hiki kitu kimenishangaza,yaani kamati ya maadili ilikosa imani kwa jaji mkuu ambaye ni kiongozi wa mfumo wa utoaji haki,waliona nini kwa huyu bwana ramadhani,kamati ya maadili ilikosa imani na msaidizi wa karibu wa rais,makamu wa rais gharib bilal,na pia waziri mkuu,hawa ni watu wa karibu sana na rais,membe naye kapigwa chini na kuvunja mila ya waziri wa mambo ya nje kuwa rais kama ilivyotokea kwa mkapa na kikwete,hakika awamu ya nne ilikosa muelekeo
Mkuu bora Membe alifikishwa kwenye vikao husika na akabwagwa kwa njia ya kura! Ila Kamati haikuwa na imani na Makamu wa Rais na Waziri Mkuu ila ikawa na imani na Naibu Waziri! Kwa siku zilizobakia Rais anapokuwa nje ya nchi atalazimika amwachie nchi huyo Naibu Waziri au itakuwaje? Hao hata wakiachiwa watakuwa na moral authority ya ki-uongozi kweli? Au ndo bora liende mpaka siku ziishe?