figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
Jeshi la Polisi limewahoji wachekeshaji wa Orijino Komedi kwa kosa la kuvaa nguo zinazoshabihiana na sare za Polisi.
Jeshi la Polisi Dar leo limewahoji wasanii wa Orijino Komedi makosa ya kuvaa sare za polisi kwenye harusi ya msanii mwenzao Emanuel Mgaya “Masanja”.
Wasanii hao, Lucas Muhuvile maarufu Joti, Alex John “Mac Reagan” na Isaya Gideon “Wakuvanga” wamehojiwa leo sambamba na meneja wa kundi hilo, Sekioni David.
Taarifa kutoka Jeshi la Polisi Dar zinaeleza kuwa wasanii hao walikamatwa tangu jana jioni na kulala kituo cha Polisi hadi walipohojiwa juu ya tukio hilo.