Picha: Zito na genge lake wanatumika kuyahujumu maono ya mwl Nyerere

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Sep 9, 2020
6,900
12,347
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika hapo chini.

Nchini kwetu kuna vyama vingi vya siasa. Na kila chama kina lengo na nia ya kushika madaraka na kutuongoza kupitia sera za chama husika.

Ingawa kila chama kina sera zake na maono yake, lakini ukiangalia kwa makini utakuta vyama vyote vina sera zenye lengo la kuijenga Tanzania yenye umoja, upendo, mshikamano, elimu bora, maendeleo ya watu na vitu nk, na hilo ndio huwa lengo kuu la uanzishwaji wa vyama au chama husika.

Sasa inashangaza leo hii kuna chama kinakuja na sera za kuigawa Tanzania na watanzania kwa ujumla. Chama hicho kimekuwa kikienda tofauti mno na misingi ya uanzishwaji wake kwa kuja na sera za kupinga Muungano wetu ambao ulikuwa ni maono ya viongozi wawili wa nchi zetu mbili baba wa taifa mwl J. K. Nyerere na mzee Abeid . A . Karume.

Wazee hao kabla ya kuungana bila shaka walikaa chini wakajadiliana kuhusu faida na hasara za muungano huo, ambapo bila shaka baadae walikaa wakagundua kuwa muungano wao utakuwa na faida nyingi kuliko hasara.

Sasa inashangaza leo hii kuna kundi lililokuwa linafaidika na utawala wa sultani, linatengeneza magenge ya kupinga muungano ili utakapovunjika waweze kuiteka tena Zanzibar na kuangukia katika mikono yao kama zamani.

Walianza kwa kulalamika kuwa tunawaonea, baada ya kuwapa kila walichokitaka, sasa leo hii wanakuja na visingizio vya kutaka mamlaka kamili.

Sipingi wao kupewa kisiwa chao ambacho kwa namna kubwa sisi wabara ndio tunaopata hasara kwa kuwabeba na kuwasaidia mengi ikiwemo kuwapa ardhi bure huku kwetu, sema sasa ni kwanini watumie njia hiyo ya kudai nchi yao kupitia chama kilichoanzishwa na mtu anaejiita msomi kutoka bara. Je lengo kuu la kuanzishwa ACT Wazalendo ilikuwa ni kuja kutumiwa na hawa wazanzibar uchwara? au imetokea tu baada ya kuhamia chama hicho na kukuta uongozi wa chama hicho chini ya Zito ni dhaifu, hivyo wakaona hapo ndio pazuri wao kupenyezea ajenda zao huku ndugu Zito ambae ndio kiongozi mkuu wa chama akiangalia tu bila kuonya swala hilo?
 

Attachments

  • Screenshot_20230528-122834.jpg
    Screenshot_20230528-122834.jpg
    59.8 KB · Views: 4
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika hapo chini.

Nchini kwetu kuna vyama vingi vya siasa. Na kila chama kina lengo na nia ya kushika madaraka na kutuongoza kupitia sera za chama husika.

Ingawa kila chama kina sera zake na maono yake, lakini ukiangalia kwa makini utakuta vyama vyote vina sera zenye lengo la kuijenga Tanzania yenye umoja, upendo, mshikamano, elimu bora, maendeleo ya watu na vitu nk, na hilo ndio huwa lengo kuu la uanzishwaji wa vyama au chama husika.

Sasa inashangaza leo hii kuna chama kinakuja na sera za kuigawa Tanzania na watanzania kwa ujumla. Chama hicho kimekuwa kikienda tofauti mno na misingi ya uanzishwaji wake kwa kuja na sera za kupinga Muungano wetu ambao ulikuwa ni maono ya viongozi wawili wa nchi zetu mbili baba wa taifa mwl J. K. Nyerere na mzee Abeid . A . Karume.

Wazee hao kabla ya kuungana bila shaka walikaa chini wakajadiliana kuhusu faida na hasara za muungano huo, ambapo bila shaka baadae walikaa wakagundua kuwa muungano wao utakuwa na faida nyingi kuliko hasara.

Sasa inashangaza leo hii kuna kundi lililokuwa linafaidika na utawala wa sultani, linatengeneza magenge ya kupinga muungano ili utakapovunjika waweze kuiteka tena Zanzibar na kuangukia katika mikono yao kama zamani.

Walianza kwa kulalamika kuwa tunawaonea, baada ya kuwapa kila walichokitaka, sasa leo hii wanakuja na visingizio vya kutaka mamlaka kamili.

Sipingi wao kupewa kisiwa chao ambacho kwa namna kubwa sisi wabara ndio tunaopata hasara kwa kuwabeba na kuwasaidia mengi ikiwemo kuwapa ardhi bure huku kwetu, sema sasa ni kwanini watumie njia hiyo ya kudai nchi yao kupitia chama kilichoanzishwa na mtu anaejiita msomi kutoka bara. Je lengo kuu la kuanzishwa ACT Wazalendo ilikuwa ni kuja kutumiwa na hawa wazanzibar uchwara? au imetokea tu baada ya kuhamia chama hicho na kukuta uongozi wa chama hicho chini ya Zito ni dhaifu, hivyo wakaona hapo ndio pazuri wao kupenyezea ajenda zao huku ndugu Zito ambae ndio kiongozi mkuu wa chama akiangalia tu bila kuonya swala hilo?
Juliasi alikuwa na maono gani ktk Muungano.. Umeandika upuuzi tu wa jutoheshimu mawazo ya wananchi.

Mnaambiwa muuvunje su muuboreshe, we unashupaa na Maono.
 
Umeshamfanya Nyerere kuwa Mungu?
Kama watu hasa wazanzibari hawautaki huo Muuungano kwani lazima??..

Mnataka katiba mpya na Demokrasia na bado hamtaki kusikia mawazo msiyoyapenda??

Mkisikia Rais kafuta deni la umeme Zanzibar mnakereka ...ila mkisikia wazanzibari hawautaki Muuungano mnakereka pia ..mnataka nini??
 
Juliasi alikuwa na maono gani ktk Muungano.. Umeandika upuuzi tu wa jutoheshimu mawazo ya wananchi.

Mnaambiwa muuvunje su muuboreshe, we unashupaa na Maono.
Sijakataa muungano kuvunjwa, ila ninachoshangaa ni kuona chama cha siasa ambacho kimeundwa kwa kufuata misingi na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndo kinatumika katika swala hilo la Zanzibar.

Kwanini wasiunde chama chao wenyewe Zanzibar ambacho kitakuwa kinapigania masilahi yao ikiwemo hili swala la kutaka Zanzibar ijitenge?
 
Zitto alishakula cake yake, hana ushawish huo..
Na Zanzibar haitokaa iwe nchi huru, kwa gharama zozote...
Ondoa hofu Tanzania ipo salama.. chini ya chama chochote cha siasa
Kidogo kidogo humaliza gogo 🤣🤣🤣
 
Umeshamfanya Nyerere kuwa Mungu?
Kama watu hasa wazanzibari hawautaki huo Muuungano kwani lazima??..

Mnataka katiba mpya na Demokrasia na bado hamtaki kusikia mawazo msiyoyapenda??

Mkisikia Rais kafuta deni la umeme Zanzibar mnakereka ...ila mkisikia wazanzibari hawautaki Muuungano mnakereka pia ..mnataka nini??
Waanzishe chama chao ambacho hakifungamani na muungano wetu.
 
ACT ni Zanzibar ,Wazanzibar wanataka serikali tatu ,Usimlishe Zitto maneno ,wazanzibar ndiyo wanataka serikali tatu toka enzi za muasisi wao Maalim Seif.

Zanzibar mdogomdogo itajitenga yenyewe ,washaanza kujenga Power Plant yao!
Sasa kwa nini Zito aongoze chama kinachopigania masilahi ya wazanzibar tu, badala ya kupigania masilahi ya taifa lote la Tanzania?
 
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika hapo chini.

Nchini kwetu kuna vyama vingi vya siasa. Na kila chama kina lengo na nia ya kushika madaraka na kutuongoza kupitia sera za chama husika.

Ingawa kila chama kina sera zake na maono yake, lakini ukiangalia kwa makini utakuta vyama vyote vina sera zenye lengo la kuijenga Tanzania yenye umoja, upendo, mshikamano, elimu bora, maendeleo ya watu na vitu nk, na hilo ndio huwa lengo kuu la uanzishwaji wa vyama au chama husika.

Sasa inashangaza leo hii kuna chama kinakuja na sera za kuigawa Tanzania na watanzania kwa ujumla. Chama hicho kimekuwa kikienda tofauti mno na misingi ya uanzishwaji wake kwa kuja na sera za kupinga Muungano wetu ambao ulikuwa ni maono ya viongozi wawili wa nchi zetu mbili baba wa taifa mwl J. K. Nyerere na mzee Abeid . A . Karume.

Wazee hao kabla ya kuungana bila shaka walikaa chini wakajadiliana kuhusu faida na hasara za muungano huo, ambapo bila shaka baadae walikaa wakagundua kuwa muungano wao utakuwa na faida nyingi kuliko hasara.

Sasa inashangaza leo hii kuna kundi lililokuwa linafaidika na utawala wa sultani, linatengeneza magenge ya kupinga muungano ili utakapovunjika waweze kuiteka tena Zanzibar na kuangukia katika mikono yao kama zamani.

Walianza kwa kulalamika kuwa tunawaonea, baada ya kuwapa kila walichokitaka, sasa leo hii wanakuja na visingizio vya kutaka mamlaka kamili.

Sipingi wao kupewa kisiwa chao ambacho kwa namna kubwa sisi wabara ndio tunaopata hasara kwa kuwabeba na kuwasaidia mengi ikiwemo kuwapa ardhi bure huku kwetu, sema sasa ni kwanini watumie njia hiyo ya kudai nchi yao kupitia chama kilichoanzishwa na mtu anaejiita msomi kutoka bara. Je lengo kuu la kuanzishwa ACT Wazalendo ilikuwa ni kuja kutumiwa na hawa wazanzibar uchwara? au imetokea tu baada ya kuhamia chama hicho na kukuta uongozi wa chama hicho chini ya Zito ni dhaifu, hivyo wakaona hapo ndio pazuri wao kupenyezea ajenda zao huku ndugu Zito ambae ndio kiongozi mkuu wa chama akiangalia tu bila kuonya swala hilo?
Hakuna anaepinga Muungano ila wanakataa Aina ya Muungano!
Mf!: Muungano wa chakwangu Chetu wote ila chako ni chakwako!

Sent from my vivo Y67 using JamiiForums mobile app
 
Sijakataa muungano kuvunjwa, ila ninachoshangaa ni kuona chama cha siasa ambacho kimeundwa kwa kufuata misingi na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndo kinatumika katika swala hilo la Zanzibar.

Kwanini wasiunde chama chao wenyewe Zanzibar ambacho kitakuwa kinapigania masilahi yao ikiwemo hili swala la kutaka Zanzibar ijitenge?
Kwani Huelewi maana ya siasa!?
Ni kuchochea Fikra mpya vichwani mwa wananchi wakikuelewa kuiondoa Serikali iliyo madarakani na fikra Zane!

Sent from my vivo Y67 using JamiiForums mobile app
 
Watanganyika bana, kutwa munalalmika kuhusu muungano, Lakini wazanzibar wanapotaka kuuvunja Pia munalalamika hamtaki !
 
Back
Top Bottom