Pigo la kwanza kwa Simbachawene

Pigo la kwanza kwa Simbachawene

Mmh... Hizi?
MshanaJr ndiyo imani zenyewe hizo tuziheshimu kwa sababu kuna watu wanaziamini.

Wazungu hawakuziheshimu za kwetu wakaziita za kishenzi, nasi tumeamua kufuata humo humo kuziita za wenzetu vibanda imani.

Bado ukoloni uko katika bongo zetu
IMG-20200204-WA0206.jpeg
IMG-20200204-WA0205.jpeg


Jr
 
Off course hayo mengine in udhalilishaji na ni kinyume cha hata na maadili ya kiafrika. Sitetei imani za kudhalilisha
 
Kuna kitu kimemuingia huyu mama, siku ya kwanza alionekana ktk video akikemea aina ya mahubiri ya nabii. Tena alishangazwa atawezaje kutatua matatizo ya watu wengi vile kwa wakati mmoja!!, akaenda mbali zaidi kwa kusema Alichokiona pale ni biashara, kila kitu kinauzwa tena kwa bei ya juu. Maji ya 700, yanauzwa 1000. Mama ghafla kabadili msimamo wake.

Mungu ameingilia Kati ndo maana hata Mh Rais amekaa kimya
 
Hakuna wa kumfunga paka kengele.
Ulinzi ulikuwa mbovu - polisi ilaumiwe
Utaratibu wa ugawaji mafuta ulikuwa mbovu- mchungaji alaumiwe
Waumini walikosa ustaarabu - waumini walaumiwe
Waziri katoa tamko la haraka kabla ya mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama hajanyoosha maelezo - waziri alaumiwe
RC kuwa na kauli mbili tofauti kabla na baada ya kutuambia kaongea na rais - rc alaumiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yule mama RC ni mtu mnafiki na ni mtu mwenye ndimi mbili, juzi mchana alikuwa live na star tv alisema anashangaa kwanini mafuta yaliwekwa mlango mmoja tu wakati uwanja una milango mitatu na akahoji kwanini alizidisha muda aliyopewa toka saa 6 mchana hadi saa 12 jioni maana mkanyagano umetokea kati ya saa moja na nusu jioni hadi saa 2 usiku

Akalaumu imekuwaje Mwamposa kakimbia wakati hadi maafa yanatokea alikuwepo kabla hajapotea ghafla na lawama kadha wa kadha kwa mwamposa lakini nashangaa jana wakati wa kuaga miili anayakana maneno yake yote na kujigeuza kuwa Wakili wa Mwamposa, nahisi kapewa amri toka juu au kala mlungula.
Mkuu si amekwambia amepigiwa simu na Rais,hapo ndipo palipoleta mabadiliko...
Nasikia Mwammposya na Meko wanakutana usiku Gamboshi.Kwahiyo chama kimoja mwendo wa Kafara tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kapokewa ofisini na vifo mfululizo. Ukiachana na vifo vya majanga asilia ya mvua nk. Kuna haya yaliyotokana na mwenendo wa matendo ya kibinadamu

Kabla hata hatujamaliza wiki ya kwanza ya mwezi wa pili tayari tumeshapoteza Watanzania wenzetu wasiopungua 40 kwenye matukio mawili tu. La mkanyagano Moshi kwenye kongamano la kidini.. Na vijana wetu 10 wa JKT waliopoteza maisha kambini Msata..

Hili la JKT taarifa rasmi bado lakini la Moshi tayari matamko yenye kukanganya yameshatolewa na viongozi mbali mbali. Wa kwanza kutoa Tamko na ambaye ni mhusika mkuu ni Waziri wa mambo ya ndani. Na alitoa angalizo zuri kuhusu sasa kuvifuatilia hivi vibanda na mabanda ya imani na shughuli zake. Amepongezwa na wengi

Kwa mstuko wa wengi jana kwenye shughuli za kuaga marehemu waliopoteza maisha yao kwenye kongamano la kukanyaga mafuta mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro alisema hakuna haja ya kuzuia shughuli kama hizo na waliosababisha mkanyagano ni vijana vibaka waliotoka nje wakitakaa kuingia ndani

Mkuu wa mkoa kajuaje kuwa walikuwa vibaka na si watu wengine wowote?
Mkuu wa mkoa hakuzungumzia kuhusu hali ya ulinzi na usalama wa eneo husika
Mkuu wa mkoa hakuzungumzia muda ulioongezeka nje ya muda wa kibali
Mkuu wa mkoa hakuzungumzia kuhusu uzembe na uwajibikaji wa pamoja kwenye swala zima.
Sana sana amemkata kalima Waziri mwenye dhamana na sasa hawezi tena kuendelea kuchukua hatua alizotaka kuchukua.
Kwa hali ilivyo hakuna atakayewajibika wala kuwajibishwa....

Je, Mwamposa ni mkubwa kuliko mamlaka? Badala ya viongozi kuungana kukemea haya yanayotendwa na hawa viongozi wa dini janja janja ndio kwanza wanahamasishwa...

Jr
Kwetu lakusikitisha zaidi na zaidi ni vijana waliofia mafunzoni, nina uhakika hatutapata maelezo yaliyokamilika, ukifa jeshini tena mafunzoni inakuwa shughuli, kwanza upelelezi ni wao, sidhani kama wanawashirikisha polisi wetu wa kawaida, dola inakuwa na usiri mno kwenye vifo visivyoeleweka huko jeshini, RIP makamanda, ukweli utajulikana tu...
 
waumini wa hawa manabii feki huwambiii kitu nakwambia

sijui wanalishwaga nini huko kwenye ibada wanazoendaga
 
Back
Top Bottom