Polisi, bunduki Hanang ni za nini?

Polisi, bunduki Hanang ni za nini?

Huelewi kazi ya bunduki ya polisi kwenye maafa?

Njoo Dar upinduke na gari au daladala ipinduke vibaka hawahangaiki kuokoa majeruhi Wala kubeba maiti ni kupora tu na ku search mifukoni Hadi maiti kuchukua pochi Simu Hadi viatu ,nguo na chupi watauza kama mitumba.waweza Kuta daladala abiria wote wako uchi wa mnyama kuanzia walio wazima,majeruhi Hadi maiti polisi wakichelewa kuwahi na bunduki zao

Kama ni nyumba mfano imevamiwa na maji au moto vibaka watawahi kubeba Hadi magodoro ,Vitanda ,TV,makochi nk hata yawe yamejaa maji na kutokomea kusikojulikana

Wewe mleta mada ni kibaka mia Kwa mia ulitaka askari wasije na bunduki upore jambazi wewe

Askari wamekudhibiti
Mkuu vijana wa chadema wamefundishwa kupinga kila kitu. Hivyo wala usiwashangae
 
Acha uongo wewe ,kwanza mmesubiri maji yamepoa ndio mkafika eneo la tukio na mavitambi vyenu!

Nendeni shule wengi wenu hamna vyeti ,sehemu ya kutumia akili mnatumia maguvu! Panya road wamewashinda mtaweza maji yenye matope!

Nipo hapa madongo kuinama!
Haya majamaa ni yale yaliyozaliwa kwenye familia za kishenzi. Ustaarabu ni sifuri kabisa na bongo zao ni kama za punda. Tatizo kubwa la Tanzania ni kuwa likitokea janga kama hili viongozi hawaendi kusaidia chochote zaidi ya kujionyesha ili waonekane. Na hizo bunduki ni za kuwalinda kwani unajua tena watawala wetu popope walipo wanajiona kama hawapo salama.
 
Nilidhan vikosi vikazanie UOKOZI na kuwajengea makazi waathirika. Badala yake Ni mwendo wa kupiga picha na kuzunguka na Mabunduki.

NB:
Mmepanga kuua majeruhi Kwa hizo Bunduki?
kuna siku utakuja kuelewa.

hata vibaka huwa wanachukia sana polisi mpaka siku wapiga kura wakiwaweka kati,hutamani hata polisi mmoja apite.

wakati wa majanga vibaka na watu wenye nia ovu hutumia pia mwanya huo kujinufaisha,siku pinduka na gari au anguka kwenye piki piki,kuna watu watakusachi mpaka mifukoni.hapo tope linatembea na mapaa ya nyumba,kuna mtu anatafakari ataondokaje na cable ya umeme ya tanesco akauze kopa?

Sent from my Redmi Note 8 using JamiiForums mobile app
 
kuna siku utakuja kuelewa.

haya vibaka huwa wanachukia sana polisi mpaka siku wapiga kura wakiwaweka kati,hutamani hata polisi mmoja apite.

wakati wa majanga vibaka na watu wenye nia ovu hutumia pia mwanya huo kujinufaisha,siku pinduka na gari au anguka kwenye piki piki,kuna watu watakusachi mpaka mifukoni.hapo tope linatembea na mapaa ya nyumba,kuna mtu anatafakari ataondokaje na cable ya umeme ya tanesco akauze kopa?

Sent from my Redmi Note 8 using JamiiForums mobile app
Mali na uhai kipi muhimu? Au wanalinda tope na magome ya miti?
 
Uokozi huu wa kubeba bunduki utashangaza dunia. PRESS RELEASE zinataja idadi ya waliokufa kuliko waliopona
 
Umenikumbusha documentary moja ya JICHO PEVU. Nchini Kenya, baada ya magaidi wapatao 8 kuvamia mall moja maarufu na kuuwa raia kwa kuwafyatulia risasi ovyo ovyo ndipo kisanga kilianza.

Walienda makomandoo wapatao 6 kutoka Israel (maana inadaiwa mmiliki wa ile mall, mfano wa mlimani city alikuwa ni muisrael). Lengo lao waingie humo ndani na kuwakamata hao magaidi dead or alive. Serikali ya Kenya ikawazuia.

Cha kushangaza kikaja kikosi cha wanajeshi wapatao 100 na mabunduki, mabomu, mizinga na vifaru kufanya hiyo operation. Waliishia kulipua na kuharibu jengo, walivunja ATM mashine ili waibe hela, wakavunja Mcdonald na kuiba kuku na pizzas. Kiufupi walitia aibu taifa na hawakumpata hata gaidi mmoja. Kuficha aibu wakaenda kumkamata mama mmoja mjane wa kisomali kwa jina la 'white widow' ndiye muhusika wa lile shambulio.

Ile documentary ilileta utata mpaka kupelekea mwanahabari kukimbia nchi. Naamini itakuwepo YouTube.
 
Back
Top Bottom