Polisi apigwa risasi na kufa

Mambo ya kawaida binadamu kufa, mungu ndiyo kampangia afe kwa njia hiyo, nimeona kuna watu fulani humu wanataka kulikuza hili suala na kulifanya la kisiasa zaidi, mimi naomba tusiende huko. huwezi kujua sababu ya kuuliwa, labda alikuwa akichukua mke wa mtu, labda alikuwa akishirikiana kwenye biashara za magendo, labda labda, labda!...hakuna jibu hapa jibu lililobaki ni labda tu, hili suala tuwaachie wahusika.
 
Mimi niko Arusha, habari tulizozipata ni kwamba wale walikuwa ni majambazi na wameiba kwenye duka la jirani na pale idara ya maji. Wakiwa wanaondoka wakamwona askari na wakahisi anaweza kuwadhuru, kujiwahi wakaamua kumpiga risasi. Yule askari alikuwa akisubili wenzake ambao pia walikuwa wapo ndani ya duka jirani na hapo.
 
wakuu....hii story ya kupigwa risasi polisi nilivyosikia ni kwamba kuna majambazi yamemliza mfanyabiashara kiasi cha pesa ambacho mpaka sasa hakijajulikana.....mfanyabiashara huyo alikuwa anaenda kuweka pesa hizo CRDB bank pale uhuru road, wachizi wakamtokea, walipokuwa wapo njiani kukimbia wakakutana na huyo polisi hana hili wala lile katoka duka la hardware kununua anachojua mwenyewe.....wanaume wakajua huyu ni nuksi wakamuwahi.....kwa hiyo polisi amekufa bila kujua kilichomuua ni nini.....huku nyuma majambazi hao wakimuacha yule baba mfanyabiashara akilia barabarani kama mtoto mdogo.....kweli pesa ni maua....hunyauka na kuchanua
 
Wana JF polisi mmoja akiwa katika uniform amepigwa risasi hadi kufa maeneo ya Arusha chini ya mti karibu na stand ya magari ya kwenda Kisongo, Kwamrombo.
Ilikuja gari aina ya RA4 ikiwa imewasha taa kisha baadhi ya magari yakapisha wakijua labda ilikuwa na dharura, lakini walipofika alipokuwa askari huyo alipokaa basi alishuka jamaa mmoja na kumpiga risasi kwa bastola kisha kuingia ndani ya gari na kutokomea kusikojulikana.
Hadi napost thread hakuna habari za kukamatwa kwa jamaa hao ambao haikujulikana walikuwa majambazi au walikuwa na visasi nae marehemu.

Duh this is damn serious! Kama taifa kuna haja ya kurudisha heshima ya Taifa. Sidhani kama wachakachuaji wa kura wana confidence ya kuliaddress!
 
Unajua jamani kuweni wakweli na binadamu,inakuwaje mtu anapigwa risasi wengi mnafurahia?kwanza taarifa za mtoa topic si zakweli na kasha ataumbuka kwani habari za polisi kupigwa risasi ni kweli ila kafa,au la,kapigwa na majambazi au wafuasi wenye kulipa kisasi......sikweli,kasho mtajua unwell na ushabiki wa namna hii simzuri na inaonyesha kutokomaa.Majambazi watasherekea nakesho wanahamia kwako sijui utasema nao wanalipa kisasi!!!!!!!
 
wakuu....hii story ya kupigwa risasi polisi nilivyosikia ni kwamba kuna majambazi yamemliza mfanyabiashara kiasi cha pesa ambacho mpaka sasa hakijajulikana.....mfanyabiashara huyo alikuwa anaenda kuweka pesa hizo CRDB bank pale uhuru road, wachizi wakamtokea, walipokuwa wapo njiani kukimbia wakakutana na huyo polisi hana hili wala lile katoka duka la hardware kununua anachojua mwenyewe.....wanaume wakajua huyu ni nuksi wakamuwahi.....kwa hiyo polisi amekufa bila kujua kilichomuua ni nini.....huku nyuma majambazi hao wakimuacha yule baba mfanyabiashara akilia barabarani kama mtoto mdogo.....kweli pesa ni maua....hunyauka na kuchanua

ooho..sasa walokua wanashabikia labda watuambie ni majambazi wa chama gani walioua
 
RIP police aliyeuawa and poleni wafiwa. Hakuna kitu kibaya kama kifo jamani. Sisi wote ni binadamu na sioni sababu yoyoye inayotufanya tufurahie kifo cha binadamu mwenzetu. Whether or not ni polisi aliyeuawa budo ni binadamu kama sisi. Whether ameauwa na majambazi or watu waliokuwa na kisasi, still ni binadamu kama sisi. Who knows, the next target will be you?
 
Rest-in-Peace kamanda. Pole kwa wafiwa.

Je hii haina uhusiano na polisi walivyowaua watu siku ya maandamano Arusha?

Isije ikawa ni tit-for-tat.
 
When a system in equilibrium is subjected to a change,the system will also try to change so as to halt the effect of that changes until stability is re-attained.Tazama Iraq,Afghanistan etc

Masika,

Uliyoisema
mkuu ni Le Chatelier's principle of equilibrium kwa lugha ya kikemia hasa ina sema hivi ''when a system in chemical equilibrium is disturbed by a change of temperature, pressure, or a concentration, the system shifts in equilibrium composition in a way that tends to counteract this change of variable''.

Lakini pia Sir Isaac Newton katika ile sheria ya tatu inayotawala vitu kwenye mwendo (Newton's 3rd law of motion) inasema hivi, ''For every action there is an equal and opposite re-action' kwa maneno mengine ni kwamba unaposukuma pia na wewe utasukumwa.

Precisely
This means that for every force there is a reaction force that is equal in size, but opposite in direction. That is to say that whenever an object pushes another object it gets pushed back in the opposite direction equally hard.

Hii ni nature inafanya kazi kila mahali. Siungi mkono na wala sifurahii mauaji na kama wengine wanavosema hatujui kisa cha mauji. Lakini nina uhakika na sheria hizi za asili. Ukitenda utatendwa pia. Viongozi wetu lazima waelewe ukiua kwa upanga utauwa kwa upanga pia. Arusha itakuja kulipa tu siku moja. Kumnyoshea mwanadamu mwenzako bunduki na kumuua kama mbwa kichaa ilihali wewe una nguvu na uwezo wote wa kumthibiti na wakati huo huo mwenzio hana silaha nzito kama za kwako - italipa tu siku moja.

Said Mwema hatakaa apumzike maisha yake yote na wale wote waliotekeleza amri hiyo. Rais naye hatakuwa salama kama mwenzake asivo salama hadi sasa hivi. Mwinyi aligombana na sisi tukiwa wanafunzi hakutuua japo alikuwa anaweza kufanya hivo, leo Jk na SM wanaua vijana wetu, halafu Waziri mkuu anawapongeza polisi. INANIUMA SANA.

Cain wa Biblia kitabu cha mwanzo aliua mdogo wake, Mungu akimwambia damu ya nduguyo inaninilia. Mungu leo anawaambia JK na SM damu za Watanzania wale wawili na mgeni jirani yetu kutoka Kenya zinawalilia. Hawatakwepa hizo sheria hizo mbili hapo juu.
 
Mambo ya kawaida binadamu kufa, mungu ndiyo kampangia afe kwa njia hiyo, nimeona kuna watu fulani humu wanataka kulikuza hili suala na kulifanya la kisiasa zaidi, mimi naomba tusiende huko. huwezi kujua sababu ya kuuliwa, labda alikuwa akichukua mke wa mtu, labda alikuwa akishirikiana kwenye biashara za magendo, labda labda, labda!...hakuna jibu hapa jibu lililobaki ni labda tu, hili suala tuwaachie wahusika.

Sio kila kifo kinapangwa na Mungu mkuu!!
 
Hakuna namna tunaweza kushangilia mtu kuua mtu mwingine. Ila jamani kuna kazi tuzifanye kwa uadilifu kama tunataka kufika mbali. Dhuluma na ujanja ujanja wengine wanatoa adhabu hapa hapa hawasubiri kesho ahela.
 
ndo hivyo mkuu cdm wasiiingizwe tusiendelee kutoa majibu mepesi kwenye maswali magumu!

Mimi bado nipo palepale kuwa mauaji ya raia wasio na hatia yalaaniwe. Kwa yeyote atakayekuja na propaganda za kisiasa kwenye hili naye alaaniwe laana saba mara sabini. Ninajua kutakuwa na pea heads watakaoona kuwa kuna haja ya kulihusisha tukio hili na siasa ili kutimiza matakwa yao, nao wajue kuwa moto hauzimwi kwa mafuta.

Na wakifika huko watakuwa wanazidi kuonesha ni jinsi gani vyombo vya dola visivyofanya kazi zake kisayansi bali kwa hisia na ushabiki. No spin on this event kwani no facts on the table about the real motive of a killer no right to speculate. Otherwise we have to condemn these types of actions because they don't reflect our culture and attitude as Tanzanians, but those in power should read the minds and will of the people as they reflect a cultural shift from tolerance to intolerance which shows that people are fed up from the way they run the country. You can not rule by iron fist its time to use democracy as a weapon to calm people and reject the intimidation tactics.
 
Ukiangalia furaha za watu hapa JF kwa POLISI kupigwa Risasi, zinaleta picha moja kubwa sana kuwa kati ya RAIA wa Tanzania na POLISI, kuna uhasama mkubwa sana.

Waziri wa Mambo ya ndani na Wema kama wangelikuwa Mbayuwayu, ingelibidi wafanye kazi ya ziada kurekebisha hili swala.

Mwanzo nilifikiri Wachaga wameanza kulipa kisasi kwa ndugu zao kadhaa hadi leo kupigwa Risasi Arusha.

Yakija ya Egypt, Tanzania kweli itawaka moto maana watu wakija kuwakamata Polisi hasa Arusha, Kilimanjaro, Mbeya na Mwanza, kwa kweli watapiga kama vibaka. Nina wasiwasi Egypt ya Tanzania itakuwa mbaya zaidi na kumwaga damu kwingi maana Tanzania kila mtu anajifanyia kazi apendwavyo.

RIP POLIS, RIP Watanzania wote waliouawa au kufa bila sababu ya msingi.
 
wakuu....hii story ya kupigwa risasi polisi nilivyosikia ni kwamba kuna majambazi yamemliza mfanyabiashara kiasi cha pesa ambacho mpaka sasa hakijajulikana.....mfanyabiashara huyo alikuwa anaenda kuweka pesa hizo CRDB bank pale uhuru road, wachizi wakamtokea, walipokuwa wapo njiani kukimbia wakakutana na huyo polisi hana hili wala lile katoka duka la hardware kununua anachojua mwenyewe.....wanaume wakajua huyu ni nuksi wakamuwahi.....kwa hiyo polisi amekufa bila kujua kilichomuua ni nini.....huku nyuma majambazi hao wakimuacha yule baba mfanyabiashara akilia barabarani kama mtoto mdogo.....kweli pesa ni maua....hunyauka na kuchanua
Umegundua eeeh! Afadhali hela yangu nikainywe sasa hivi kuliko kufikiri itajaa halafu watu wakaichukua kama yao siku moja.
 
Duh! hii mbona polisi wenzake hawakupata habari za kiinteligensia kuwa askari wao atauliwa????????
Wao ni habari za CDM tu ndo wnapata. :clap2:
 
Mimi niko Arusha, habari tulizozipata ni kwamba wale walikuwa ni majambazi na wameiba kwenye duka la jirani na pale idara ya maji. Wakiwa wanaondoka wakamwona askari na wakahisi anaweza kuwadhuru, kujiwahi wakaamua kumpiga risasi. Yule askari alikuwa akisubili wenzake ambao pia walikuwa wapo ndani ya duka jirani na hapo.

This is developing story if it is true. Maoni mengi yaliyotolewa humu yameona the bitterness between people and our police forces. Lets take these comments seriously that Mwema needs to do something to clear a negative image created by his front liners on the public.
 
Back
Top Bottom