Sijawahi kuona VX za police zinakwenda kupambana na magaidi na sijawahi ona Gaidi wapo kwenye maandalizi ya kukusanya silaha na nguvu kazi watu eti wakiwa wanamtangazia adui ambae ni serikali tena kwenye media eti tupo tunakusanya nguvu tufanye ugaidi hii ni kali kweli,Osama hakutangaza maandalizi ya september 11 alipiga ndio akasema yeye kapiga.
Kwa kuongezea tu mkuu, hakuna kikundi chchote TZ kinaweza kujitangazia uasi sehemu kama Tanga maana hakiwezi kusurvive kabisa, walau kingeanzia mpanda na Tabora. Hebu fikiria hata Al shabab wameshindwa kujitangazia himaya Kenya kiasi kwamba wanaishia kuvizia na kurudi mafichoni Somalia, hivi inawezekanaje wahuni wawili watatu ambao hawajui hata logistics za vita tuambiwe wamepigana na JWTZ masaa 48?
Kabla ya Al shabab kuibuka kulikuwa na instability somalia kwa zaidi ya miaka 20, Boko haram imeibuka kutokana na factors ambazo zimekuwepo Nigeria kwa zaidi ya miaka 40, hayo matatizo ndio yaliyosababisha iibuke mwaka 2007 na bado wamekuja kupata nguvu zaidi baada ya Libya kusambaratika maana sasa waliweza kupata silaha kirahisi, na waliweza kuibuka kwasababu hata mazingira yanasupport kama DRC vile, mpaka wa Nigeria, chad, niger na Cameroon ni very isolated areas. Kwahiyo hakuna kikundi kilichodhamiria kufanya ugaidi kinaweza kikaenda kuweka base ya kudumu Tanga.
Sasa utashangaa kwanini polisi wanashindwa kuwashika wale vijana walioupload clip? maana hawa polisi waliweza kuchora picha ya mtu aliyetuhumiwa kushiriki mauaji ya padre zanzibar kwa kusikiliza maelezo ya shuhuda, iweje washindwe kujua identity ya mtu ambaye anaonekana na sauti inasikika? Na polisi wanawezaje kushindwa kutrack mahali hiyo clip ilikuwa uploaded wakati hata TCRA hicho kitu sio shida kwao?
Halafu wakati wote kwenye matukio huwa majeruhi wanatajwa na waandishi huwa wanaruhusiwa hata kuwapiga picha, kwenye hili tukio eti hawataki waandishi wawaone wala kuwapiga picha. Iweje wanajeshi huko DRC tujue kila kitu juu ya waliokufa halafu aliyekufa hapo Tanga anazikwa kimyakimya?
Hiyo ni movie tu kama movie zingine zinavyotolewa kila uchaguzi unapokaribia.