Polisi: Hatumsaki Zitto kwa uchochezi

Polisi: Hatumsaki Zitto kwa uchochezi

Mbona wanadhihirisha UJINGA wao kwa wananchi? Yani unaweza kwenda na difenda 5 kukamata gari lisilokua na vibali? Kama wewe ni mjinga usions wengine ni wajinga.
 
Kuna watu 7 wamekufa katika sandarusi,hakuna anayejali

Kuna kesi hazina majibu hadi leo , hakuna anayejali

Ujambazi umetamalaki hadi walinzi wanavamiwa na kuuwa. Hakuna anayejali

Hivi kweli Taifa hili halina kazi za kufanya kiasi cha kukimbizana na vibali vya gari.!

Kuna umasikini uliojaa miongoni mwa wananchi.
Kuna mambo ya maendeleo yanataka fikra

Leo hatuwezi kujenga std , Kenya wanamaliza.

Halafu kuna watu hawalali wakikimbizana na kadi za magari ambazo hazina maana yoyote

Hizi ndizo dalili za kufeli ! Yaani kama vile hakuna kazi za kufanya kabisa

Mambo ya aibu kila asubuhi, wakimaliza wanapitisha bakuli kuomba pesa za ujenzi wa miundo mbinu

Aibu sana hii nchi! Dah!
Inashangaza sana kuona mijitu inafurahia nakuusifia uongozi wa awamu hii. Aliyeturoga wa Tz keshakufa.
 
JESHI la Polisi Mkoa wa Shinyanga limemtaka Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ajisalimilishe kwa kupeleka vibali kuondoa utata wa gari alilokuwa akilitumia katika kampeni za uchaguzi mdogo uliofanyika Januari 22, mwaka huu wilayani Kahama.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Elias Mwita, alisema kiongozi huyo anasakwa kutokana kuwapo taarifa za intelijensia zinazoeleza alikuwa akitumia gari hiyo ambayo haikuwa na vibali.

Mwita alisema jeshi hilo linamtaka Zitto apeleke taarifa kuhusu gari analomiliki aina ya Toyota Land Cruiser V8 ambalo hakulitaja namba za usajili.

“Siku ya kufunga mkutano wa kampeni uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Isagehe wilayani Kahama, tulipata taarifa kwamba Kabwe anatumia gari ambalo si halali, halina vibali.

“Tukawa tumefikiria tumpate baada ya mkutano atupe maelezo kuhusu gari analolimiliki, lakini kabla hata hatujaonana naye, alitoweka,” alisema Mwita.

Alisema Jeshi la Polisi linamtaka kiongozi huyo wa ACT Wazalendo apeleke vibali vya gari hilo.

“Kwa hiyo sisi mpaka sasa Kabwe tunamtaka atuletee vibali vya gari hilo na ndiyo kitu ambacho sisi tunamuhitaji.

“Baada ya kuona gari hilo linachukua muda mrefu kwetu tulimkabidhi dereva wa gari hilo na kumtaka amtafute bosi wake atuletee vibali vya gari hilo,” alisema.


Chanzo: Mtanzania
Hii taarifa mbona kichekesho?
 
Mkuu jeshi la police ni Law enforcement agent. Kuna sheria imevunjwa hapo kama gari halina vibali halali. Ndio maana hao TRA wakienda kumkamata mtu anaesafirisha bidhaa za magendo wanaomba msaada wa jeshi la police. Sio kila jambo ni siasa.
Kama ni hivyo kwanini wameliachia gari? Si vema kuwaza kwa makalio.
 
Ukichunguza sana hawa polisi wameleta hii habari kuficha kitu. Wanaweza kuwa nae wanacheza na akili za watz tu
 
Ni yale yale tunayosema kila siku. Traffic police wanakamata gari likiwa halina vibali, lkn lina dereva wake. Kisha anatafutwa Zitto kuhojiwa? Kwa nn usimhoji dereva wa gari na kumwomba hivyo vibali? Kwani sheria za usalama barabarani zinasemaje umapokamata gari likiwa na makosa? Je inasema unamtafuta abiria au mmiliki wa gari au dereva wa gari?
 
Kama ni hivyo kwanini wameliachia gari? Si vema kuwaza kwa makalio.
Kwa hivyo ukitumia matusi ndio hoja yako inaeleweka vizuri au unasikika vizuri? Ukikua utaacha mambo ya kitoto. Au viroba ndio vinaongea?
 
JESHI la Polisi Mkoa wa Shinyanga limemtaka Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ajisalimilishe kwa kupeleka vibali kuondoa utata wa gari alilokuwa akilitumia katika kampeni za uchaguzi mdogo uliofanyika Januari 22, mwaka huu wilayani Kahama.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Elias Mwita, alisema kiongozi huyo anasakwa kutokana kuwapo taarifa za intelijensia zinazoeleza alikuwa akitumia gari hiyo ambayo haikuwa na vibali.

Mwita alisema jeshi hilo linamtaka Zitto apeleke taarifa kuhusu gari analomiliki aina ya Toyota Land Cruiser V8 ambalo hakulitaja namba za usajili.

“Siku ya kufunga mkutano wa kampeni uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Isagehe wilayani Kahama, tulipata taarifa kwamba Kabwe anatumia gari ambalo si halali, halina vibali.

“Tukawa tumefikiria tumpate baada ya mkutano atupe maelezo kuhusu gari analolimiliki, lakini kabla hata hatujaonana naye, alitoweka,” alisema Mwita.

Alisema Jeshi la Polisi linamtaka kiongozi huyo wa ACT Wazalendo apeleke vibali vya gari hilo.

“Kwa hiyo sisi mpaka sasa Kabwe tunamtaka atuletee vibali vya gari hilo na ndiyo kitu ambacho sisi tunamuhitaji.

“Baada ya kuona gari hilo linachukua muda mrefu kwetu tulimkabidhi dereva wa gari hilo na kumtaka amtafute bosi wake atuletee vibali vya gari hilo,” alisema.


Chanzo: Mtanzania
Hapo ndipo unaona tofauti ya wapiga midomo majukwaani wakitafuta wanaufyata. Nampigia Salute Mangi Meri Godbless Lema. haogopi kitu hakimbii.
 
Zito umefanya nini mpaka uwakimbie polisi!
 
Sijaona cha maana kwani kutokuwa na vibari ni kosa la dereva kuendesha gari lisilo na vibali na kama wanahitaji vibali sasa ulazima wa zito kupeleka uko wapi? na kama ni ishu ya kujua kama gari limelipiwa hakuna haja ya kulazimisha kuletwa kwa vibali kwani wanaweza kucheki online?. Na kama halikuwa na vibali waliachia la nini? inabidi taarifa zinazotolewa ziendane na uhalisia.
Bora wangekaa kimya mkuu
 
JESHI la Polisi Mkoa wa Shinyanga limemtaka Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ajisalimilishe kwa kupeleka vibali kuondoa utata wa gari alilokuwa akilitumia katika kampeni za uchaguzi mdogo uliofanyika Januari 22, mwaka huu wilayani Kahama.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Elias Mwita, alisema kiongozi huyo anasakwa kutokana kuwapo taarifa za intelijensia zinazoeleza alikuwa akitumia gari hiyo ambayo haikuwa na vibali.

Mwita alisema jeshi hilo linamtaka Zitto apeleke taarifa kuhusu gari analomiliki aina ya Toyota Land Cruiser V8 ambalo hakulitaja namba za usajili.

“Siku ya kufunga mkutano wa kampeni uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Isagehe wilayani Kahama, tulipata taarifa kwamba Kabwe anatumia gari ambalo si halali, halina vibali.

“Tukawa tumefikiria tumpate baada ya mkutano atupe maelezo kuhusu gari analolimiliki, lakini kabla hata hatujaonana naye, alitoweka,” alisema Mwita.

Alisema Jeshi la Polisi linamtaka kiongozi huyo wa ACT Wazalendo apeleke vibali vya gari hilo.

“Kwa hiyo sisi mpaka sasa Kabwe tunamtaka atuletee vibali vya gari hilo na ndiyo kitu ambacho sisi tunamuhitaji.

“Baada ya kuona gari hilo linachukua muda mrefu kwetu tulimkabidhi dereva wa gari hilo na kumtaka amtafute bosi wake atuletee vibali vya gari hilo,” alisema.


Chanzo: Mtanzania
Hata kutunga uongo hamjui maana mlishakabidhiwa hati zote za gari na dereva.

Kama mlimwachia dereva bila vibali ni wapuuzi tu na agenda yenu ya kukandamiza upinzani kwa maagizo toka juu
 
Heee..!

Na hilo gari lenye shida ya vibali mmeshaliachia kumbe..!??

I doubt kama hilo gari lina shida yoyote ya vibali...
Mbona mmeliachia??

Si ndio kosa lilipo..?? Unaliachia vipi gari.

Shida inaweza kuwa mlikuwa mnamtafuta ZZK kutokana na hotuba yake kwenye huu mkutano.. Au ndio mlikuwa mnahakikisha ulinzi wake kama wa Lowassa kule Geita??

Jeshi hili liache kutumika jamani.

Mnajidhalilisha sana kwa kweli.
Mkuu umeiweka vizuri tatizo jamaa hao wanadhani watz bado wajinga wajinga.... wanadhani hatuna uwezo wa kug'amua walitaka kufanya nn...

.
 
Mmejaa uwongo tu hamna zaidi, eti taarifa za kintelijensia mngekuwa mnaamtaarifa hizo msingekuwa mnaporwa silaha au kuuwawa hovyo na majambazi, mmekaa kutumika mtatumika sana awamu hii, mwisho wa siku namba tunasoma wote mtaani na nyumba zenu za full suti ya bati mkiwa ndani mchana jua linawaka kama mmewekwa kwenye oven
 
Back
Top Bottom