PostGE2025 Pingamizi la Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Baba Levo latupiliwa mbali, Kesi ya Uchaguzi

PostGE2025 Pingamizi la Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Baba Levo latupiliwa mbali, Kesi ya Uchaguzi

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Mafyangula

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2025
Posts
505
Reaction score
887
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Kigoma, imetupilia mbali pingamizi la awali lililowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na Clayton Revocatus Chipando maarufu kama Baba Levo, na hivyo kufungua rasmi mlango wa kusikilizwa kwa ushahidi katika shauri la uchaguzi la Jimbo la Kigoma Mjini.

Uamuzi huo umetolewa leo, Desemba 16, 2025, na Mheshimiwa Jaji Projestus Khayoza katika Shauri la Uchaguzi Namba 28949 la Mwaka 2025, ambapo mahakama imewapa ushindi walalamikaji Johary K. Kabourou, Loum H. Mwitu, Pendo D. Kombolela na Luma H. Akilimali, wanaosimamiwa na Wakili John Seka.

Kupitia uamuzi huo, Mahakama Kuu imekubaliana na hoja za walalamikaji kuwa shauri hilo ni halali, lina msingi wa kisheria na limekidhi matakwa ya Sheria ya Uchaguzi pamoja na Kanuni za Mashauri ya Uchaguzi, hivyo kuondoa kikwazo kilichokuwa kikizuia kesi hiyo kusikilizwa kwa misingi yake.

Hapo awali, walalamikiwa kupitia mawakili wao waliwasilisha pingamizi la awali wakiiomba mahakama itupilie mbali shauri hilo kabla ya kusikiliza ushahidi, wakidai kuwa kulikuwa na mapungufu katika Aya ya Uthibitisho wa hati za shauri, pamoja na hoja kwamba walalamikaji walipaswa kuomba msamaha wa dhamana ya gharama za kesi hata kama walikuwa na hati ya msamaha kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS). Aidha, walalamikiwa walidai walalamikaji hawakuwa na mamlaka ya kisheria kuomba baadhi ya nafuu ikiwemo upekuzi na uhesabuji upya wa kura.

Source: Jambo
 
Jamaa yake siku ile anamnadi kawatukana wasomi wote wenye degree kwamba ni mafala wafanye kazi...
Hiyo ni kawaida ya aliyebahatika kushiba,hawezi kumbuka yupo,wapo waliolala njaa pindi yeye ameshiba.
 
Kumeanza kuchangamka, ngoja tusubiri jini mkata kamba pale chamwino atalimaliza vipi hili.
 
Mchezo huo wanataka kumkata ili kuwapa furaha bandia wananchi..!!

Mtasikia mengi yote ili tusahau MO29
 
Baba levo ameshachokwa haraka sana kupitia uchaguzi batili uliompa ushindi feki
Huo ni mchezo wa Ccm na Act kututoa kwenye reli
Wewe mkongwe unadanganyikaje kirahisi

Mahakama za ccm zinatafuta kujisafisha Kwa upinzani
 
Simpendi Baba Levo na CCM yake lakini naona bora aendele kuwa mbunge ili huyu msaliti, mdini na mnafiki Zitto Kabwe azidi kunyooshwa.
 
Back
Top Bottom