Rogart Ngaillo
JF-Expert Member
- Apr 27, 2013
- 899
- 1,887
Dar es Salaam.
Jeshi la Polisi Dar leo
limewahoji wasanii wa Orijino Komedi kwa
makosa ya kuvaa sare za polisi kwenye
harusi ya msanii mwenzao Emanuel Mgaya
“Masanja”. Wasanii hao, Lucas Muhuvile maarufu Joti,
Alex John “Mac Reagan” na Isaya Gideon
“Wakuvanga” wamehojiwa leo sambamba
na meneja wa kundi hilo, Sekioni David. Taarifa kutoka Jeshi la Polisi Dar zinaeleza
kuwa wasanii hao walikamatwa tangu jana
jioni na kulala kituo cha Polisi hadi
walipohojiwa juu ya tukio hilo. Picha zilizosambaa kwenye mitandao ya
kijamii zinawaonesha wasanii hao wakiwa
wamevalia sare zinazofanana na zile za
Jeshi la Polisi wakiwa wanafanya gwaride,
kama ishara ya kumpa heshima mwenzao,
Emmanuel Mgaya “Masanja” aliyeachana na ukapera.
Source: Mwananchi
Jeshi la Polisi Dar leo
limewahoji wasanii wa Orijino Komedi kwa
makosa ya kuvaa sare za polisi kwenye
harusi ya msanii mwenzao Emanuel Mgaya
“Masanja”. Wasanii hao, Lucas Muhuvile maarufu Joti,
Alex John “Mac Reagan” na Isaya Gideon
“Wakuvanga” wamehojiwa leo sambamba
na meneja wa kundi hilo, Sekioni David. Taarifa kutoka Jeshi la Polisi Dar zinaeleza
kuwa wasanii hao walikamatwa tangu jana
jioni na kulala kituo cha Polisi hadi
walipohojiwa juu ya tukio hilo. Picha zilizosambaa kwenye mitandao ya
kijamii zinawaonesha wasanii hao wakiwa
wamevalia sare zinazofanana na zile za
Jeshi la Polisi wakiwa wanafanya gwaride,
kama ishara ya kumpa heshima mwenzao,
Emmanuel Mgaya “Masanja” aliyeachana na ukapera.
Source: Mwananchi