Hawa polisi wetu ni bure kabisa, tena legelege na goigoi wa hali ya juu, Wanatuonyesha mikwara ya miwani nyeusi na silaha walizovaa, lakini ukivamiwa na majambazi usiku waite uone kama watathubutu kuja. Hawa hawana maana ya kuwa nao, ni heri kuwa na mbwa aliye hai kuliko kuwa na simba aliyekufa.