuliwa kwa jina la Casto Kawambwa mkazi Mbalizi mkoani Mbeya na kuwa baada ya kupigwa risasi alikimbizwa katika Hospitali ya wilaya ya Makete ambako inadaiwa kabla ya kupatiwa matibabu amefariki dunia .
Kutokana na tukio hilo jeshi la polisi liliwazuia wanahabari kutimiza wajibu wao kwa kupiga picha wala kusogea eneo hilo la Hospitali na badala yake kuweka ulinzi mkali eneo hilo la Hospitali ili kuzuia wanahabari kusogea eneo hilo .
Hata hivyo mmoja kati ya askari ambae jina lake halikufahamika mara moja alisikika akidai kuwa chanzo cha mteja huyo wa benki kupigwa risasi alikuwa akihisiwa kuwa ni jambazi na hivyo baada ya kufika eneo hilo kwa usafiri wake wa piki piki (boda boda ) walihisi kuwa amefika kwa ajili ya kufanya vitendo vya uporaji katika benki hiyo na hivyo askari katika hali ya kujihamia aliamua kumpiga risasi .
Jitihada za kumtafuta kamanda wa polisi wa mkoa wa Njombe ili kuzungumzia undani wa tukio hilo linafanyika na mtandao huu.
Hisani ya Mzee wa Matukio daima
kwanza majambazi walio wengi ni Polisi!! Amini usiamini ndugu! Pia ndo wafadhili waku wa ujambazi!! Imeniuma sana!! R.I.P Mwalimu!!!hawa mapolisi wamekuwa hatari kuliko zaidi ya majambazi,R.I.P brother