Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 988
Kama hutaweza kuona vizuri picha hizi ni kwamba zimepigwa mara mbili. Moja ni Benjamin Mkapa akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Josephat Kiboko Nyerere, huku pembeni yake akiwepo Anne Mkapa, Maria Nyerere na Chief Japhet Wanzagi.
Nyuma ya Mkapa ni Vincent Nyerere huyu mbunge wa CHADEMA lakini wakati huo yaani December 19, 2007 hajawa mbunge. Utaona picha ya Vincent imezungushiwa duara ili kumuonyesha vizuri.
Hapo ni nyumbani kwa marehemu yaani kwao na Vincent Nyerere.
Picha ya chini ni kwenye misa ya mazishi katika Kanisa Katoliki, parokia ya Butiama. Mnamuona Benjamin Mkapa amekaa kiti cha mbele kanisani akiwa ameshika kitabu akifuatilia misa. Hapa vilevile nyuma ya Mkapa ni Vincent Nyerere.
Kazi kwenu wana JF, the place we dare talk, the place we dare expose the unexposed!
Source:
JAMHURI,
ISSN-1821-8156, No. 17
March 27, 2012