Pinda akubali kujiuzulu jioni hii

Status
Not open for further replies.
Duu Waziri mkuu sikuzote amekuwa ni wakuficha madhaifu ya Maraisi wetu. Waziri mkuu wetu hana madaraka ya kisheria na kikatiba ya kuwawajibisha viongozi walioteuliwa na raisi. Hana uwezo hata wa kumsimamisha kazi mkuu wa wilaya. Lakini wakati unapofika inabidi awajibike hata kwa makosa ya watu asioweza kuwawajibisha. Kuna haja ya kufuta cheo hichi kwenye katiba pendekezwa au kumpa madaraka waziri mkuu ya kuwafukuza watendaji dhaifu. BILA hivyo lawama zitaendelea kuelekezwa kwa mawaziri wakuu ambao kwangu nawaona kama wanaficha uchafu na udhaifu wa mfumo raisi. Mwangalie kawawa enzi zile, mwangalie malecela enzi zile, mwangalie msuya enzi zile ,mwangalie Sumaye Enzi zile ,Mwangalie lowassa enzi zile, mwangalie Pinda sasa. Tatizo ni mfumo raisi tulionao. Kwaheri Pinda laikini tushirikiane kufuta cheo hiki au kuongeza madaraka ya nafasi ya waziri mkuu aweze kuwafukuza hata mawaziri wasiotekeleza maagizo yake.
 
Katika utawala bora Pinda, Prof. muhongo, Ag werema na Maswi walipaswa kuwa wamejiuzulu mara tu baada ya taarifa ya CAG. Maana walisema zile pesa za tegeta escraw ni za Watu binafsi uchunguzi wa CAG ukasema za Umma.

Hapa kama wanagoma kujiuzulu inaonyesha walivyosema ni za binafsi walikuwa wanamaanisha wameshazifanya za kwao eti?
 
BABU PETER KAYANZA MIZENGO PINDA
majina yote manne yana dhihirisha hatua unayotaka kuchukua .pita_yaan aondoke apite_kayanza...yaan ndokayanza mapito.mizengo_mambo yame mwendea mazengo. yaan kiatu cha kulia kavaa kushoto kushoto kavaa kulia.PINDA yaan hapo ndo mambo yamepinda vibaya.
 
Kumbuka Na Mbowe naye wanamtaja taja...

Kama Mbowe naye yupo ataenda na maji.. Chadema sio Mbowe wala Dr. Slaa.. Kwa sasa orodha tuliyonayo ni ya mawaziri na wabunge wa ccm.. wafanyakazi wa TRA pamoja na viongozi wa kiroho ambao wamesahau maadili yao ya kuwaongoza kondoo wa Bwana bila ya kuwasahau waheshimiwa majaji wa mahakama zetu hizi..

Stay tuned..
 
Ungesema kajikabidhi polisi ili kesho apelekwe mahakamani tungekuelewa
 
Taarifa zilizonifikia japo sijazibitisha ni kwamba waziri mkuu pinda amekubali yaishe kwenye kikao cha uongozi bungeni kilichodumu kwa zaidi ya masaa matatu. Stay tune

Mambwa hao, hata wajiuzulu vipi haiwajengei heshima tena. Wameiba wameiba wameiba wameiba wameiba wameibaaaaaaaaaaaaa


Wezi lazima tuwachome moto tarehe 14/12/2014
 
Mambwa hao, hata wajiuzulu vipi haiwajengei heshima tena. Wameiba wameiba wameiba wameiba wameiba wameibaaaaaaaaaaaaa


Wezi lazima tuwachome moto tarehe 14/12/2014


Safari lazima tuwapeleke jela
 
Mtu anafanya kazi miaka 35 serikalini tena kwenye managerial post, ukijumlisha mshahara na pensions zake havifiki hata million 160m lakini hawa jamaa anapiga dili lake anapata 5b alafu anajiuzulu. Then wanakuwa wanamuita 'mstaafu' na wala sio aliyejiuzuru huku akiendelea kula pension, matibabu bure. Kwa ufupi anakuwa anaishi maisha mazuri hata zaidi ya Bakhresa, nasi kweli tuendelee kucheka bila hata kurudisha japo 5% ya alichoiba!?
 
Kuna habari za kuaminika kuwa KINANA atapewa UWAZIRI MKUU mara baada ya PINDA KUNYOOSHWA jioni hii.
Source: Tembo ( Mikumi).
 
Updates:

Ni kweli amekubali ila amesema hatma yake itategemea majadiliano ndani ya bunge, ikiwa wabunge wataamua kwa kauli moja kuwa niondoke nitaondoka, amesema pinda.

Werema naye amekubali kujiuzulu.


Tibaijuka naye karidhia

Ila muhongo ndo bado.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom