Polepole kazungumza, J.Makamba Je!

Polepole kazungumza, J.Makamba Je!

Kalamu

Platinum Member
Joined
Nov 26, 2006
Posts
19,495
Reaction score
26,120
Nilianza kumfahamu (au kumjuwa?), kijana Januari Makamba kupitia kwenye jukwaa hili hili la JF, kwa kusoma barua yake aliyoipa kichwa cha habari cha "Coming to America".
Andiko lake lile lilinivutia, kwa vile maelezo yake yalionyesha kuwa kijana mwenye uzalendo wa nchi yetu Tanzania.

Historia inaonyesha kwamba baada ya hapo amepitia kwenye mikanganyiko mingi, kiasikwamba hata ule uzalendo uliokuwa unajitokeza kwenye barua ile haukuweza kuonekana tena.

kinachonifanya nimkumbuke sasa huyu kijana ni tukio hili la hivi karibuni ambalo Polepole (kijana mwingine) ambaye historia yake haipishani sana na ya huyu Makamba kuamua kulipuka na kudai maslahi ya nchi yake kuwa muhimu zaidi ya chama kinachowanufaisha wao binafsi na watu wao wa karibu.

Sasa namsihi Januari Makamba ajitokeze mbele awaeleze waTanzania kinagaubaga; ile kazi ya kuhesabu kura za ushindi wa CCM mwaka 2015 aliyoisimamia yeye na yule mwenzake aliyempachika Tanesco alipoukwaa uwaziri wa Nishati ilihusika na nini hasa?
Ndiyo haya aliyo yaeleza Polepole?

Januari, ulipo simama sasa hivi, ni fursa nzuri kabisa ya kujirudi na kulikumbuka lile andiko lako uliloliweka kwenye ile barua yako ya "Comimg to America".

Please, do the right thing for your country, which is in a worse situation than it has ever been before.
 
Ili wammalizie 😂😂😂 hamphley anaongelea sijui wapi makamba hapo bumbuli patageuzwa Kosovo🫣🫣🫣 akatafute mahali apumzike Bado ana nguvu za kufanya kazi ana elimu ya kumtosha kama.vipi aachane na ccm aendelee na mambo mengine KULIKO kudhalilija Kila uchao
 
Nilianza kumfahamu (au kumjuwa?), kijana Januari Makamba kupitia kwenye jukwaa hili hili la JF, kwa kusoma barua yake aliyoipa kichwa cha habari cha "Coming to America".
Andiko lake lile lilinivutia, kwa vile maelezo yake yalionyesha kuwa kijana mwenye uzalendo wa nchi yetu Tanzania.

Historia inaonyesha kwamba baada ya hapo amepitia kwenye mikanganyiko mingi, kiasikwamba hata ule uzalendo uliokuwa unajitokeza kwenye barua ile haukuweza kuonekana tena.

kinachonifanya nimkumbuke sasa huyu kijana ni tukio hili la hivi karibuni ambalo Polepole (kijana mwingine) ambaye historia yake haipishani sana na ya huyu Makamba kuamua kulipuka na kudai maslahi ya nchi yake kuwa muhimu zaidi ya chama kinachowanufaisha wao binafsi na watu wao wa karibu.

Sasa namsihi Januari Makamba ajitokeze mbele awaeleze waTanzania kinagaubaga; ile kazi ya kuhesabu kura za ushindi wa CCM mwaka 2015 aliyoisimamia yeye na yule mwenzake aliyempachika Tanesco alipoukwaa uwaziri wa Nishati ilihusika na nini hasa?
Ndiyo haya aliyo yaeleza Polepole?

Januari, ulipo simama sasa hivi, ni fursa nzuri kabisa ya kujirudi na kulikumbuka lile andiko lako uliloliweka kwenye ile barua yako ya "Comimg to America".

Please, do the right thing for your country, which is in a worse situation than it has ever been before.
Hawezi kuongea hayo unayotaka. Polepole ameamua kujitoa sadaka, January bado ana uroho au hamu ya madaraka ambapo akianza kuingia "kajificheni" kama Polepole kisha ayazungumze hayo means mambo ya madaraka ndio basi tena
 
Hawezi kuongea hayo unayotaka. Polepole ameamua kujitoa sadaka, January bado ana uroho au hamu ya madaraka ambapo akianza kjuingia "kajificheni" kama Polepole kisha ayazungumze hayo means mambo ya madaraka ndio basi tena
Unaweza kuwa sahihi kabisa juu ya "uroho wa madaraka", na unufaika anaotegemea kuendelea kuupata kwa kunyamazia maovu yanayotendwa dhidi ya Tanzania.
Mimi namkumbushia tu, ule msukumo uliomfanya aandike ile barua iliyoonekana kuwa ilitoka ndani ya moyo wake kwelikweli kuhusu taifa lake la Tanzania.
Kama mtanzanzania; bado sioni sababu ya kumkatia tamaa juu ya uzalendo wake juu ya nchi hii.

Je, wewe ulitegemea kuwa mtu kama Polepole angezungumza aliyoyasema hadi sasa!
 
Unaweza kuwa sahihi kabisa juu ya "uroho wa madaraka", na unufaika anaotegemea kuendelea kuupata kwa kunyamazia maovu yanayotendwa dhidi ya Tanzania.
Mimi namkumbushia tu, ule msukumo uliomfanya aandike ile barua iliyoonekana kuwa ilitoka ndani ya moyo wake kwelikweli kuhusu taifa lake la Tanzania.
Kama mtanzanzania; bado sioni sababu ya kumkatia tamaa juu ya uzalendo wake juu ya nchi hii.

Je, wewe ulitegemea kuwa mtu kama Polepole angezungumza aliyoyasema hadi sasa!
Unajua huyu jamaa nae ana mabaya yake ambayo wakiamua ku deal nayo hachomoki. Ukwasi alio nao ni questionable so ni heri aendelee kubaki na alicho nacho hata kama sio cha halali kuliko achokoze vilivyolala waamke nae
 
Hahahahaha Kwa hiyo JM akianza naye kutuma scripts kuongelea Serikali na dhambi alizoshiriki naye tutamsamehe na kumuita Mzalendo! aka Kamanda na tutamuweka kwenye NRNE kama mtetezi wa wanyonge.

Tena huyu anayajua mengi kuliko HP, akianza kuyaongea server zote zitajaa, maana kwenye vile vikao yeye ndiye katibu na amekaa Sana jumba jeupe.

safarini Khartoum Sudani.
 
Vijana wa masaki 2015
Ile tallying ya kura ya TACCEO na LHRC pale Kijitonyama ilikuwa moto wakuotea mbali,ilikusanya kura halisi almost vituo vyote Nchi nzima. Magufuli alikuwa kaachwa mbali sana na Lowasa baada ya kuona hivyo JK na Genge lake wakatuma TISS na Polisi kwenda kuwakamata vijana wa Mama Kijogi Simba na Computer zao.
 
Makamba, Nape na Kinana hawa ni wabinafsi. Kwakuwa wamechuma na kujilimbikozia mali hawaoni sababu ya kuwasaidia wenye njaa .
Nape ningemwondoa hata kumfikiria kwa lolote mbali ya ubinafsi. Kinana zipo sababu chungu nzima za kutomhusisha katika maswala ya aina hii; pamoja na kwamba anao uwezo mkubwa wa kimkakati.
 
Polepole vitabu vya maadili ya utumishi wa umma na ukwasi wake vinasoma safi.
Hao wengine wakijaribu tu wataenda kusafisha vyoo vya hospital za umma kama akina Basil Mramba na Daniel Yona. Wazee wa "wananchi watakula nyasi".
 
Hahahahaha Kwa hiyo JM akianza naye kutuma scripts kuongelea Serikali na dhambi alizoshiriki naye tutamsamehe na kumuita Mzalendo! aka Kamanda na tutamuweka kwenye NRNE kama mtetezi wa wanyonge.

Tena huyu anayajua mengi kuliko HP, akianza kuyaongea server zote zitajaa, maana kwenye vile vikao yeye ndiye katibu na amekaa Sana jumba jeupe.

safarini Khartoum Sudani.
"Uzalendo" ni lebo tu inayoweza kutumiwa na mtu yeyote kwa sababu mbalimbali. Ni matendo yanayomhusu mtu ndiyo yanayoweza kumtambulisha kuhusu uzalendo wake kwa wanao yashuhudia matendo hayo.

Sasa sijui kama kuna muda/kipindi maalum ambacho mtu anaweza kuwa kajiondoa kabisa kufanya matendo yanayoweza kuhesabika kuwa ya kizalendo kwa nchi yake. Kuna jambo ammbalo limefanyika linaloweza kumwondolea sifa ya kuonekana kwa waTanzania wezake kwamba anastahili hiyo lebo kwa matendo mazuri baada ya mabaya aliyokwisha onyesha hadi sasa?
 
Unajua huyu jamaa nae ana mabaya yake ambayo wakiamua ku deal nayo hachomoki. Ukwasi alio nao ni questionable so ni heri aendelee kubaki na alicho nacho hata kama sio cha halali kuliko achokoze vilivyolala waamke nae
Hawa waliopo sasa ni kama farasi mfu tayari. Kuzungumzia "kushughulikia" ni kujitia hofu tu.

Huyu Makamba atakuwa anayo madudu mazito kiasi gani ya kumtisha namna hii iwapo kweli hali ya kisiasa iliyopo sasa inamuumiza kama inavyo waumiza waTanzania wengine?

Kueleza ni namna gani walivyoweza kughushi matokeo ya uchaguzi ndiyo iwe sababu ya kuogopa madudu yake yasianikwe?
 
Ile tallying ya kura ya TACCEO na LHRC pale Kijitonyama ilikuwa moto wakuotea mbali,ilikusanya kura halisi almost vituo vyote Nchi nzima. Magufuli alikuwa kaachwa mbali sana na Lowasa baada ya kuona hivyo JK na Genge lake wakatuma TISS na Polisi kwenda kuwakamata vijana wa Mama Kijogi Simba na Computer zao.
Kwa hiyo, Makamba anayaelewa vizuri sana haya maswala yalivyo tokea; na ushuhuda wake huo ndio ungetoa mwanga kamili wa kinachozungumziwa sasa hivi na Polepole.
 
Hawa waliopo sasa ni kama farasi mfu tayari. Kuzungumzia "kushughulikia" ni kujitia hofu tu.

Huyu Makamba atakuwa anayo madudu mazito kiasi gani ya kumtisha namna hii iwapo kweli hali ya kisiasa iliyopo sasa inamuumiza kama inavyo waumiza waTanzania wengine?

Kueleza ni namna gani walivyoweza kughushi matokeo ya uchaguzi ndiyo iwe sababu ya kuogopa madudu yake yasianikwe?
Yesu alipowaambia wafuasi wake kua ambae anajiona hana dhambi ndie awe wa kwanza kumrushia jiwe yule mwanamke mzinzi (John 8.7) hakuna aliejitokeza. Bwana JM ana usafi wa kutosha kuweza kutaja uchafu wa wengine??
 
Hata aongee wasira,kinana,Makamba sr,mahita na yeyote mnae mtaka aongee,.haitakua na maana yeyote kama wananchi hawatachukua hatua..
 
Marope ni sehemu ya wana mtandao na anefaidika kweli kweli.. Hana ubavu wa kusimama na kuongea chochote
Najuwa.
Ndiyo maana nimeanza kwa kumkumbusha juu ya yale aliyowahi kuyaeleza juu ya Tanzania kwenye barua yake aliyoiweka mtandaoni miaka kadhaa iliyopita.

Polepole kang'ang'ania mara kadhaa kuwa yeye ni mwana CCM; na wala hilo hadi sasa hajalikana, pamoja na ubovu woote uliomo ndani ya chama hicho.

Huo "mtandao" utakuwa umemshikilia kiasi gani Makamba; ari hali ni wazi kwamba ndicho chanzo cha vurugu zote ndani ya CCM na kutafuta kuliangamiza taifa zima?
Mtandao huu utakuwa na uhai gani zaidi baada ya mvuruganyo huu kupita, ambao ni lazima utauangamiza kimoja.
Kikwete na kundi lake hawatavuka baada ya Samia kuondolewa madarakani.
 
Back
Top Bottom