Ze burner
JF-Expert Member
- Jan 5, 2011
- 514
- 83
habari wana jf.
nikiwa home nimeketi kwa umakini mkubwa nikisikiliza taarifa ya habari kutoka tbc1 nikasikia habari ya chanjo mpya ya maleria ambayo kwa maelezo ya watafiti wanasema inaweza kuzuia mtu aliyechanjwa kutopata malaria kwa muda wa miaka miwili. uhakika wa chanjo hiyo ni wa asilimia hamsini. watafiti bado wanaendelea kusema kuwa licha ya chanjo hiyo kuonekana inafaa bado inabidi itumike katika hali ya majaribio kwa kwa miaka miwili zaidi kabla ya kutumika rasmi.
Kilichonishtua zaidi ni kwamba majaribio ya chanjo hiyo yamefanyika katika nchi saba tu zote za afrika ikiwemo nchi yetu ya Tanzania. mikoa iliyotumika kwa majaribio ya chanjo iyo ni mkoa wa tanga (wilaya ya korogwe) na mkoa wa pwani ( wilaya ya bagamoyo).
hivi wana jf kweli serikali yetu inatutakia mema kwa kutufanya sisi ndo chambo kwa chanjo hiyo, hivi serikali haikujiuliza ni kwanini chanjo hiyo haifanyiwa majaribio pia katika nchi za wanaojiita watu weupe? ninachokiona mimi ni kwamba serikali kwa kweli imetuchoka raia wake kwa kiasi kikubwa. mimi sifahamu zaidi ila kwa suala la kujaribiwa sumu hii imeniuma sana maana ki kawaida wanyama wenye mifumo sawa na wanadamu ndio hujaribiwa kwa dawa fulani na siyo mwanadamu.
Poleni sana ndugu zetu wa maeneo mliolishwa sumu hiyo. ni Mungu tu awanusuru waja wake ila serikali yenu kamwe haijawatendea haki.
Ndugu wana Jf wenzangu. dua zetu ni muhimu sana ili kunusuru janga lolote kwa majaribu hayo. tena siju kama hao wanaojaribiwa wanafahamu kuwa wanajaribiwa... na hii ndiyo sirikali yetu.
wenye uelewa zaidi watutoe hofu. karibuni sana
nikiwa home nimeketi kwa umakini mkubwa nikisikiliza taarifa ya habari kutoka tbc1 nikasikia habari ya chanjo mpya ya maleria ambayo kwa maelezo ya watafiti wanasema inaweza kuzuia mtu aliyechanjwa kutopata malaria kwa muda wa miaka miwili. uhakika wa chanjo hiyo ni wa asilimia hamsini. watafiti bado wanaendelea kusema kuwa licha ya chanjo hiyo kuonekana inafaa bado inabidi itumike katika hali ya majaribio kwa kwa miaka miwili zaidi kabla ya kutumika rasmi.
Kilichonishtua zaidi ni kwamba majaribio ya chanjo hiyo yamefanyika katika nchi saba tu zote za afrika ikiwemo nchi yetu ya Tanzania. mikoa iliyotumika kwa majaribio ya chanjo iyo ni mkoa wa tanga (wilaya ya korogwe) na mkoa wa pwani ( wilaya ya bagamoyo).
hivi wana jf kweli serikali yetu inatutakia mema kwa kutufanya sisi ndo chambo kwa chanjo hiyo, hivi serikali haikujiuliza ni kwanini chanjo hiyo haifanyiwa majaribio pia katika nchi za wanaojiita watu weupe? ninachokiona mimi ni kwamba serikali kwa kweli imetuchoka raia wake kwa kiasi kikubwa. mimi sifahamu zaidi ila kwa suala la kujaribiwa sumu hii imeniuma sana maana ki kawaida wanyama wenye mifumo sawa na wanadamu ndio hujaribiwa kwa dawa fulani na siyo mwanadamu.
Poleni sana ndugu zetu wa maeneo mliolishwa sumu hiyo. ni Mungu tu awanusuru waja wake ila serikali yenu kamwe haijawatendea haki.
Ndugu wana Jf wenzangu. dua zetu ni muhimu sana ili kunusuru janga lolote kwa majaribu hayo. tena siju kama hao wanaojaribiwa wanafahamu kuwa wanajaribiwa... na hii ndiyo sirikali yetu.
wenye uelewa zaidi watutoe hofu. karibuni sana