Pole sana Alphonce modest - TFF mko wapi?

MTAZAMO

JF-Expert Member
Feb 8, 2011
19,643
33,427
Wanabodi,

Nimesoma habari kupitia gazeti la Championi kuhusu hali mbaya ya kiafya ya mchezaji mkongwe aliyewahi kuchezea Simba kwa mafanikio makubwa na pia kucheza Taifa Stars kwa kipindi kirefu sana tena kwa kiwango cha juu Alphonce Modest.

Mchezaji huyu kwa mujibu wa Championi la leo anasumbuliwa na figo amelazwa Bugando Mwanza na hali yake kimaisha ni mbaya kumudu matibabu yake.Alphonce Modest amewataja Juma Kaseja na Mrisho Ngassa kama wachezaji pekee wanaomsaidia.

Namkumbuka mchezaji huyu alivyokuwa na nidhamu kubwa,mpole na mtu wa dini na hasa soka lake akiwa moja ya beki namba tatu bora kuwahi kutokea Tanzania.
Hali ya soka huko nyuma kifedha ilikuwa mbaya zaidi ya sasa na wachezaji wengi wamebaki maskini.

Naomba nitoe wito kwa TFF lifanye juhudi za kumsaidia Alphonce Modest ikibidi uwekwe utaratibu wananchi tumsaidie kuchangia tulicho nacho ili Modest ajue tunathamini mchango wake ktk Taifa hili na iwe motisha kwa vijana tunaowahimiza washiriki michezo.

Pole sana Alphonce Modest,Mungu mwenye huruma akupe nafuu ya haraka ili uendelee kujenga Taifa letu.

Mods habari hii ni zaidi ya sports!
 
Wadau wa Soka la Mwanza,Alphonce Modest ni moja ya matunda ya Pamba Sport Club kabla ya kwenda Simba alikocheza kwa muda mrefu.
 
pole sana Alphonce Modest...moja ya majembe ya ukweli Stars ya kitambo
 
pole sana Alphonce Modest...moja ya majembe ya ukweli Stars ya kitambo

Mtu kama Alphonce Modest kodi yetu ikitumika kumtibu hata abroad naona haki kabisa kwa jinsi alivyotumikia taifa lake tena kipindi hicho Taifa Stars haina wadhamini lakini walipigania kulinda heshima ya nchi pamoja na hali zao.
 
Kama watu walimchangia kwa kasi kubwa yule mwanafilamu mpaka akapelekwa India, naomba tufanye utaratibu achangiwe Alphonce. SIMBA na MTIBWA ongozeni harambee. Mchango wa jamaa ulikuwa mkubwa sana.
 
Pole sana modest wadau watafikishiwa salaam sasa hata wangeweka no simu yake lakini watu wamrushie japo kidogo!alietoa habari ajitahidi kwa hilo
 
Weka namba ya m pesa /tigo pesa etc tuchangamkie michango.
By the way nini maana ya kuwa na SPUTANZA,mwenyekiti ex mbunge wa kilolo na DC wa kigoma kwa sasa ( jina limenitoka) vipi umelala tu au ndo wale wale mkishapigiwa kura mnapotea hadi next uchaguzi?
 
Ndo upumbafu wa wachezaji wa tanzania..sijui wanakuwaga wapi kuandaa future..hivi akina messi watakuja kuwa hivi
 
Wanabodi,

Nimesoma habari kupitia gazeti la Championi kuhusu hali mbaya ya kiafya ya mchezaji mkongwe aliyewahi kuchezea Simba kwa mafanikio makubwa na pia kucheza Taifa Stars kwa kipindi kirefu sana tena kwa kiwango cha juu Alphonce Modest.

Mchezaji huyu kwa mujibu wa Championi la leo anasumbuliwa na figo amelazwa Bugando Mwanza na hali yake kimaisha ni mbaya kumudu matibabu yake.Alphonce Modest amewataja Juma Kaseja na Mrisho Ngassa kama wachezaji pekee wanaomsaidia.

Namkumbuka mchezaji huyu alivyokuwa na nidhamu kubwa,mpole na mtu wa dini na hasa soka lake akiwa moja ya beki namba tatu bora kuwahi kutokea Tanzania.
Hali ya soka huko nyuma kifedha ilikuwa mbaya zaidi ya sasa na wachezaji wengi wamebaki maskini.

Naomba nitoe wito kwa TFF lifanye juhudi za kumsaidia Alphonce Modest ikibidi uwekwe utaratibu wananchi tumsaidie kuchangia tulicho nacho ili Modest ajue tunathamini mchango wake ktk Taifa hili na iwe motisha kwa vijana tunaowahimiza washiriki michezo.

Pole sana Alphonce Modest,Mungu mwenye huruma akupe nafuu ya haraka ili uendelee kujenga Taifa letu.

Mods habari hii ni zaidi ya sports!
Watanzania mnapenda kulalamika sana,hivi nani anapaswa kumhudumia huyo mchezaji?si alikuwa anafanya kazi kipindi hicho?huu utaratibu wa kuwalaumu tff kwa kila mchezaji anaeumwa itaisha lini?na mm ambaye sina kazi nitamlaumu nani nikiumwa?tuache kulalamikakila mtu ana haki ya kumsaidia mwenzake!
 
Mimi naamini kuwa vilabu ndio vina jukumu la msingi kusaidia wachezaji wake pale inapobidi. Hivyo basi mwito huu ungeelekezwa kwa Simba kwanza. Ni mtazamo wangu tu wadau msinimeze.
 
Pole sna alphonce ila hii ni msg tosha kwa ngassa kwamba ukichezea simba ukastaafu hawakuthamini tena, angalia kilichotokea kwa mafisango vyombo kutupwa nje. Simba hawajali wachezaji wao wa zamani.
 
Watanzania mnapenda kulalamika sana,hivi nani anapaswa kumhudumia huyo mchezaji?si alikuwa anafanya kazi kipindi hicho?huu utaratibu wa kuwalaumu tff kwa kila mchezaji anaeumwa itaisha lini?na mm ambaye sina kazi nitamlaumu nani nikiumwa?tuache kulalamikakila mtu ana haki ya kumsaidia mwenzake!

michezo yote tanzania ni ya ridhaa, usikurupuke!!!!!

Alphonce Modest ni wakusaidiwa na watanzania wote, napendekeza apelekwe india haraka sana, wizara ya habari utamaduni na michezo ilipie, AM ni balozi mstaafu wa tanzania kwenye nchi zenye viwanja vya mpira wa miguu.
 
Kama watu walimchangia kwa kasi kubwa yule mwanafilamu mpaka akapelekwa India, naomba tufanye utaratibu achangiwe Alphonce. SIMBA na MTIBWA ongozeni harambee. Mchango wa jamaa ulikuwa mkubwa sana.

gazeti la championi wakishirikiana na Magic Fm kipindi cha michezo limeanzisha kampeni "MSAIDIE MODEST" wasiliana nao kupitia +255 716 260 778.
 
gazeti la championi wakishirikiana na Magic Fm kipindi cha michezo limeanzisha kampeni "MSAIDIE MODEST" wasiliana nao kupitia +255 716 260 778.

Kampuni ya Msama imetoa sh Milioni moja kama mchango kwa ajili ya matibabu ya Modest.
 
Back
Top Bottom