Picha. . . .

nyumbani kwangu nina sanduku maalum linakaa darini,humo nimejaza bad memories zote,siku nikipigwa chepe watakaobaki duniani watajua wenyewe nini walifanyie.Ila hata mimi huwa najiuliza hao mahawara ambao tuki differ huwa tunatelekeza huko nguo (mpaka za ndani) baadae huwa wanazifanyia nini?

Bishanga utasababisha matatizo makubwa sana ukimaliza safari yako hapa duniani! Na hii inonesha wewe huwa hausamehe toka. Usifanye hivyo ndg yangu samehe na usiweke kumbukumbu
 
Julie kwani hivyo vitu ndivyo vinavyoita "baby come back" ??Unaweza ukachoma kila kitu na bado ukashawishika kurudi kama unashawishika kirahisi.

Mi nikibwagwa nimebagwa au nikibwaga nimebwaga no point of return
 
Kwenye mahusiano/ndoa watu hua wanapiga picha pamoja . . . kwa ajili ya ukumbusho.

Kwa wale mlioko facebook mnajua siku hizi hizo picha haziishi kwenye album makabatini tu na ukutani ila mpaka mitandaoni unakuta mmoja ana picha kibao za mwenzake bila kusahau description za ohh huyu ndie. . baby wangu and so so.Nimeona mmoja kajaza kweli za girlfriend wake nikajikuta najiuliza kama siku wakiachana atazifutilia tu mbali au itakuaje.

Swali. . .je ikiwa mahusiano yatavunjika zile picha mlizopeana na kupiga pamoja zinatakiwa zifanyweje?Ni sahihi kuziweka tu?Zinatakiwa zitupwe/chanwe. . . kama jibu ni ndio je za harusi?Ni sahihi kweli kuharibu/tupa picha unayopenda kisa tu uliyeachana nae yumo?Na kama ukiweka kuna madhara?

Lizzy, Just keep the memories alive.. those pictures were taken during the good old days. Even if you have partned/ fallen apart, the memories of the good days (which have been almost swallowed by the bad days) remain there and you can not erase it easily (unless you want to).
Keep it, you never know, sometimes there is baby come back...
 
mi nilizichana,nikazichoma moto,majivu nikayafunga kwenye kitambaa kichafu,nikatupa porini!

Feis buku, mbona unaonyesha ulipata hasira sana mdogo wangu, huyo shemeji alikutenda / kuukudhi nini kiasi cha kuhamishia hasira zote kwenye picha!!!
 
Lizzy umenikumbusha mshikaji wangu mmoja nilipotembelea fesi buku yake nilikutana na picha karibia 200 walizopiga yeye na girlfriend wake baada ya kama miezi minne hivi nikatembelea tena profile yake nikakuta ametoa picha zote hakuna hata moja halafu kwenye relationship status ameweka 'Its Complicated" nilicheka sana nikamwambia mara hii yamekuwa hayo...lol
 
Hehehe. . . yeah unamchana mhusika we unabaki na kipande kinachokuhusu.

lol...sa kipande changu kikibaki si kitanikumbusha tu kuwa hii picha tulipiga na mtu na tulikuwa mahali fulani kwa sababu fulani pengine?
 
za kuchana unachana
za kufuta unafuta
nguo na vitu vyake namrudishia ikiwezekana ikishindikana vitapigwa vibiriti
hakuna baby come back kama nilikaa, nikatafakari na kuchukua uamuzi wa kuachana hakuna kurudi nyuma

yaani un-aerase kila kitu
mpaka namba yake ya simu naifuta
 
Picha ni taswira inayobakia kutokana na muonekano wa mtu kutokana na tukio na kipindi maalumu.
Kuzitupilia mbalini, au kuzihifadhi kutatokana na utashi wa mtu. Kwangu mie binafsi sioni hasara kuhifadhi
kumbukumbu ya matukio ya awali, kwani nishajikubalisha ya kale hayanuki.
 
mi nilizichana,nikazichoma moto,majivu nikayafunga kwenye kitambaa kichafu,nikatupa porini!

Mhhhhhhhhhhhhhh! Hebu fafanua unamaanisha nini na 'kitambaa kichafu'! Isije ikawa ndo kama umemlaani na kumfanya awe mtoto si 'rizki'.
 
Picha ni taswira inayobakia kutokana na muonekano wa mtu kutokana na tukio na kipindi maalumu.
Kuzitupilia mbalini, au kuzihifadhi kutatokana na utashi wa mtu. Kwangu mie binafsi sioni hasara kuhifadhi
kumbukumbu ya matukio ya awali, kwani nishajikubalisha ya kale hayanuki.

Hiyo ni zaidi ya busara ndugu.
 
Picha ni taswira inayobakia kutokana na muonekano wa mtu kutokana na tukio na kipindi maalumu.
Kuzitupilia mbalini, au kuzihifadhi kutatokana na utashi wa mtu. Kwangu mie binafsi sioni hasara kuhifadhi
kumbukumbu ya matukio ya awali, kwani nishajikubalisha ya kale hayanuki.

Mfano una hifadhi picha video ya mzazi wako wkt wanamzika hivi kweli utakuwa na ujasiri wa kuangalia? wapi na ni lini?
 
Lini umekua? Si tumekucheza juzi tu wewe.

Imagine mtu umeishi naye mfano 10 years, mna watoto, do u think its easy?

Julie kwani hivyo vitu ndivyo vinavyoita "baby come back" ??Unaweza ukachoma kila kitu na bado ukashawishika kurudi kama unashawishika kirahisi.
 
Back
Top Bottom