Ni kweli utawala wa JK umekuwa wa kiujanja ujanja,fitina, udugu, chuki na makundi. Hili jambo siyo siri ndivyo alivyoingia pia kwenye madaraka ya urais. Watendaji wake wamekuwa hawamwamini kwa jambo lolote, hata wanapotaka kfanya maamuzi yoyote hata kwenye nafasi walizo na dhamananazo huhofia bosi wao atawaonaje. Hili pia limejidhihirisha pale waziri anaposema lingekuwa langu ningeamua hivi, lakini kwa sababu kuna mkubwa wangu siwezi kuamua. Tafsiri rahisi ni kuwa maamuzi hayapo kiserikali yako more Personal kuliko kuwa oficialised.
Lakini wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM wa mwaka 2015 wamemthibitishia JK kuwa CCM si chama cha wajanjajanja kwa kumchagua Magufuli kwa kuangalia umahiri utendaji kazi wake.
Ni kama uchaguzi wa mwaka 1985 wakati Nyerere alimwandaa Salim Ahamed Salim kuwa mgombea wa rais kwa kuangalia uchapakazi wake akisindikizwa na mtu aliyedhani dhaifu Ali Hassan Mwinyi, lakini wajumbe wakamchagua Ali Hassan Mwinyi kwa kuangalia Upemba na Uunguja. Wakakataa kuwa rubber stamp wa Mwalimu. JK alimtaka Bernad Membe au Rose Migiro lakini akitaka asindikizwe na John Pombe Magufuli, wajumbe wa Kamati kuu na Mkutano Mkuu wamekataa kuburuzwa na JK wakamchagua John Pombe Magufuli.
Kingunge nimemzungumzia sana katika uzi mwingine nisingependa kurudia lakini itoshe kuwa maoni yake hayako huru kwa sababu yupo kundi la Lowasa hivyo anakosa uhalali wa kuwa hakimu katika shauri alilo na maslahi nalo.