Polepole alikataa kuwa DC sasa auvalia suti

Polepole alikataa kuwa DC sasa auvalia suti

Utawezas kumpinga Mbowe wewe? Lowassa alijiunga CHADEMA asubuhi mchana akatangazwa mgombea bila kupingwa ingawa wapinzani walikuwapo tayari, jioni katangazwa mjumbe halimashauri kuu. Mashinji ilikuwaje? Jaribu kumpinga Mbowe uone, asiyejua kufa achungulie kaburi. Wewe kaburi lako ni kina wangwe, zitto, slaa n.k.
Naulizia fomu za kugombea uenyekiti wa ccm taifa
 
sukari ndo unayoona issue sana! kudai demokrasia wakati ulipo hamna demokrasia nikuwatukana wananchi! leo fisadi kesho msafi kiaa kaungana na wewe poor party
Sawa naomba unijuze bei ya sukari kilo moja ni sh ngapi tafadhali!kuwa muungwana
 
Wana jamvi,

Tutakumbuka ni jinsi gani Polepole alivyokuwa anapinga nafasi za Wakuu wa Wilaya kwa kuisimamia rasimu ya katiba ya Jaji Warioba, alienda mbali zaidi kwa kusema kuwa vyeo hivyo ni vya kupoteza fedha!

Sasa nashangaa kuvalia suti kuingia ofisi hiyo hiyo baada ya kupewa nafasi hiyo na mh. rais Magufuli, je tuendelee kumwamini Polepole?

Ni vigumu sana ukiwa hai na kuyaishi unayojiapiza
 
Sijui mzee jaji warioba atakuwa anajisikiaje kwa kumuona kijana wake anamgeuka ktk walio kuwa wana hubiri
Jitahidi kuwa na kumbukumbu huyo Warioba na yeye mbona aliishageuka kitambo? ulishuhudia alichokuwa akikiongea wakati wa kampeni na je umeishawahi kumsikia akiongea lolote juu ya umuhimu wa maoni ya katiba waliyokuwa wameiandaa?
 
Kumbuka Lowasa alisema ahami CCM lakini akahama, na CHADEMA akisema aichukui makapi kutoka CCM lakini sasa ni wajumbe wa kamati kuu CHADEMA, na wengine wanagombea uenyekiti, na wengine walipewa nafasi nyeti.
 
Mwanadamu sio ukuta huwa wakati mwingine anaamini hiki na wakati mwingine huamini kile hii ni kawaida sana kwa mwadamu na hii wala isifasiliwe kama ni njaa
 
Na ikumbukwe kwamba muheshimiwa Lowassa aliwahi kutamka kwa hatotoka Ccm na hana mpango B lakini baadae wote tulishuhudia akisema kuwa ccm sio baba wala sio mama na tukashuhudia mpango b ukiendewa bila ya mafanikio
 
Njaaa mbaya jamani muacheni mwenzeni anyonye.Polepole oyeee katiba ya wananchi mbele ya njaaa kitu gani bwana mdogo polepole
 
Sijui mzee jaji warioba atakuwa anajisikiaje kwa kumuona kijana wake anamgeuka ktk walio kuwa wana hubiri

Mzee Warioba hana neno, alisimama jukwaani kuinadi CCM katika uchaguzi mkuu uliopita. Katika mazingira ya kawaida Mheshimiwa Polepole angefanyaje?. Lawama nyingine hazina msingi kwa maana akikataa yeye unadhani nafasi hiyo haitajazwa?

Hata hivyo Mheshimiwa Polepole kwa umri wake bado anayo nafasi ya kutetea kile anachokiamini na wakati huo huo anapata uzoefu wa kuutumikia umma na anaweza kutatua baadhi ya matatizo aliyonayo ya kiuchumi kama binadamu na matatizo ya kijamii kama mkuu wa wilaya. Ninachojua na tunachotakiwa kukiamini ni kwamba mheshimiwa huyu ni mchambuzi mzuri na anao uwezo wa kujenga hoja kuliko wasomi wengi na watu wengi wa umri wake. Kaza buti Mheshimiwa.
 
Siasa hazina maana, Yericko, Mnyika na Lema jinsi walivyomtukana Lowassa usingeamini kuwa leo wapo pamoja.

Fidel Castro aliwahi kusema " sitakumbatia upumbavu niliousema jana eti kwa sababu yakujionyesha nina msimamo"
Ninaongelea dhana nzima ya kubadilisha msimamo na sio kwamba Lowasa alibadilika alipohamia CHADEMA.
 
Mna wivu kweli? Nasubiri unipe taarifa kama mbaazi zimeanza kukauka. Mwaka huu nataka kuexport za kutosha
lizaboni mbona umesahaulika kwenye teuzi za mkulu au elimu haitoshii maana nasikia mkulu anateua wasomi tu.
 
Back
Top Bottom