Pole sana rafiki yangu. Ndoa hizi!

Pole sana rafiki yangu. Ndoa hizi!

Nikajua ni kitu cha maaana kumbe ushuzi. Nilidhani jamaa amekatwa kichwa kumbe analia tu. Mke wa mtu sumu.
Punguza roho mbaya mkuu,akikatwa kichwa then mkataji na wewe mnanufaikaje?
 
Maskini ana tatizo gani??? Wewe ndo huna akili kabisaaaaaaa.... Unaacha kuwashauri waoe watu wenye hofu ya mungu unawashauri wasioe maskini..... Haya maskini na kutoka nje ya ndoa vina uhusiano gani


Ni ushauri tuu. Utakaye mfaa atauchukua usiye mfaa atauacha.

Binafsi kama wewe ni masikini huwezi kunivutia hata ungekaa uchi hapo.
 
Maskini ana tatizo gani??? Wewe ndo huna akili kabisaaaaaaa.... Unaacha kuwashauri waoe watu wenye hofu ya mungu unawashauri wasioe maskini..... Haya maskini na kutoka nje ya ndoa vina uhusiano gani

Uliona wapi mtu asiye na bikra akawa na hofu ya Mungu.

Uliona wapi Masikini akawa na hofu ya Mungu.

Hivi unawajua masikini Mkuu?
 
Wanaume wanachepuka sana kama jadi yao na inaonekana kawaida sababu ya matamanio ya muda, lakini mpaka mwanamke atoke nje ujue hapo kuna tatizo .... Ila mamiloo kachemsha
 
Wakuu mimi ni mtata sana ila amini siwezi kumpiga mwanamke nikifumania akiliwa na mwanaume mwingine..

Ningekuwa mimi hapo, kiroho safi kama nimethibitisha kwamba amechepuka
namruhusu tangu siku hiyo akaishi na huyo bwana mimi narudi kufanya mambo yangu.

Yawezekana dudu langu halimkidhi so alikuwa kwangu tu kwa sababu ya ndoa, hivyo nampa uhuru aende kwa huyo anaekimdhi na mimi kiroho naenda kutafuta mwingine wa kuendeleza gurudumu.
Yaani hata mm katika kitu siwezi ni kuthibitisha mke au demu wangu kulala au kuwa na mahusiano na mwingine huwa niko radhi kuachana kuliko kuishi na mtu wa hivyo,,mtu achepuke nisipojua sina tatizo nikijua sijui kusamehe japo na mimi nachepuka
 
Bila kupoteza muda, naomba kushea nanyi mkasa mzito ulomfika rafiki yangu.

Jamaa yangu anayeishi mkoani alifunga ndoa miaka kadhaa iliyopita, (jamaa alimuoa bibie akiwa na mahaba mazito sana na jamaa mmoja ambaye walisoma pamoja).

Baada ya miaka kadhaa kwenye ndoa na kubarikiwa watoto wawili, mke akakumbuka penzi la mpenzi wake wa zamani, akaanza kumbembeleza sana mpenzi wake wa kale waendelee na mahusiano huku akieleza magumu anayokutana nayo kwenye ndoa yake, jamaa alikataa. (Mke wa mtu hakukata tamaa, akaendelea kumuomba sana jamaa waendelee na mahusiano yao).

Baada ya mvutano wa muda mrefu, mke wa jamaa akaomba ruhusa kwa mumewe kwenda jijini Dar kusabahi ndugu zake. Jamaa akamruhusu, lakini kwa kuwa alikuwa na mashaka na mwenendo wa mkewe, alipanda ndege kwenda Dar wakati mke alipanda bus (mume akawahi kufika kabla ya mke,bna hivyo kusubiri uelekeo wa mke).

Mke amefika Dar, akapokelewa na mpenzi wake wa kale. Wakaenda hotel fulani karibu Ubungo, wakavunja amri ya sita mpaka asubuhi, wakati wote huo mume anamuuliza mkewe amefikia kwa ndugu yupi mke anamdanganya mumewe pasipo kujua jamaa yupo jijini tayari.

Asubuhi ya jana tarehe 20/10/2019 wameachana (wapenzi wa zamani) na kuahidiana kukutana siku itakayofuata kuendeleza usaliti wao. Mke anakwenda mchana kwa nduguye, akamkuta mumewe!

Mume kwa hasira kaanza kumpiga mkewe. Kampiga sana na kuondoka naye kurejea mkoani, (usiku wa kuamkia leo). Jamaa (mpenzi wa chuo) nipo naye hapa anajutia sana kukubali kulala na mke wa mtu, analia wakati wote tangu asubuhi, sasa sijui analia mpenzi wake kupigwa au analia kujutia kumkosea Mungu wake.

Wakati wengine wanakesha kuomba wapate waume hata waletwao na upepo wa kisulisuli, wengine walio ndoani wanasaliti ndoa zao na kufanya mambo ya kipuuzi kabisa (hapa justifications za kufanya usaliti sijazingatia).

Sijui huko mkoani kama huyu mwanamke yupo salama, mioyo imejaa hofu sana tukifikiria hasira za jamaa!

Wanawake kwa wanaume, mkiamua kuingia kwenye ndoa basi mjitahidi kuheshimu ndoa zenu (na kama mkishindwana basi achaneni kwa amani na maisha yaendelee). Lakini hii habari ya kusalitiana inaleta madhara makubwa sana, na wakati fulani inakatisha maisha ya watu kabisa!

Mungu aturehemu, pole sana dada kwa kipigo lakini pia pole sana brother kwa msukosuko huu mzito, kikubwa usimuue mkeo, unaweza kumuacha kwa kosa la kukusaliti au unaweza kumsamehe maisha yaendelee!

Usiingie Ndoani kama hakuna mapenzi ya dhati au upendo wa Agape. Jamani tusidanganyike, mwanamke kama hajakupenda mwanzoni ni ngumu kukupenda mbeleni. Ndoa si mchezo, linahitajika penzi la dhati na uaminifu wa dhati. Huyo jamaa hata akipiga, kama mwanamke hamtaki ndo imetoka hiyo. Mimi ningemshauri asali sana Mungu aweze change moyo wa uyo dada maana si vita ya kimwili ni ya kiroho. Kama haitowezekani basi waachane kwa amani.
 
Wewe unawasema wanaoenda kanisani au misikitini hovyo, Kuna mawili hapo kuhudhuria nyumba, za ibada na usiwe mchamungu na kinyume chake pia
Wanatimbwa na wakina baba mchungaji sema hujui tu
 
Usimsingizie maskini na kutokuwa na hofu ya mungu hivyo vitu ni Maji na mafuta............
Kama ni hivyo hao wenye pesa mimi najua 75% hawana hofu ya mungu, chunguza
Uliona wapi mtu asiye na bikra akawa na hofu ya Mungu.

Uliona wapi Masikini akawa na hofu ya Mungu.

Hivi unawajua masikini Mkuu?
 
Back
Top Bottom