Joshua justine
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 792
- 1,007
Nawasalimu wadau wote wa jukwaa hili; ninaomba tushirikiane kwa pamoja kuangalia jambo hili kutoka pande mbalimbali na kuona kama linaweza kuwa ni uamuzi sahihi kwa majira haya ambayo taifa letu limefikia sasa.
Wote tunakubaliana kuwa kila jambo huwa na mwisho wake na historia inajengwa na matukio. Huwezi kupingana na uhalisia halisi pale matukio yanapokuwa yakijenga historia, tumeona falme zilivyoinuka zikafika kileleni zikang'ara na zikaporomoka muda wake ulipoisha, na ni matukio ndio yamesababisha, cause and effect. Uingereza iliwika ikaja marekani na sasa mchina anatake over mbele ya macho ya ulimwengu mzima na hakuna awezaye kuzuia hata mmarekani mwenyewe anafurukuta tu, kwa sababu yameshafanywa matukio na mmarekani mwenyewe na wenzzie yanayosababisha hayo, hivyo hawezi tena kuzuia.
Tanzania tunapotimiza miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika kuna mambo mengi yametokea katika historia ya siasa yetu. Ni kitabu kizima unaweza kujaza matukio hayo yakiwemo ya ufisadi, vifo vya viongozi wema kama hayati sokoine, n.k na hayajaacha kutokea mpk kesho! Wote tunakumbuka viongozi kama Nyerere alipokuwepo alivyolazimika kuwa anakemea mpaka watawala kama watoto wadogo wasiojua nin wanafanya, tumeona hayati Magufuli nae alijaribu kukemea na kuwaadhibu pia, leo hii watu hao wa kukemea na kuwafunga kengele viongozi waovu wote wamekwenda zao, je taifa litaelekea wapi wale mbwa wakifunguliwa?
Tunaona watu kama Polepole wanavyojaribu kuongea lakini wote tunajua na hata yy mwenyewe amekiri mara nyingi kujaribu kutishwa na wengine ndani yachama ili asiongee, je ameongea lipi baya la kutaka kumfunga mdomo?
Ni wazi chama cha mapinduzi sasa kimepoteza legitimacy ya kutawala nchi rasmi! Kwani yote yanayofanyika humo ni kinyume na misingi ya siasa za nchi yetu na siasa za chama hicho chenyewe ambavyo vyote pamoja viliwekwa na waasisi wa taifa letu mwanzoni kabisa. Ni matukio mengi yametokea na leo ni ukomavu wa matukio hayo tu, huwezi kusema eti bado tukipe nafasi utakuwa hujuihistoria vizuri wewe, maaana ikifika ukomavu wa matukio historia inadai mabadiriko na utake usitake yatakuja tu hata ulie, ugalegale , no way!
Chama cha mapinduzi ndani yake chembe za watu wasafi zimebaki chache kuliko walio waovu, na tunaona wanavyokuja kwa nguvu mpaka raia wote wamejikatia tamaa kabisa. Sasa kuibuka tena mtu mzalendo na kufanya miujiza aliyofanya hayati Magufuli ndani ya chama hicho ni ndoto isiyowezekana.
TUFANYAJE
Wazalendo waliobaki ndani ya chama hicho mkubali matokeo, (ngumu kumeza), lakini ni wakati wa nyinyi kuja na CHAMA KIPYA CHA SIASA NCHI HII.
Najua mtasema kuwa kuna vyama vingi vimeshindwa, lakini napenda kuwakumbusha kuwa kila tukio lina right timing yake, umri wa CCM ulikuwa haujaisha wakati Mkapa, Magufuli na wengine bado wapo hai, maana chama kilifikia hatua waatu hawaiogopi katiba yao bali wanaogopa viongozi wakali waliopo, sasa hawapo, je niambie nani ni , "BABA NDANI YA CHAMA HICHO SASA, NA ANA SIFA GANI?"
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa CCM sio mama yake, je nyie mlioikuta tu mnajifanya CCM ni zaidi ya mama zenu?
NI UKWELI KUWA UPINZANI SAHIHI UTAKAOSHIKA NCHI HII UNAPASWA UTOKEE NDANI YA CCM KWA SABABU ZIFUATAZO:
JE, hakuna mpasuko humo ndani ya chama hata sasa watu wanagombaniana vyeo na mali humo?
Historia hakuna wa kushindana nayo, mkiogopa kuanzisha chama jambo ambalo sio dhambi kikatiba ipo siku raia watachoka na risasi ya kwanza itakaporushwa katika tukio lolote lile hapohapo ndipo mafuriko yatakapopasulia njia (MARK MY WORDS)
SUGGESTED READINGS;
*Mwili umekosa kichwa ( jukwaa la siasa)
*Hili liwe funzo: tudai katiba bora zaidi (maboresho) - jukwaa la katiba mpya.
Tuepuke mawazo mgando, CCM milele, sio Mungu CCM, inaweza anguka pia kama marekani, kama zambia!
Wote tunakubaliana kuwa kila jambo huwa na mwisho wake na historia inajengwa na matukio. Huwezi kupingana na uhalisia halisi pale matukio yanapokuwa yakijenga historia, tumeona falme zilivyoinuka zikafika kileleni zikang'ara na zikaporomoka muda wake ulipoisha, na ni matukio ndio yamesababisha, cause and effect. Uingereza iliwika ikaja marekani na sasa mchina anatake over mbele ya macho ya ulimwengu mzima na hakuna awezaye kuzuia hata mmarekani mwenyewe anafurukuta tu, kwa sababu yameshafanywa matukio na mmarekani mwenyewe na wenzzie yanayosababisha hayo, hivyo hawezi tena kuzuia.
Tanzania tunapotimiza miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika kuna mambo mengi yametokea katika historia ya siasa yetu. Ni kitabu kizima unaweza kujaza matukio hayo yakiwemo ya ufisadi, vifo vya viongozi wema kama hayati sokoine, n.k na hayajaacha kutokea mpk kesho! Wote tunakumbuka viongozi kama Nyerere alipokuwepo alivyolazimika kuwa anakemea mpaka watawala kama watoto wadogo wasiojua nin wanafanya, tumeona hayati Magufuli nae alijaribu kukemea na kuwaadhibu pia, leo hii watu hao wa kukemea na kuwafunga kengele viongozi waovu wote wamekwenda zao, je taifa litaelekea wapi wale mbwa wakifunguliwa?
Tunaona watu kama Polepole wanavyojaribu kuongea lakini wote tunajua na hata yy mwenyewe amekiri mara nyingi kujaribu kutishwa na wengine ndani yachama ili asiongee, je ameongea lipi baya la kutaka kumfunga mdomo?
Ni wazi chama cha mapinduzi sasa kimepoteza legitimacy ya kutawala nchi rasmi! Kwani yote yanayofanyika humo ni kinyume na misingi ya siasa za nchi yetu na siasa za chama hicho chenyewe ambavyo vyote pamoja viliwekwa na waasisi wa taifa letu mwanzoni kabisa. Ni matukio mengi yametokea na leo ni ukomavu wa matukio hayo tu, huwezi kusema eti bado tukipe nafasi utakuwa hujuihistoria vizuri wewe, maaana ikifika ukomavu wa matukio historia inadai mabadiriko na utake usitake yatakuja tu hata ulie, ugalegale , no way!
Chama cha mapinduzi ndani yake chembe za watu wasafi zimebaki chache kuliko walio waovu, na tunaona wanavyokuja kwa nguvu mpaka raia wote wamejikatia tamaa kabisa. Sasa kuibuka tena mtu mzalendo na kufanya miujiza aliyofanya hayati Magufuli ndani ya chama hicho ni ndoto isiyowezekana.
TUFANYAJE
Wazalendo waliobaki ndani ya chama hicho mkubali matokeo, (ngumu kumeza), lakini ni wakati wa nyinyi kuja na CHAMA KIPYA CHA SIASA NCHI HII.
Najua mtasema kuwa kuna vyama vingi vimeshindwa, lakini napenda kuwakumbusha kuwa kila tukio lina right timing yake, umri wa CCM ulikuwa haujaisha wakati Mkapa, Magufuli na wengine bado wapo hai, maana chama kilifikia hatua waatu hawaiogopi katiba yao bali wanaogopa viongozi wakali waliopo, sasa hawapo, je niambie nani ni , "BABA NDANI YA CHAMA HICHO SASA, NA ANA SIFA GANI?"
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa CCM sio mama yake, je nyie mlioikuta tu mnajifanya CCM ni zaidi ya mama zenu?
NI UKWELI KUWA UPINZANI SAHIHI UTAKAOSHIKA NCHI HII UNAPASWA UTOKEE NDANI YA CCM KWA SABABU ZIFUATAZO:
- Viongozi watakaounda chama kipya watakuwa wana uzoefu mzuri wa siasa ya nchi yetu na misingi yake iliyowekwa na waasisi hivyo wataanzisha chama kinachokuja kurudisha uzalendo upya bila kuiasi misingi ya taifa (ni lazima wakubali kutoka na yale mema CCM, maana hayo ni ya waasisi na wananchi sio ya hao mafisadi watakaobaki humo)
- Kwakuwa watakuwa ni watu walewale (ila wazalendo), hawatakuwa na kazi kubwa kufikia matawi yote na mashina yote nchi nzima kwani CCM itapasuka juu mpaka chini kama pazia la hekalu, hii itawarahisiahia kuwa tayari wakati uchaguzi utakapofika 2025, jambo hilo ni tofauti iliyosababisha vyama kama Chadema kushindwa kuchukua madaraka kwa urahisi.
- Ni chama kipya ndio kutoka CCM ndio kitawezesha kuwe na power check na power balance ya ukweli katika taifa hili itakayorudisha nguvu ya kura ya raia na hivyo kuimarisha ama kurudisha demokrasia ya ukweli kwenye taifa letu.
- Ni chama kipya kutoka CCM ndio kitawezesha kuandikwa katiba mpya ya wananchi katika taifa hili( kubotesha katiba iwe ya wananchi zaidi)
JE, hakuna mpasuko humo ndani ya chama hata sasa watu wanagombaniana vyeo na mali humo?
Historia hakuna wa kushindana nayo, mkiogopa kuanzisha chama jambo ambalo sio dhambi kikatiba ipo siku raia watachoka na risasi ya kwanza itakaporushwa katika tukio lolote lile hapohapo ndipo mafuriko yatakapopasulia njia (MARK MY WORDS)
SUGGESTED READINGS;
*Mwili umekosa kichwa ( jukwaa la siasa)
*Hili liwe funzo: tudai katiba bora zaidi (maboresho) - jukwaa la katiba mpya.
- Serikali na mwarobaini wa matatizo yetu (Jukwaa la siasa)
- Ukweli mchungu, ngumu lakini ndivyo ilivo ( jukwaa la siasa)
Tuepuke mawazo mgando, CCM milele, sio Mungu CCM, inaweza anguka pia kama marekani, kama zambia!