Pinda adanganya tena bungeni

Pinda adanganya tena bungeni

Isango

R I P
Joined
Jul 23, 2008
Posts
295
Reaction score
450
Nahisi kuwa watu wa usalama, au washauri wa viongozi wetu wakuu sasa mmezidi kukosea, na kuwakosesha viongozi.

Mizengo Pinda Waziri Mkuu anahutubia Bunge ili kuahirisha na kudanganya kuwa Askofu Amedeus Msarikie AMEFARIKI USIKU WA KUAMKIA LEO, wakati hata stori za kuhusu kifo hicho zimekuwa kwenye Mitandao tangu jana, vipi viongozi hawa?

Kweli ndio Maana Rais alisema MwanaHALISI limeandika habari za wanajeshi kuasi. Kwa kuwa vijana wetu wanaolipwa na kula ubwabwa wa serikali hawafanyi kazi, tunawatumia tangazo lililotolewa na Baraza la Maaskofu Tanzania tangu jana, kuwa Askofu alifariki Usiku wa kuamkia jana, sio usiku wa kuamkia leo kama Waziri Mkuu anavyodanganya Bungeni.....

... vipi TBC leo ipo Analogy mbona matangazo hayo pamoja na kuwa yanadanganya yanakatikakatika, au wanataka tusiunganishe sentensi za kudanganywa?
 

Attachments

tanzania, waziri mkuu hana uwezo wa kusema uongo.
 
Ameleweshwa na ASALI!!kalamba nyingi
 
Waziri mkuu muongo, mawaziri waongo wambea sijui kama tutafika.
 
Nitarudi baadae maana naona kama kwenye hili tangazo kuna tatizo. Ngoja wataalamu waliangalie vizuri.
 
Viongozi wetu wanasoma tuu walichoandikiwa bila kuhariri. Nangojea siku “KICHAA” Mmoja atakapo mwandikia PM hotuba yake na kuchomeka “.....namshukuru sana mhe. Rais Dr Slaa kwa hamasa anayotupatia katika kuleta maendeleo ...” Naye akaisoma hivi hivyo. Ndiko tunakoelekea.
 
Namshauri Pinda awe anatembelea JF kwani asingebabaika kujua askofu alifariki lini coz humu ilirushwa dakika chache baada ya kifo cha askofu.
 
Kwa kweli ni muhimu sana jukwaa hili likatenga uzi maalum kujadili 'uongo' wa waziri mkuu, maana askofu hakufariki muda huo aliosema waziri mkuu. Naomba CDM iandae maandamano ya nchi nzima kuonesha hili ili nchi yetu izidi kusonga mbele...pipooooooooozzzz
 
Isango the great, nimekupata mwana habari.

Sasa sisi inatuhusu nini kafa jana au leo watu wengine munakosaga vitu vya kuandika mtu akifa akazikwe huu mfumo kristo sijui utakwisha lini eti bunge linatangaziwa askofu fulani kafariki "IGNORANT PEOPLE"
 
Kwa kweli ni muhimu sana jukwaa hili likatenga uzi maalum kujadili 'uongo' wa waziri mkuu, maana askofu hakufariki muda huo aliosema waziri mkuu. Naomba CDM iandae maandamano ya nchi nzima kuonesha hili ili nchi yetu izidi kusonga mbele...pipooooooooozzzz


MJEPU hapo nilikoweka Bluu, na wewe unahusika. Suala la Waziri Mkuu kudanganya, na tangazo ambalo limetolewa, linahusu nini na CDM?, na waandamane kwa suala gani hapa? Any way wapo watakujibu!
 
Hiyo thread binafsi sijaielewa.Sioni essence ya udanganyifu
 
Sasa sisi inatuhusu nini kafa jana au leo watu wengine munakosaga vitu vya kuandika mtu akifa akazikwe huu mfumo kristo sijui utakwisha lini eti bunge linatangaziwa askofu fulani kafariki "IGNORANT PEOPLE"

Boko haram, mambo ya udini yameingiaje hapa? soma upya hoja inayojadiliwa
 
Back
Top Bottom