Poleni wazazi ambao watoto wenu wamekosa vyuo

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,875
Hadi muda huu ninaongea,
kuna wanafunzi wengi sana wenye vigezo hawajapata vyuo.Wana one ,two na three. Mwezi Juni 2017 ,pale UDSM Mh.Rais aliagiza wanafunzi waombe vyuo kupitia chuo chenyewe na sio TCU (Central Admission System).

Alitoa sababu kadhaa kuwa vyuo baadhi vina honga staffs kadhaa wa TCU ili wapate wanafunzi.

Kipindi hicho nilikuwa Naibu waziri wa mikopo DARUSO,hata nilipokuja kuwa Mwenyekiti-TSNP nimekuwa na msimamo wangu hadi sasa kuwa mfumo wa CAS-TCU ulikuwa imara.

Ni wazi kabisa,sababu za Mh.Rais zilikuwa za msingi sana ,watendaji wake wangemshauri kuzifanyia kazi changamoto alizozitaja kuliko kubadilisha mfumo wote.Na mimi simlaumu sababu yeye alikuwa na lengo la utatuzi wa tatizo.

Nchi yetu ina vyuo vingi sana ,vyenye majina,visivyo na majina ila pia wanafunzi au waombaji wameongezeka sana.Kinachopelekea wanafunzi kukosa vyuo ni kwamba wengi wamejikita kuomba vyuo pendwa,vikubwa na vyenye majina na kwasababu hawapo centralized katika mfumo mmoja ina kuwa ningumu sana kwao,sio rahisi wote kuchaguliwa katika vyuo hivyo hata awamu zote huku vyuo vingine visivyo na majina vikikosa wanafunzi.Kulipaswa kuwe na utoaji wa elimu na ufahamu wa kutosha kwa wanafunzi, ukizingatia mfumo wa kuomba kupitia chuo upo tofauti na ule wa CAS-TCU.

CAS (Central Admission system) ya TCU ilikuwa na uwezo kupeleka wanafunzi katika vyuo walivyoomba na kama hawana vigezo au Admission capacity ipo limited vyuo alivyoomba walikuwa wanasaidia kumpeleka mwanafunzi chuo kingine ,hata kama hajakiomba kuliko kukosa chuo.

Shida ilianzia hapo kuwa wanafunzi wanapelekwa vyuo ambavyo hawakuomba ,ni kwasababu sio wote walioomba UDSM wataenda UDSM ,au Mzumbe,au UDOM nafasi zipo limited na wanafunzi wengine huomba bila ufahamu wa vigezo (Cut point ya faculty huzika/Admission capacity ya faculty).

Hivyo CAS-TCU ikawa inawapeleka katika vyuo ambavyo ,vina nafasi ya udahili ila ambavyo wanafunzi hawakuviomba.

Sasa hivi wanafunzi wanaomba chuo moja kwa moja,wanaomba UDSM ,MZUMBE,UDOM,ARDH na NIT unakuta vyuo hivi vimeombwa na wengi ,hivyo havichukui wote hata kama wanavigezo au hawana ,wanatemwa na awamu ya pili wanaomba programs zingine katika aina ya vyuo hivi wanatemwa .Hatimaye anakosa chuo.CAS-TCU ilikuwa inaweza kumpatia chuo mwanafunzi hata kama hakukiomba kuliko kukosa kama wanavyokosa sasa.

Pia wanafunzi wengi wa Diploma waliokosa AVN hawajaomba chuo hadi sasa ,suala la AVN ni pana mno ,ni shida kubwa .NACTE inapaswa iwajibike kabisa kabisa imeshindwa kusimamia vyuo hivi vinavyotoa diploma , kupeleka matokeo kwa wakati.

Ombi langu kwa TCU,Mimi najua kuna vyuo bado vina nafasi ya udahili ,naomba dirisha lingine lifunguliwe kwa hawa wanafunzi waliokosa vyuo.Vyuo hivyo viruhusiwe kufungua dirisha .

Vijana wana shida mno ,kubwa mno kuanzia katika mfumo wa udahili upo hovyo,mfumo wa kupata AVN upo hovyo, penalty ya 10% bodi ya mikopo baada ya miaka tangu kuhitimu chuo ina umiza watu ,mfumo wa ajira upo hovyo.

Mambo yote kwa vijana yapo hovyo ,mabaraza ya vijana ya vyama (Youth wings) wapo kimya ,kila mtu yupo kimya.

Mungu azidi kutubariki .



Abdul Nondo.

abdulnondo10@gmail.com
Screenshot_20190919-105507~2.jpeg
 
Tatizo lenu nyie watoto huwa mnawaza chuo ni udsm na Udom tu nchi hii ina vyuo kalibu hamsini kwanini wote mkajazane udsm alafu udsm wana sitting capacity let say kozi moja inataka wanafunzi 40 tu nyie mmeomba mia 200 hamuwezi kuchukuliwa wote mtakaa wapi au mnataka msomee madirishani. Chagueni vyuo vya mikoani huko kwasababu vyuo vyote vina hadhi sawa acheni kukalili
 
UDSM competition ni kubwa sana mi nakumbuka miaka yetu nilikua nina one kali na nilikosa nafasi hapo udsm na nilikua na connection ya ndugu kabisa na wakanitema. Roho iliuma but nilikoenda kumbe ndio kulikua the best full watoto wakali maisha yakawa matamu balaa
 
Hadi muda huu ninaongea,
kuna wanafunzi wengi sana wenye vigezo hawajapata vyuo.Wana one ,two na three. Mwezi Juni 2017 ,pale UDSM Mh.Rais aliagiza wanafunzi waombe vyuo kupitia chuo chenyewe na sio TCU (Central Admission System).

Alitoa sababu kadhaa kuwa vyuo baadhi vina honga staffs kadhaa wa TCU ili wapate wanafunzi.

Kipindi hicho nilikuwa Naibu waziri wa mikopo DARUSO,hata nilipokuja kuwa Mwenyekiti-TSNP nimekuwa na msimamo wangu hadi sasa kuwa mfumo wa CAS-TCU ulikuwa imara.

Ni wazi kabisa,sababu za Mh.Rais zilikuwa za msingi sana ,watendaji wake wangemshauri kuzifanyia kazi changamoto alizozitaja kuliko kubadilisha mfumo wote.Na mimi simlaumu sababu yeye alikuwa na lengo la utatuzi wa tatizo.

Nchi yetu ina vyuo vingi sana ,vyenye majina,visivyo na majina ila pia wanafunzi au waombaji wameongezeka sana.Kinachopelekea wanafunzi kukosa vyuo ni kwamba wengi wamejikita kuomba vyuo pendwa,vikubwa na vyenye majina na kwasababu hawapo centralized katika mfumo mmoja ina kuwa ningumu sana kwao,sio rahisi wote kuchaguliwa katika vyuo hivyo hata awamu zote huku vyuo vingine visivyo na majina vikikosa wanafunzi.Kulipaswa kuwe na utoaji wa elimu na ufahamu wa kutosha kwa wanafunzi, ukizingatia mfumo wa kuomba kupitia chuo upo tofauti na ule wa CAS-TCU.

CAS (Central Admission system) ya TCU ilikuwa na uwezo kupeleka wanafunzi katika vyuo walivyoomba na kama hawana vigezo au Admission capacity ipo limited vyuo alivyoomba walikuwa wanasaidia kumpeleka mwanafunzi chuo kingine ,hata kama hajakiomba kuliko kukosa chuo.

Shida ilianzia hapo kuwa wanafunzi wanapelekwa vyuo ambavyo hawakuomba ,ni kwasababu sio wote walioomba UDSM wataenda UDSM ,au Mzumbe,au UDOM nafasi zipo limited na wanafunzi wengine huomba bila ufahamu wa vigezo (Cut point ya faculty huzika/Admission capacity ya faculty).

Hivyo CAS-TCU ikawa inawapeleka katika vyuo ambavyo ,vina nafasi ya udahili ila ambavyo wanafunzi hawakuviomba.

Sasa hivi wanafunzi wanaomba chuo moja kwa moja,wanaomba UDSM ,MZUMBE,UDOM,ARDH na NIT unakuta vyuo hivi vimeombwa na wengi ,hivyo havichukui wote hata kama wanavigezo au hawana ,wanatemwa na awamu ya pili wanaomba programs zingine katika aina ya vyuo hivi wanatemwa .Hatimaye anakosa chuo.CAS-TCU ilikuwa inaweza kumpatia chuo mwanafunzi hata kama hakukiomba kuliko kukosa kama wanavyokosa sasa.

Pia wanafunzi wengi wa Diploma waliokosa AVN hawajaomba chuo hadi sasa ,suala la AVN ni pana mno ,ni shida kubwa .NACTE inapaswa iwajibike kabisa kabisa imeshindwa kusimamia vyuo hivi vinavyotoa diploma , kupeleka matokeo kwa wakati.

Ombi langu kwa TCU,Mimi najua kuna vyuo bado vina nafasi ya udahili ,naomba dirisha lingine lifunguliwe kwa hawa wanafunzi waliokosa vyuo.Vyuo hivyo viruhusiwe kufungua dirisha .

Vijana wana shida mno ,kubwa mno kuanzia katika mfumo wa udahili upo hovyo,mfumo wa kupata AVN upo hovyo, penalty ya 10% bodi ya mikopo baada ya miaka tangu kuhitimu chuo ina umiza watu ,mfumo wa ajira upo hovyo.

Mambo yote kwa vijana yapo hovyo ,mabaraza ya vijana ya vyama (Youth wings) wapo kimya ,kila mtu yupo kimya.

Mungu azidi kutubariki .



Abdul Nondo.

abdulnondo10@gmail.comView attachment 1211250
ongezea na hili...
unakuta mtu alipata alama ambayo haikumuwezesha kwenda kidato cha tano, lakini hizo alama alizopata zilimuwezesha kupata elimu ya astashada kisha stashahada.. na kwa bahati nzuri kwa level ya stashahada akapata alama nzuri za kumuwezesha kudahiliwa kwa muendelezo wa ngazi ya shahada..
sasa tatizo lipo hapa... mtu mwenye ufaulu mzuri ngazi ya stashahada anafanya maombi lakini moja ya kigezo ni kuwa na (credit) ufaulu wa masomo matatu kidato cha nne, sasa huyu mtu stashahada yake ina maana si lolote..??
mwengine unakuta kati ya haya masomo ya physics na chemistry mojawapo hajalifanyia mtihani kidato cha nne, na alipata ufaulu ambao ulimuwezesha kudahiliwa chuo cha kilimo ngazi ya astashahada, huyu mtu anasoma hadi ngazi ya stashahada na kufaulu vizuri kwa alama ambazo zinamuwezesha kusoma ngazi ya shahada ya kwanza katila kozi zenye kuhusiana na kilimo,
lakini cha ajabu kwenye udahili anakwama kutokana na cheti cha kidato cha nne kwamba hana ufaulu wa masomo manne ya sayansi...
 
Bongo ni shida sana. Changamoto zipo kwa wanafunzi, bodi ya mikopo na tcu kote.
 
Kuna issue moja kubwa sana umeioverlook. APPLICATION FEE.

Mimi kuna dogo nimemfanyia application MD. Alikuwa ana II:10 ya PCB. Lengo lake lilikuwa asome MD.

Lkn kwa huo ufaulu nilijua kupata MD ni kwa majaaliwa. Sikutaka kumvunja moyo, ila nikamshauri aapply vyuo vyooote vinavyotoa MD.

Kwa hiyo aliapply MUHAS, UDOM, UDSM, CUHAS, KCMUCo, HERBET KAIRUKI, ST JOSEPH. Jumla vyuo 7.

Gharama za kila chuo ni kama ifuatavyo:
MUHAS----------10,000/=
UDOM----------10,000/=
UDSM----------10,000/=
CUHAS----------30,000/=
KCMUCo----------50,000/=
KAIRUKI----------50,000/=
ST JOSEPH----------0/=​


Sasa ukipiga jumla kuu hapo ni shilingi laki moja na sitini elfu (160,000/=).

Kwa maisha ya kitanzania hiyo gharama ni mzigo mzito sana.

CAS-TCU wanafunzi walikuwa wanaapply kwa shilingi elfu thelathini (30,000/=) tuu.

Unaposema kwamba tatizo ni wanafunzi kuapply vyuo vyenye competion kubwa sio sahihi, sababu kuna factors nyingi wanazoangalia ikiwemo kupata mkopo.

Pia unaposema hawajui vyuo vingine si kweli kwa sababu kwenye TCU GUIDELINE kuna orodha ya vyuo vyooote.


Unforgetable
 
CAS (Central Admission system) ya TCU ilikuwa na uwezo kupeleka wanafunzi katika vyuo walivyoomba na kama hawana vigezo au Admission capacity ipo limited vyuo alivyoomba walikuwa wanasaidia kumpeleka mwanafunzi chuo kingine ,hata kama hajakiomba kuliko kukosa chuo.
Naona ingawa hili jambo limeongelewa hapa JF kwa muda sasa toka walipo ua CAS hakuna mwenye nia ya kumuambia mhusika kuwa tumefumua matatizo mengi kuliko yale tuliyo fikiria tuna yatibu. Multiple selection ni shida kubwa na TCU sasa naona hawataki kutoa "msaada" waliokuwa wanatoa huko mwanzo. Halafu vijana wanachagua vyuo na program wakichaguliwa wanakana kuwa hawakuchagua. Ndio tumefika hapa. Itabidi waziri Ndalichako alisimamie hili awe na werevu wa kufanya tathmini kuhusu ufanisi wa hii system ya maombi ya mja kw moja. Nilisoma mahali hata huko UK wakikaribia tamati CAS yao huwatafutia nafasi wale waliokosa.
Kitu kingine hatuna uwazi wa kutosha zamani UDSM walikua wanatoa points za waliochaguliwa na wale walioachwa hutoa sababu. Hivyo ukiachwa unaweza kujiridhisha kama haki imetendeka. Na CAS ilikuwa inaweka data nafasi ziko wapi wakifungua round ya pili, kwa sasa haiwezekani kwa sababu ya multiple selections, hivyo waombaji wanaomba wakiwa gizani. LABDA TUNAHITAJI HAKI ELIMU YA VYUO HIVI. Watawala mpaka sasa hawatuelewi.


Pia wanafunzi wengi wa Diploma waliokosa AVN hawajaomba chuo hadi sasa ,suala la AVN ni pana mno ,ni shida kubwa .NACTE inapaswa iwajibike kabisa kabisa imeshindwa kusimamia vyuo hivi vinavyotoa diploma , kupeleka matokeo kwa wakati.
Kwa hili pia tumelisema sana-ukweli NACTE hapa naona wamefika mwisho na vyuo pia vinashindwa kuoanisha cycles za udahili na almanc zao. Juzi nimekutana na kijana ndio yuko field mwaka wa mwisho hivyo hawezi kupata matokeo kwa muda muafaka inabidi asubiri mwakani. Hivi hakuna njia ya kusimamia vyuo ili kitu kama AVN kipatikane mwanafunzi afanyapo mitihani na matokeo yake yakihakikiwa NACTE basi shughuli iwe imekwisha. Nina hakika technologia ipo ya kuwezesha haya mambo. HUENDA MUDA UMEFIKA WA KUJA NA TAASISI MOJA TU YA KUSIMAMIA VYUO VYA KATI NA VYUO VIKUU.
 
Kuna issue moja kubwa sana umeioverlook. APPLICATION FEE.

Mimi kuna dogo nimemfanyia application MD. Alikuwa ana II:10 ya PCB. Lengo lake lilikuwa asome MD.

Lkn kwa huo ufaulu nilijua kupata MD ni kwa majaaliwa. Sikutaka kumvunja moyo, ila nikamshauri aapply vyuo vyooote vinavyotoa MD.

Kwa hiyo aliapply MUHAS, UDOM, UDSM, CUHAS, KCMUCo, HERBET KAIRUKI, ST JOSEPH. Jumla vyuo 7.

Gharama za kila chuo ni kama ifuatavyo:
MUHAS----------10,000/=
UDOM----------10,000/=
UDSM----------10,000/=
CUHAS----------30,000/=
KCMUCo----------50,000/=
KAIRUKI----------50,000/=
ST JOSEPH----------0/=​


Sasa ukipiga jumla kuu hapo ni shilingi laki moja na sitini elfu (160,000/=).

Kwa maisha ya kitanzania hiyo gharama ni mzigo mzito sana.

CAS-TCU wanafunzi walikuwa wanaapply kwa shilingi elfu thelathini (30,000/=) tuu.

Unaposema kwamba tatizo ni wanafunzi kuapply vyuo vyenye competion kubwa sio sahihi, sababu kuna factors nyingi wanazoangalia ikiwemo kupata mkopo.

Pia unaposema hawajui vyuo vingine si kweli kwa sababu kwenye TCU GUIDELINE kuna orodha ya vyuo vyooote.


Unforgetable
Vp amebahatika kuchaguliwa chuo gani??
 
UDSM competition ni kubwa sana mi nakumbuka miaka yetu nilikua nina one kali na nilikosa nafasi hapo udsm na nilikua na connection ya ndugu kabisa na wakanitema. Roho iliuma but nilikoenda kumbe ndio kulikua the best full watoto wakali maisha yakawa matamu balaa
dah kwa kauli yako hii ndo nmegundua kama ww dume kweli id fake hizi ni mtihan
 
Ni wazi kabisa,sababu za Mh.Rais zilikuwa za msingi sana ,watendaji wake wangemshauri kuzifanyia kazi changamoto alizozitaja kuliko kubadilisha mfumo wote.Na mimi simlaumu sababu yeye alikuwa na lengo la utatuzi wa tatizo.
Mkuu hapa tunapishana, yeye ni wa kulaumiwa kwenye hili kwani naamini anajua kwa jinsi serikali yetu ilivyo akitoa neno walio chini yake wanasema katoa maagizo na kawaida wengi "hawatafakari" zaidi. Je aliomba ushauri kwenye hili au aliamini kuwa agizo lake liko sawa? Alijua CAS inafanyaje kazi na kile alichotaka kitaleta matatizo gani?. Sidhani kama alifanya due diligence kwenye hili.

By the way leo 20/09/2019 selections za ROUND THREE ambayo ni ya mwisho kwenye calender yetu ya udahili zitatoka. Sijui kama kutakuwa na TAMKO lolote. Huko nyuma kote (kuanzia 2017) imebidi waongeze madirisha ya udahili kwani mfumo unashindwa kuwapatia wenye ufaulu nafasi kwa muda muafaka. TUFATILIE na KUPAZA SAUTI.TUNAHITAJI TATHMINI YA MATOKEO YA HILI AGIZO la RAISI.
 
Kuna mdau alisema i round ya tatu ni kama kiini macho tu....walio kosa round ii ni wengi sana
 
Kuna issue moja kubwa sana umeioverlook. APPLICATION FEE.

Mimi kuna dogo nimemfanyia application MD. Alikuwa ana II:10 ya PCB. Lengo lake lilikuwa asome MD.

Lkn kwa huo ufaulu nilijua kupata MD ni kwa majaaliwa. Sikutaka kumvunja moyo, ila nikamshauri aapply vyuo vyooote vinavyotoa MD.

Kwa hiyo aliapply MUHAS, UDOM, UDSM, CUHAS, KCMUCo, HERBET KAIRUKI, ST JOSEPH. Jumla vyuo 7.

Gharama za kila chuo ni kama ifuatavyo:

MUHAS----------10,000/=

UDOM----------10,000/=

UDSM----------10,000/=

CUHAS----------30,000/=

KCMUCo----------50,000/=

KAIRUKI----------50,000/=

ST JOSEPH----------0/=




Sasa ukipiga jumla kuu hapo ni shilingi laki moja na sitini elfu (160,000/=).

Kwa maisha ya kitanzania hiyo gharama ni mzigo mzito sana.

CAS-TCU wanafunzi walikuwa wanaapply kwa shilingi elfu thelathini (30,000/=) tuu.

Unaposema kwamba tatizo ni wanafunzi kuapply vyuo vyenye competion kubwa sio sahihi, sababu kuna factors nyingi wanazoangalia ikiwemo kupata mkopo.

Pia unaposema hawajui vyuo vingine si kweli kwa sababu kwenye TCU GUIDELINE kuna orodha ya vyuo vyooote.


Unforgetable
Uwe unasoma guidebook,mtakuwa mnalaumu tu,two ya 10 hawezi kwenda MD labda akasome vyuo private
 
Back
Top Bottom