Kapokewa ofisini na vifo mfululizo. Ukiachana na vifo vya majanga asilia ya mvua nk. Kuna haya yaliyotokana na mwenendo wa matendo ya kibinadamu
Kabla hata hatujamaliza wiki ya kwanza ya mwezi wa pili tayari tumeshapoteza Watanzania wenzetu wasiopungua 40 kwenye matukio mawili tu. La mkanyagano Moshi kwenye kongamano la kidini.. Na vijana wetu 10 wa JKT waliopoteza maisha kambini Msata..
Hili la JKT taarifa rasmi bado lakini la Moshi tayari matamko yenye kukanganya yameshatolewa na viongozi mbali mbali. Wa kwanza kutoa Tamko na ambaye ni mhusika mkuu ni Waziri wa mambo ya ndani. Na alitoa angalizo zuri kuhusu sasa kuvifuatilia hivi vibanda na mabanda ya imani na shughuli zake. Amepongezwa na wengi
Kwa mstuko wa wengi jana kwenye shughuli za kuaga marehemu waliopoteza maisha yao kwenye kongamano la kukanyaga mafuta mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro alisema hakuna haja ya kuzuia shughuli kama hizo na waliosababisha mkanyagano ni vijana vibaka waliotoka nje wakitakaa kuingia ndani
Mkuu wa mkoa kajuaje kuwa walikuwa vibaka na si watu wengine wowote?
Mkuu wa mkoa hakuzungumzia kuhusu hali ya ulinzi na usalama wa eneo husika
Mkuu wa mkoa hakuzungumzia muda ulioongezeka nje ya muda wa kibali
Mkuu wa mkoa hakuzungumzia kuhusu uzembe na uwajibikaji wa pamoja kwenye swala zima.
Sana sana amemkata kalima Waziri mwenye dhamana na sasa hawezi tena kuendelea kuchukua hatua alizotaka kuchukua.
Kwa hali ilivyo hakuna atakayewajibika wala kuwajibishwa....
Je, Mwamposa ni mkubwa kuliko mamlaka? Badala ya viongozi kuungana kukemea haya yanayotendwa na hawa viongozi wa dini janja janja ndio kwanza wanahamasishwa...
Jr