Pituitary grand huwa inakua na shida?

Pituitary grand huwa inakua na shida?

malembeka18

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2018
Posts
3,834
Reaction score
4,561
Habar wakuu hivi pituitary gland huwa nayo inaweza kuwa na shida na itasababisha mtu kupata tatizo gani
 
Habar wakuu hivi pituitary gland huwa nayo inaweza kuwa na shida na itasababisha mtu kupata tatizo gani
Ndiyo hupata shida. Na tatizo hutegemeana na jinsia pamoja na ukubwa wa tatizo lenyewe.

Zaidi, huweza kusababisha kisukari, kushindwa kusimamisha na uzalishaji wa mayai na mbegu, kupunguza uzalishaji wa maziwa (unyonyeshaji), uzito uliopindukia na mambo mengine mengi.

Pituitary gland ndo tezi kuu. Ina kazi kubwa sana mwilini. Athari hutegemeana na aina ya tatizo kwenye tezi husika.

Wahi hospitali kwa uchunguzi zaidi.
 
Ndiyo hupata shida. Na tatizo hutegemeana na jinsia pamoja na ukubwa wa tatizo lenyewe.

Zaidi, huweza kusababisha kisukari, kushindwa kusimamisha na uzalishaji wa mayai na mbegu, kupunguza uzalishaji wa maziwa (unyonyeshaji), uzito uliopindukia na mambo mengine mengi.

Pituitary gland ndo tezi kuu. Ina kazi kubwa sana mwilini. Athari hutegemeana na aina ya tatizo kwenye tezi husika.

Wahi hospitali kwa uchunguzi zaidi.
Dalili zake huwa ni ni
 
Ndiyo hupata shida. Na tatizo hutegemeana na jinsia pamoja na ukubwa wa tatizo lenyewe.

Zaidi, huweza kusababisha kisukari, kushindwa kusimamisha na uzalishaji wa mayai na mbegu, kupunguza uzalishaji wa maziwa (unyonyeshaji), uzito uliopindukia na mambo mengine mengi.

Pituitary gland ndo tezi kuu. Ina kazi kubwa sana mwilini. Athari hutegemeana na aina ya tatizo kwenye tezi husika.

Wahi hospitali kwa uchunguzi zaidi.
Pituitary ikiwa nashida inaweza kusababisha goita
 
Pituitary ikiwa nashida inaweza kusababisha goita
Ndiyo.

Goita ni uvimbe wa tezi ya Thyroid. Hiyo tezi ipo chini kidogo ya koromeo.

Tezi ya thyroid hutengeneza homoni za aina tatu, thyroxine (T4), triiodothyronine (T3) na calcitonin.

Sasa matatizo kwenye tezi ya pituitary husababishaje Goita?
Awali nilishakueleza kuwa Pituitary ndiyo tezi kuu. Yenyewe inapohisi kuna kiwango kidogo cha T3 na T4, tezi ya pituitary huachia kiwango fulani cha homoni zao (pamoja na hypothalamus) ili kuweza kubalance kiwango cha homoni ya thyroid.

Vivyo hivyo, inapohisi kuna kiwango kikubwa cha homoni ya thryroid huminya utengenezaji wa homoni zao ili kuleta uwiano wa homoni hiyo katika damu.

Hivyo, tezi ya pituitary hudhibiti tezi ya thyroid.

Sasa, matatizo kwenye tezi ya pituiitary husabisha tezi husika kushindwa kuhisi kwa usahihi kiwango cha homoni ya Thyroid Stimulating (TSH) kinachopaswa kutolewa ili kuleta uwiano.

Hivyo, inaweza kutoa kwa kiwango kiwango kikubwa (hyperthyroidism) ama kwa kiwango hafifu (hypothyroidism).

Sasa endapo itatoa kwa kiwango kikubwa itasababisha kuvimba kwa tezi husika na ambayo huitwa goita.
 
Nin kinatakiwa kufanyika ili pituitary isiwe nashida
 
Nin kinatakiwa kufanyika ili pituitary isiwe nashida
Kwanza tambua, kisababishi kikuu cha goita ni ukosefu wa madini ya Iodine.

Kama umeambiwa kuwa multinoduler goiter imesababishwa na tatizo kwenye tezi ya pituitary basi unapaswa kuitibu tezi husika. Ama kumeza substitutes za homoni husika. Kama ipo kwa kiwango kikubwa basi unameza dawa za kupunguza. Kama zipo kwa kiwango kidogo basi unameza za kuboost homoni hiyo.
 
Kwanza tambua, kisababishi kikuu cha goita ni ukosefu wa madini ya Iodine.

Kama umeambiwa kuwa multinoduler goiter imesababishwa na tatizo kwenye tezi ya pituitary basi unapaswa kuitibu tezi husika. Ama kumeza substitutes za homoni husika. Kama ipo kwa kiwango kikubwa basi unameza dawa za kupunguza. Kama zipo kwa kiwango kidogo basi unameza za kuboost homoni hiyo.
Mim niliambiwa diffused multnoduler goiter nkapewa lcarbimazole nkatumia ikareturn to hypo
 
Kwanza tambua, kisababishi kikuu cha goita ni ukosefu wa madini ya Iodine.

Kama umeambiwa kuwa multinoduler goiter imesababishwa na tatizo kwenye tezi ya pituitary basi unapaswa kuitibu tezi husika. Ama kumeza substitutes za homoni husika. Kama ipo kwa kiwango kikubwa basi unameza dawa za kupunguza. Kama zipo kwa kiwango kidogo basi unameza za kuboost homoni hiyo.
Sasa mkuu samahani kwa usumbufu hivi grave diseases nikitu Gani,na hashimotos ni kitu gani
 
Mim niliambiwa diffused multnoduler goiter nkapewa lcarbimazole nkatumia ikareturn to hypo
Maana yake wewe Thyroid ilikuwa inazalishwa kwa kiwango kikubwa (hyperthyroidism)..

Carbimazole hupunguza utengenezaji wa hormone ya Thyroid.

Kama imerudi kwenye hypothyroidism basi acha kuitumia. Kwa sababu itazidi kudidimiza kiwango cha thyroid.

Subiri kwa muda kisha kama bado itakuwa kwenye hypo basi kuna dawa iitwayo Levothyroxine.

Ila kwanza iache hiyo. Wasiliana na daktari wako kwa msaada zaidi.
 
Sasa mkuu samahani kwa usumbufu hivi grave diseases nikitu Gani,na hashimotos ni kitu gani
Grave disease na hashimoto ugonjwa mmoja ila reaction zake ndiyo tofauti. Inaposababisha hypothyrodism basi ni Hashimoto. Na ikiwa itasabisha hyperthyrodism basi hiyo ndiyo Grave disease.

Kwa muktadha huo ni kuwa, mwili hutengeneza askari kwa ajili ya kujilinda kutokana na maambukizi. Inapohisi kuna kirusi kimeingia basi askari huwajibika kupambana naye.

Lakini katika hali isiyo ya kawaida, kuna askari wanaanza kuishambulia tezi ya thyroid na kuiongezea kasi katika utengenezaji wa homoni. Huko ndipo hutokea Grave disease.

Endapo askari hao wakaishambulia tezi ya thyroid na kupunguza utengenezaji wa homoni basi hutokea hypothyrodism. Na ndipo huitwa hashimoto.
 
Maana yake wewe Thyroid ilikuwa inazalishwa kwa kiwango kikubwa (hyperthyroidism)..

Icarbimazole hupunguza utengenezaji wa hormone ya Thyroid.

Kama imerudi kwenye hypothyroidism basi acha kuitumia. Kwa sababu itazidi kudidimiza kiwango cha thyroid.

Subiri kwa muda kisha kama bado itakuwa kwenye hypo basi kuna dawa iitwayo Subiri kwa muda kisha kama bado itakuwa kwenye hypo basi kuna dawa iitwayo Levothyroxine.

Ila kwanza iache hiyo. Wasiliana na daktari wako kwa msaada zaidi.
Iliturn to hypo nkacontact na dokta akanambia niendelee so mwezi wa pili nlipima clinic Tena ikaja normal ila still nkabiwa niendelee nkapunguziwa dozi ila Sasa hivi takriban wiki tatu nakua naskia maumivu upande wa kushoto ktk kifua chini ya ziwa inshort upande wa moyo pia nakua namaumivu yakukereketa mwanzo wa Taya ktk shingo na upande wakulia
 
Grave disease na hashimoto ugonjwa mmoja ila reaction zake ndiyo tofauti. Inaposababisha hypothyrodism basi ni Hashimoto. Na ikiwa itasabisha hyperthyrodism basi hiyo ndiyo Grave disease.

Kwa muktadha huo ni kuwa, mwili hutengeneza askari kwa ajili ya kujilinda kutokana na maambukizi. Inapohisi kuna kirusi kimeingia basi askari huwajibika kupambana naye.

Lakini katika hali isiyo ya kawaida, kuna askari wanaanza kuishambulia tezi ya thyroid na kuiongezea kasi katika utengenezaji wa homoni. Huko ndipo hutokea Grave disease.

Endapo askari hao wakaishambulia tezi ya thyroid na kupunguza utengenezaji wa homoni basi hutokea hypothyrodism. Na ndipo huitwa hashimoto.
Daa umenielewesha vizur sana shukrani maana hata hospital sielekezwi hivi nimwendo wafaster faster tu
 
Back
Top Bottom