BilioneaPATIGOO
JF-Expert Member
- Jun 23, 2012
- 12,320
- 11,345
Unatakiwa uhojiwe wewe, unajuaje yuko bujumburaZitto alishawahi kusema hamuogopi Magufuli anamuogopa Mungu tu,leo hii kajificha Bujumbura
Unatakiwa uhojiwe wewe, unajuaje yuko bujumburaZitto alishawahi kusema hamuogopi Magufuli anamuogopa Mungu tu,leo hii kajificha Bujumbura
Hizo ndio habari zinazotakiwa nowdays, marufuku kutumia zile 5W kwenye kazi ya uandishi. Andika utakaloambiwa.PERIODTaarifa hii ndo ipo kichochezi, kweli mtanzania halikuhoji yafuatayo!
1. Kwa hiyo alitoweka akaliacha gari?
2. Dereva walimkamata akiwa na gari ama wapi?
3. Wamemwachia kazi Dereva kumtafuta Zitto wao wafanye kazi gani?
3. Kama walilikamata gari na Dereva, kwa kumuachia Dereva, gari nalo wamemwachia?
Ndo, maana nikasema, taarifa hii ndio imekaa kichochezi!
Sikiliza kauli hii ya dereva juu ya kukamatwa kwa gari la Zitto.JESHI la Polisi Mkoa wa Shinyanga limemtaka Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ajisalimilishe kwa kupeleka vibali kuondoa utata wa gari alilokuwa akilitumia katika kampeni za uchaguzi mdogo uliofanyika Januari 22, mwaka huu wilayani Kahama.
Akizungumza na MTANZANIA jana, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Elias Mwita, alisema kiongozi huyo anasakwa kutokana kuwapo taarifa za intelijensia zinazoeleza alikuwa akitumia gari hiyo ambayo haikuwa na vibali.
Mwita alisema jeshi hilo linamtaka Zitto apeleke taarifa kuhusu gari analomiliki aina ya Toyota Land Cruiser V8 ambalo hakulitaja namba za usajili.
“Siku ya kufunga mkutano wa kampeni uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Isagehe wilayani Kahama, tulipata taarifa kwamba Kabwe anatumia gari ambalo si halali, halina vibali.
“Tukawa tumefikiria tumpate baada ya mkutano atupe maelezo kuhusu gari analolimiliki, lakini kabla hata hatujaonana naye, alitoweka,” alisema Mwita.
Alisema Jeshi la Polisi linamtaka kiongozi huyo wa ACT Wazalendo apeleke vibali vya gari hilo.
“Kwa hiyo sisi mpaka sasa Kabwe tunamtaka atuletee vibali vya gari hilo na ndiyo kitu ambacho sisi tunamuhitaji.
“Baada ya kuona gari hilo linachukua muda mrefu kwetu tulimkabidhi dereva wa gari hilo na kumtaka amtafute bosi wake atuletee vibali vya gari hilo,” alisema.
Chanzo: Mtanzania
Gari lina vibali tata, umelikamata, mwenyewe haonekani unaliachia kabla ya kuviona vibali vyake ujiridhishe, unaliachia kwanini?! Mwanzo wa series nyingine huu?!
Njia ya muongo ni fupi.Bora wangekaa kimya kuliko kujidharirisha
Kamanda alijuaje kama gari mmiliki wake ni Zitto na wakati kuna magari mengi? jamani Tz ni zaidi ya maigizo.
Heee..!
Na hilo gari lenye shida ya vibali mmeshaliachia kumbe..!??
I doubt kama hilo gari lina shida yoyote ya vibali...
Mbona mmeliachia??
Si ndio kosa lilipo..?? Unaliachia vipi gari.
Shida inaweza kuwa mlikuwa mnamtafuta ZZK kutokana na hotuba yake kwenye huu mkutano.. Au ndio mlikuwa mnahakikisha ulinzi wake kama wa Lowassa kule Geita??
Jeshi hili liache kutumika jamani.
Mnajidhalilisha sana kwa kweli.
Halafu wanaongea utadhan watz ni hatuna akili ..unamdanganya mtu mzima
Pumbavu kabisa,umewai kumiliki gari wewe,uliwai kusikia wapi mtu akitaka kununua gari polisi wanausika,iyo itakuwa bunduki,icho unachokiongelea ni baada ya gari kuanza kutumika,ni usalama wa gari,kuwa linakidhi utaratibu wa kutumika sio umiliki,iwapo mtu akanunua gari akaliweka gerage ao traffic vehicle inspection watakuja huko,kama watakuja ni kupekua kama wanaisi la wizi au la magumashi,hapa patakuwa na documents za TRA na wauzaji tu sio za polisi.
Pumbavu kabisa,umewai kumiliki gari wewe,uliwai kusikia wapi mtu akitaka kununua gari polisi wanausika,iyo itakuwa bunduki,icho unachokiongelea ni baada ya gari kuanza kutumika,ni usalama wa gari,kuwa linakidhi utaratibu wa kutumika sio umiliki,iwapo mtu akanunua gari akaliweka gerage ao traffic vehicle inspection watakuja huko,kama watakuja ni kupekua kama wanaisi la wizi au la magumashi,hapa patakuwa na documents za TRA na wauzaji tu sio za polisi.
Kama ni hivyo ....basi anaweza tuma muwakilishi....mwenye power of attorney....akamuwakilisha kuleta vibali....sio lazima awe yy kufika in person ...muwakilishi anatosha..labda kama kuna jingine
Hata kumsalimia anaweza akakutengeneza uwe dili lakeKumpangisha polisi katika nyumba yako ni kujichumia laana ya bure!