Pinda: Uvumilivu ukimshinda Kikwete msimlaumu - Onyo Chadema

Mhe Pinda leo amelonga hapa Bukoba mida ya saa 12 na kusema

Pamoja na serkali kuleta maendeleo makubwa Kagera. Pamoja na shule, barabara na mkonga wa mawasiliano.

Bei ya sukari ataishughulikia katika ziara yake. Bukoba ni km 70 toka kiwandani. Hadi tar 8 itatelemka bei.

Kuh amani ya nchi anasema Kikwete amewavumilia sana watanzania. Anasema maandamano haya yanapima uvumilivu wa Kikwete. Ila anasema anavyojua yeye uvumilivu wake unakaribia mwisho. Watu wenyewe hata mabomu mnaogopa, likipigwa moja watu wanakimbia wala hakuna hata mmoja anayesimama. Karibu sasa atasema basi na hapo ndipo mtakapo ona cha moto.

My take baby face anatishia amani ya tz na kujenga hofu katika mioyo ya watu kuwa wakati wowote watashambuliwa na vyombo vya dola.

Anayemvumilia mwenzake ni nani? Wananchi ndio uvumilivu wao umekoma watakiona cha moto wataondoka Magogoni kwa viboko.
 
Hizi ni dalili kuwa kile wakitakacho waTanzania hawawezi tena kukitekeleza. Watuachie nchi yetu kwa kukaa pembeni kiungwana vinginevyo umma nao utaamua hatima yao.
<br />

<br
/>
Nasikia umma.....umma... ni upi huo mnaouzungumzia?hawa wanaofika katika maandamano?lakini wengi hawakuwa wafuasi wa CDM ila walifata agenda ya kupinga Dowans asilipwe,sasa kama ushiriki wao ndio umekuwa mtaji wa kudhani chama kimepata wafuasi imekula kwenu?
 
Huyu pinda ni mjinga anachokisema kiko kinyume, mimi kama mwananchi mimi ndo nina haki ya kusema nimekuvumilia mkwere na wenzako
sasa nimewachoka inabidi m resign, sasa ww
pinda unanitishia mimi raia ambaye nimekuajiri unaniambia umenivumilia vya kutosha? Huo ujasiri wa kutamka hayo unatoa wapi? Kama nikitaka kuandamana mwaka mzima si ni haki yangu! Unanitishia kuandama kwangu kweli wewe pinda ni mfano halisi wa viongozi wajinga, na ni bora ulizaliwa tz na ukapata uongozi tz ambako hamna neno uwajibikaji kila kitu mnafanya mazoea.
<br />
<br />
Sikiliza bwana mdogo,nguvu ya umma huwa haiamshwi na wanasiasa kama wanavyofanya Slaa na kundi lake.Umma unapozidiwa usimama wenyewe na wanasiasa wakatokeza baadae.Hii ya CDM si nguvu ya umma ni Chama cha siasa katika uzushi ili kupata member wa kudhani watakifikisha ikulu baada ya ballot box kushindikana.Huu ni uchochezi na hakuna nguvu ya umma hapa dogo.
 
hivi huyu mtoto wa mkulima amekuja kuwaje! Mbona niaje niaje hapa nani anamvumilia mwenzake sisi au wao? Na tena uvumilivu wetu ndo huo unakaribia kukoma sidhani kama tutavumilia hadi 2015 kwa hali hii! kama sisi mmetupa jukumu la kuelimisha watoto wenu afu hamtulipi? Mnacheza nyie hadi leo baadhi yetu no salary ingawa pia hautoshelezi unasema nyie ndo mnatuvumilia! Aisee acha masihara PM siku tukichoka kuvuilia mtafrahi otherwise mtuboreshee hali zetu watz wa kawaida ingawa kwa elimu zetu hatukupaswa kuwa na maisha haya. Tunasurvive sababu ya title mwalimu tunakopeshwa, na kusaidiwa like ombaomba unadai mnatuvumilia aisee angalia hii mambo ooohoo, mbali na matatizo yote tunaenda kazini daily tunafundisha afu mnadai mnatuvumilia aisee. Kiukweli hiyo kauli kuwa uvumilivu wa JK una mwisho imeniuma na kunikasirisha saana wakati sisi ndo tunawavumilia nyie afu ktk perspective yenu nyie ndo wavumilivu kweli mmelewa madaraka yani mko ridhimu mbaya hata hamuoni poa lkn one day yes
 
CDM wametumia mapungufu yaliyoko kwenye katiba ambayo katika ilani yao ya uchaguzi walisisitiza tuifanyie marekebisho. Kwa sasa imekuwa kero kwa chama tawala na kuna hatari ya kutumia nguvu za dola kuwarudisha nyuma wasiimarishe chama chao tena kwa matamko tofauti tofauti. Katika hili nashauri anayevunja sheria achukuliwe hatua za kisheria, anayetaka kukiimarisha chama chake kisiasa tupambane naye kwa hoja za kisiasa. Matumizi ya mabavu iwe kwa dola au chama chochote cha siasa ni hatari kwa ustawi wa Taifa. Daima mwiba hutoka kupitia mahali ulipoingilia. TAFAKARI.
 
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewaonya wakazi wa Manispaa ya Bukoba na Watanzania wote kwa ujumla kuacha kuchezea hali ya amani ambayo imekuwepo kwa muda mrefu hapa nchini.

Ametoa onyo hilo jana jioni (Ijumaa, Machi 4, 2011), wakati akijibu risala ya Wazee wa Manispaa hiyo ambao waliwaomba Watanzania wote waitunze amani na wasikubali kudanganywa na kauli za uchochezi zenye lengo la kuwatia hofu na kuwakatisha tamaa.


Akizungumza na maelfu ya wakazi wa Manispaa ya Bukoba kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Mayunga (Uhuru Platform), Waziri Mkuu alisema: "Wana-Kagera mnajua maana ya vita kwa sababu mmepata rasharasha mwaka 1972 wakati Idd Amin aliposema anataka aje kunywa chai Mwanza lakini ninyi pia ni mashahidi wa vita halisi ya mwaka 1978," alisema.


"Hivi majuzi tumepata matatizo kule Gongo la Mboto, wakati watu wanakimbia kuokoa maisha yao, wako wengine waaliokuwa wakikimbilia kwenye nyumba za wenzao ili kuiba mali zilizoachwa. Ni ajabu iliyoje kumsikia mtu akitamka: Bora vurugu bwana!" alishangaa.


Alisema kama kamwe wananchi wasikubali uchochezi huo kwani maandamano na vurugu siyo suluhisho na amani ikishapotea kuirudisha ni gharama kubwa mno.


"Kila kukicha, kuna watu wanazua madai ya kila aina, mara kura zimeibiwa, mara Katiba mpya; walichoamua ni kutembea nchi nzima &#8230; pengine hawana kazi za kufanya ndiyo maana wanatembea kuitisha maandamano huku na kule," alisema.


Alisema: "Kama suala ni kuing'oa CCM madarakani ni laima wajiulize maswali ya msingi ni vipi wataweza kuindoa CCM katika matawi, mashina, kwenye kata na tena mjijengee uhalali kwa wananchi hadi wawakubali."


"Msipofanya hivyo, mtatembea weee lakini CCM haingoki ngo!," alionya na kuongeza kwamba: "Uongozi unategemea wananchi wanavyotutazama&#8230; wanatupima, je watu hawa wataweza kutusaidia? Je watajali shida zetu?" alitahadharisha.


Mapema, katika risala yao iliyosomwa na Mzee Haruna Almasi, wazee hao waliomba kupatiwa matibabu bila mlolongo mrefu ili wasihangaike. "Tunaomba Serikali ituwekee utaratibu mwepesi wa kuwasaidia wazee kupata tiba&#8230;", alisema Mzee Almasi.


Wazee hao ambao walisema wanaiunga mkono hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa Februari 28, 2011 wakati akilihutubia Taifa, pia waliomba kuwe na uwakilishi wa wazee katika ngazi mbalimbali za vikao vya kufanya maamuzi kuanzia kwenye Serikali za Mitaa hadi Bungeni.


Kesho (Jumapili, Machi 6, 2011), Waziri Mkuu atakuwa wilayani Chato ambako anatarajiwa kuweka jiwe la msingi katika jengo la Halmashauri ya Wilaya hiyo na kufungua SACCOS ya Mshikamano kabla ya kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara kwenye shule ya msingi ya Chato.




IMETOLEWA NA:


OFISI YA WAZIRI MKUU,

JUMAMOSI, MACHI 05, 2011


FBlukuwi said:
Hivi karibuni nimeshangazwa na mambo ya hawa viongozi wetu kuanzia JK na mawaziri wake kudai kuwa watu wanaoandamana wanataka kuiangusha serikali yake na hii kauli ya Pinda ndo inanichefua kabisa. kitendo cha serikali kudai kuwa kuandamana kitamaliza uvumilivu wa JK ni umbumbumbu na ulevi wa madaraka. Wanasahau kuwa haki ya kukusanyika ni ya kikatiba na mtu yeyote anayezuia hilo anaivunja katiba yetu.

JK au mtu mwingine yeyote hana madaraka ya kuzuia watu wasiandamane apende au asipende. kinachonisikitisha ni kuwa hawa viongozi wanataka watu wote wafanye wanavyotaka wao.

Kikubwa cha viongozi hawa wanachoweza kufanya ni kumshitaki mtu anayevunja sheria bila kuathiri haki ya kuandamana. Hadi sasa hawajamshitaki mtu yeyote kwa kuvunja sheria kwenye haya maandamano. Cha kusikitisha zaidi hawa NCCR, TLP na UDP nao wamejiunga na wenzao CCM kuponda CDM. So far mimi sijaipata hofu ile aliyonayo JK kuhusu usalama wa nchi yetu. mi nadhani ana hofu yeye na familia yake labda wamewakosea watanzania sasa wananchi waamka!

Go CDM tunawahitaji huku Mbeya, Iringa na Songea!
 
Kwa michango hii nasi tunajiita GREAT THINKERS !!! badala ya kutoa mawazo ya kujenga regardless ya vyama mnavyovifuata iwe CDM iwe CCM mnabaki kusengenyana!!, kwa mwelekeo huo tunategemea maendeleo ya nchi hii yatakuja kwa miujiza! I DON'T THINK so. Inaonekana kama vile wote tuna corrupted minds, what is this!
 
Nimesoma comments zote watu mlizoandika kuhusu hili lakini hakuna hata moja yenye mashiko, zaidi ya kuruka ruka tu kama kuku aliyechinjwa na kuachwa. Alilosema Pinda ni sahihi kabisa, na wala hamtishi mtu, na hakuna hata mmoja mwenye ujasiri wa kupambana na dola pindi iki react. Wengi wenu mpo maofisini tu mna comment, pindi likitokea kasheshe hakuna hata mmoja anaejitokeza, acheni kuwaangamiza wenzenu, na acheni um chicha mwiba !

toa hoja acha upuuzi wako eti geniusbrain au una maana G spot? How can you be so foolish, am shocked au ni ajira?
 
Umeongea ya maana sana,viongozi wote sasa wana hofu ya kuachia madaraka kwa mwendo wa maandamano kama inavyotokea katika nchi nyingine sasa,na kwa kuwa wanajua fika kuwa wananchi wana maisha magumu na sababu ya kufanya hivyo ipo basi hawalali kwa amani na kujikuta wanaanza kuongea hovyo hovyo,nilidhani watawashtaki viongozi wa Chadema kwa kutoa matamshi ya uchochezi na kuvunja hiyo katiba lakini naona wamebaki kutishia na kulalamika tu.
 
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda *amewaonya wakazi wa Manispaa ya Bukoba na Watanzania wote kwa ujumla kuacha kuchezea hali ya amani ambayo imekuwepo kwa muda mrefu hapa nchini.

Amani anayozungumzia waziri mkuu ni ipi, polisi wanaua raia hovyo, wananchi wanashinda njaa, wananchi hawapati matibabu, wananchi hawapeleki watoto shule, bodo ya mikopo haitoi ikopo kwa wote, jeshi linashindwa kuharibu makombora mpaka yanaua wananchi wasio na hatia. wafanyakazi wanaenda kazini lakini hawafanyi kazi, mali ya umma inaibiwa kama vile ni haki ya watu wachache kuzichukua. Rasilimali zetu tunawapa wageni huku sisi tunatabasamu,Kweli hiyo ni amani

Kuwa kama kondoo sio kiashiria cha amani, absence of war does not necessarily imply peace.
 
Hiyo ndio sera ya mwisho ya watawala walioshindwa, Tanzania kuna utulivu tu lakini hakuna amani, watu waliomaskini wa kutupwa huwa hawana cha kupoteza, ukiwahubiria amani ni kama unampigia mbuzi gitaa. kwanza huyu Pinda kama amediliki kulidanganya bunge ndio unadhani ataogopa kuwadanganya Watanzania kwa ujumla wao? ikumbukwe na kila mmoja wetu kwamba punda ni kazi yake kubeba mizigo, lakini siku hakigoma hakuna wa kumlazimisha kubeba hiyo mizigo au kunywa maji, hapo ndipo wanapoelkea Watanzania kwa sasa enough is enough.
 
Wameshaanza kutapatapa. Tatizo wanamtumia mtu ambaye hawezi kujibu hoja zaidi ya kulia lia.
 
Hawswaaaaaaaaaaaaa! Si-huko tu mkuu, hata Tabora na vitongoji vyake CDM twaihitaji saaaaaaaaana. CCM wakumbuke kuwa kila jambo lililo na mwanzo sharti liwe na mwisho pia. Hivyo mwisho wa CCM sasa uko kiganjani.
 
Kuh amani ya nchi anasema Kikwete amewavumilia sana watanzania.

is he serious? nani kamvumilia mwenzake? mbona ni kinyume kabisa....wananchi ndio wamevumilia KIKWETE/CCM.


sasa hivi kila kiongozi wa chama na serikali wako mstari wa mbele kutoa vitisho...kuhusu madawa ya kulevya nchini hawachukui hatua yoyote,kesi za EPA walikua kimya, Richmond wakajificha, Gongo la Mboto na Dowans ndio husiseme.......

sasa hivi watu wanataka Raisi atoe "tamko" wanasingizia ni kuvunja amani.....haya ....
 
Alisema kama kamwe wananchi wasikubali uchochezi huo kwani maandamano na vurugu siyo suluhisho na amani ikishapotea kuirudisha ni gharama kubwa mno.

"Kila kukicha, kuna watu wanazua madai ya kila aina, mara kura zimeibiwa, mara Katiba mpya; walichoamua ni kutembea nchi nzima &#8230; pengine hawana kazi za kufanya ndiyo maana wanatembea kuitisha maandamano huku na kule," alisema.

Wenzetu ( libya tunisia na misri) mbona wameweza sisi kwa nini tushindwe, kama kuna watu wanadai kama anavyosema basi kuna ukweli ndani yake na serikali iliyokomaa lazima ikae chini na kusikia kilio cha wananchi wake na sio kutumia vitisho kujaribu kufifisha hoja halali za wananchi.

Kama hao wanaozunguka kudai haki serikali inawaona hawana kazi ya kufanya na badala yake wanasimama kwa niaba ya wananchi kudai madai halali , basi wao ni bora zaidi kuliko watu waliopewa kazi na wananchi kuwaletea maendeleo na badala ya kufanya hivyo wamekuwa wakisinzia ofisini, kusafiri nje ya nchi na kulalamika kuwa Nyerere kashindwa, Mwinyi kashindwa, Mkapa kashindwa basi na sisi hatuwezi kumaliza matataizo ya nchi.

Kama hamuwezi mnagoja nini? Mlichaguliwa kwa sababu mlisema mnaweza kwa sababu mmekiri hamuwezi hamna sababu ya kuendelea kuongoza jahazi.
 
Hizi ni dalili kuwa kile wakitakacho waTanzania hawawezi tena kukitekeleza. Watuachie nchi yetu kwa kukaa pembeni kiungwana vinginevyo umma nao utaamua hatima yao.
Sasa tutajiongoza vp raia bila ya kuwa na kiongozi? siungi mkono Cdm, slaa toka ashindwe anahaha kutaka kuiongoza nchi,hii inaonesha ni jinsi gani hili bachela lamiaka 65 linavyopenda kuongoza maana kwa sasa sio mbunge/rais basi lengo lake lianzishe vurugu ili ligombanie tena ubunge ili arudi bungeni,slaa u must accept defeat,mie nataka jeshi lichukue nchi,CCM msiilipe Dowans kamata mafisadi tia jela otherwise mtaanguka 2015
 
Ukiwa unasoma maoni ya humu jf unaweza ukadhan bongo sasa hali c shwari yaan wkt wwt chcht kinaweza kutokea hasa kwa wananchi wa nchi hii kufanya haya ambayo humu jamvini tunayasema...jaman wantanzania walioo wemg bado hawajafika kwny maamuz tunayoyaota humu
 
Back
Top Bottom