Pingamizi la CHADEMA Arumeru latupwa nje na NEC


Mkuu maneno yako sadkta kabisa ili iwe fundisho hapo mbeleni .
 
unajua bwana sheria sio mambo ya propaganda lazima uwe na ushahidi wa juu ya unalolizungumza.nadhani sasa ni wakati wa kujikita ktk kampeni na kunadi sera ili mwisho wa siku wana arumeru waamue mchele ni upi na pumba ni zipi.

Kuna ushahidi zaidi ya barua ya immigration iliyosema SIOI hakuukana uraia wa Kenya alikozaliwa alipofikisha miaka 18!!?
 
..Naomba ufahamu tu; inaonesha CDM hawakupeleka uthibitisho unaoonesha kuwa SIYOI alizaliwa Kenya; kama vile cgeti chake cha kuzaliwa; ndio maana NEC wanasema hakuna uthibitisho wa uraia wa Kenya. Kwani kama alizaliwa huko basi ni raia wa huko. Je, uthibitisho wa kuzaliwa huko UPO?
 
CDM pingamizi lenu ndiyo hivyo limetupwa sijui mtakuja na nini tena! Kote huko ni kutapatapa tu mambo ni magumu Arumeru.
Ingekuwa vyema zaidi kama ungetuambia ni kigezo gani kilichotumika ktk kufikia maamuzi hayo, otherwise wewe ni great sinker.
 

Nilifikiri Sioi naye angeitwa ili kujibu allegations, kisha Tume kutoa maamuzi!!
 
Bashe alitemwa na CCM na sio tume jamani, tujaribu kuweka kumbukumbu vizuri

Chadema wa-file kesi Mahakama kuu huku wakiendelea na kampeni (maana hata Siyoi angetemwa bado uchaguzi ungefanyika). Hii itawasaidia CDM kama Mahakama kuu ikiukataa uraia wa Siyoi na kwa mtazamo wangu, ikiwa Mahakama itamtangaza Siyoi kuwa si Raia hata kama atakuwa kachaguliwa, atapoteza Ubunge na Watanzania watapata nafasi ya kujua umakini wa CCM vs CDM.
 
Na hakika CDM na jopo lake la wanasheria walikuwa wanajua kabisa kwamba Sioi sio Mkenya kwa mujibu wa sheria ya urai Tz, isipokuwa walitest zari baada ya kuifuma barua ya Afisa uhamiaji aliyeshinikizwa kumtosa Sioi kwa barua iliyotakiwa kufikishwa mbele ya kamati kuu kimya kimya ili kumuengua kwenye uteuzi
 
NEC wanaweza wakawa wamefunika kombe kwa sasa lakini huko mbele ya safari ccm watapata shida sana na hii hukumu. Wameweka precedence kwa kutafsiri sheria ya Uhamiaji ya Tanzania na Kenya kwa pamoja! Na hapa ndio kwenye tatizo maana sheria ya Tanzania haisemi kuwa uraia wa mtu aliyezaliwa nje ya mipaka utaangaliwa kufuatana na sheria za huko alikozaliwa. Time will tell.
 
Kuna uhusiano gani Kati ya mgombea wa arumeru na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi? What does the rule against bias say? Je alideclare interest zake Mara baada ya hii issue kuvuka mezani kwake?

Majibu ya masuali haya ndio Tutajua ni kwa nini tume ya uchaguzi imevaa madaraka ya mahakama na kuendelea hata kutengua uamuzi wa mahakama ya rufaa.

Kulikuwa na concern kubwa wakati wa uteuzi wa mwenyekiti wa Tume watu tukapuuzia
 
Mkuu unajaribu kusema nini hapa?
Tume imetimiza wajibu wake kisheria, sasa kama haujafurahishwa na matokeo jenga hoja kwanini Sioi ni Mkenya na tume imeamua sio Mkenya
Sheria za urai zipo wazi kabisa, fafanua
 
Mkuu unajaribu kusema nini hapa?
Tume imetimiza wajibu wake kisheria, sasa kama haujafurahishwa na matokeo jenga hoja kwanini Sioi ni Mkenya na tume imeamua sio Mkenya
Sheria za urai zipo wazi kabisa, fafanua

Siko yuko kwenye sheria za uraia, niko kwenye rule against bias. Kuna uzi ulitundikwa humu kuhusu uhusiano wa mwenyekiti wa tume na baba mkwe wa sioi. Sikumbuki kama imewahi kukanushwa hadharani. Kama huo uhusiano upo basi definitely na sioi ana uhusiano na mwenyekiti wa tume.

Katika misingi hiyo mwenyekiti alitakiwa kudeclare interest zake kwenye hili suala, hata Kama sio yeye aliyeamua anaweza kuwa ameinfluence by necessary implication kutokana na nafasi yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…