Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,915
- 30,027
Sikia nikuambie,Alaaa!
Hilo ndilo linalo kuchanganya?
Maana yangu ni kuwa hiyo "serikali yenye dola" unayoendelea kuiogopa wewe na kuwatishia wengine, kama aikna Makamba, uhai wake upo ukingoni.
Kama utaendelea kututishia kivuli hicho cha hiyo serikali ili daima watu wanyamaze; basi nchi hii haitakuwa na matumaini yoyote yale milele; kitu ambacho mimi sikiamini.
Kwani Polepole aliyezungumza alisahau uwepo wa hiyo "serikali yenye dola"?
Kwa nini unataka Makamba ashikiliwe na minyororo hiyo maisha yake yote? Mimi namhimiza aondokane na hiyo minyororo, kwa kumkumbushia matamanio aliyowahi kuwa nayo akilini mwake na kuyawasilisha kwa njia ya barua watu wamsome.
Tutaogopa hii "serikali ya dola" hadi lini mkuu 'shark'!
Hata mimi ninatamani sana uhai wa serikali hii uwe ukingoni, ila nachokuambia huo ukingo hauko mwaka huu wala muongo huu. Madudu waliyoyafanya wanajua fika kua wakitoka tu madarakani hawatobaki salama. Pia kingine hii nchi ina rasilimali nyingi tu ambazo serikali hii inataka iendelee kuzifaidi milele na milele. Ndio maana kwa gharama na mbinu zozote zile wanahakikisha wanaendelea kubaki madarakani.
Sioni mikakati yoyote ya kuitoa hii serikali ikifanikiwa kwa sasa au hivi karibuni. Serikali hii inafanya chochote kile inachoweza kuhakikisha inabaki madarakani. Polepole anachoongea sio kitu kipya. Humu JF tuna misemo kama Policcm tukimaanisha CCM na Police lao ni moja. Kwamba NEC inaibeba CCM pia sio kitu kipya, tumeanza kuongea miaka na miaka, kuna lililobadilika??
Kwamba kuna waliokua wakijumlisha matokeo pale KIitonyama wakakamatwa na Computer zao kuchukuliwa sio kitu kipya, tumeongea na kuongea, tukaandika na kuandika, wale walionekana watatoa matokeo sahihi yanayokinzana na tume wakawekwa ndani kwanza uchaguzi upite.
Uchaguzi utafika, wataingia tena chama kile kile, miaka na miaka. Yaani tunapita, wanakuja wengine styles ni zile zile, hakutakua na matokeo mapya. Albert Einstein bado anasifika kwa kutukumbusha kua huwezi kurudia kuweka "inputs" zile zile ukategemea kupata "Outputs" tofauti.