Kweli kabisa Mkuu.Mkuu umeiweka vizuri tatizo jamaa hao wanadhani watz bado wajinga wajinga.... wanadhani hatuna uwezo wa kug'amua walitaka kufanya nn...
.
Na kwa nini Rais aogopwe..tumechagua kwa kura nyingi ili atuhudumie sio kutishia MTU hata kama hajamchagua. Najua hakuna anayetishiwa na Mh. RAIS anafanya kazi kwa Sheria na Katiba kama Muongozo. Sipendi aogopewe Bali aheshimiwe na nadhani mwenyewe anapenda iwe hivyo.Zitto alishawahi kusema hamuogopi Magufuli anamuogopa Mungu tu,leo hii kajificha Bujumbura
Polisi wanasahau kwamba ni raia!Heee..!
Na hilo gari lenye shida ya vibali mmeshaliachia kumbe..!??
I doubt kama hilo gari lina shida yoyote ya vibali...
Mbona mmeliachia??
Si ndio kosa lilipo..?? Unaliachia vipi gari.
Shida inaweza kuwa mlikuwa mnamtafuta ZZK kutokana na hotuba yake kwenye huu mkutano.. Au ndio mlikuwa mnahakikisha ulinzi wake kama wa Lowassa kule Geita??
Jeshi hili liache kutumika jamani.
Mnajidhalilisha sana kwa kweli.
Zito umefanya nini mpaka uwakimbie polisi!
Hapana gari kama la wizi ni kazi ya polisi labda alilipata Arusha!!!Hivi uhalali wa vibali vya gari si ni kazi ya TRA, wanalijua hilo!? Ukweli (na haki) huinua taifa.
There you are, kwa hiyo wanaomtafuta ZZK ni traffic police au ni wa kitengo gani!?Huwezi ukapata document zote za gari TRA bila kupitia polisi.Kitengo cha traffic vehicle inspection
Nlitaka niulize pia!!!!!!kwahiyo dereva akipeleka vibali vya gari na kuvilipia kama vinaitaji kulipiwa zzk hamnashida naye tena?
Eti samahani jamani nikicheka naweza kuitwa mchochezi?[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]JESHI la Polisi Mkoa wa Shinyanga limemtaka Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ajisalimilishe kwa kupeleka vibali kuondoa utata wa gari alilokuwa akilitumia katika kampeni za uchaguzi mdogo uliofanyika Januari 22, mwaka huu wilayani Kahama.
Akizungumza na MTANZANIA jana, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Elias Mwita, alisema kiongozi huyo anasakwa kutokana kuwapo taarifa za intelijensia zinazoeleza alikuwa akitumia gari hiyo ambayo haikuwa na vibali.
Mwita alisema jeshi hilo linamtaka Zitto apeleke taarifa kuhusu gari analomiliki aina ya Toyota Land Cruiser V8 ambalo hakulitaja namba za usajili.
“Siku ya kufunga mkutano wa kampeni uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Isagehe wilayani Kahama, tulipata taarifa kwamba Kabwe anatumia gari ambalo si halali, halina vibali.
“Tukawa tumefikiria tumpate baada ya mkutano atupe maelezo kuhusu gari analolimiliki, lakini kabla hata hatujaonana naye, alitoweka,” alisema Mwita.
Alisema Jeshi la Polisi linamtaka kiongozi huyo wa ACT Wazalendo apeleke vibali vya gari hilo.
“Kwa hiyo sisi mpaka sasa Kabwe tunamtaka atuletee vibali vya gari hilo na ndiyo kitu ambacho sisi tunamuhitaji.
“Baada ya kuona gari hilo linachukua muda mrefu kwetu tulimkabidhi dereva wa gari hilo na kumtaka amtafute bosi wake atuletee vibali vya gari hilo,” alisema.
Chanzo: Mtanzania
Halafu wanaongea utadhan watz ni hatuna akili ..unamdanganya mtu mzimaKamanda alijuaje kama gari mmiliki wake ni Zitto na wakati kuna magari mengi? jamani Tz ni zaidi ya maigizo.
Kabisa mkuuIla bado kuna askari wenye uzalendo maana bila wao zito angeshatupwa kizuizini zamaniii