Watu unawajali kwenye misiba? kwanini usijali haki yao ya kuchagua viongozi badala yake mnawaibia watu kura!, kwanini usiwajali wanapotaka utaratibu unaofaa wa kuandaa katiba mpya badala yake unakumbatia kila kitu ili uchakachue vizuri. Tuache ushabiki kikwete anafaa kuwa kwenye vitengo vya socialization lakini sio kwenye majukumu mazito kama urais ndo maana anasema hajui kwanini wananchi ni maskini. Kawalinda mafisadi kupita kiwango halafu mnasema anajali watu. watu gani? raia au mafisadi wachache waliomuweka kwenye system?