Picha: Mwanamke aliyedaiwa kubakwa,hadi kufa alivyozikwa na manispaa morogoro

JAFE

Senior Member
Sep 1, 2012
191
42










Mrembo huyo akishushwa kwenye lori la Manispaa



Mrembo huyo akipelekwa eneo la makaburi ya Manispaa
Mwili wa Mrembo huyo akiingizwa kwenye kishimo hicho chembamba

marmbo huyo akitumbukizwa kwa shida kwenye kishimo chembamba,mbali na mrembo huyo kuwa na mwili mkubwa lakini pia baada ya kukaa kwa muda mrefu kwenye majokovu wa Mochwari mwili wake ulizimba sana.

Wafanyakazi wa manispaa kitengo la makaburi,wakimfukia mrembo huyo kwenye makabuli ya manispaa leo asubuhi.

LICHA ya kuhifandhiwa kwenye majokofu ya chumba cha kuhifadhia maiti cha hospital ya rufaa ya mkoa wa Morogoro kwa siku 20 akisubiri kutambuliwa na ndugu zake,mwanamke huyo aliyedaiwa kubakwa hadi kufa machi 1 mwaka huu eneo la Nane Nane mkoani hapa amezikwa leo na manispaa ya morogoro baada ya kutombambiliwa na ndugu zake.

Shukrani za pekee ziwafikie wafanyakzi wote wa kuchmba cha kuhifadhia maiti'Mochwari' kwa kukubali ombi la mwandishi wa habari hizi aliyeomba mrembo huyo aongezewe siku za kuhifahdia hapo tukitegemea huenda ndugu zake wangejitokea,kwa kawaida sheria za hospital ya ya mkoa wa Morogoro,marehemu anatakiwa kuhifadhia kwenye chumba hicho kwa majuma mawili[siku 14] ambapo baada ya hapo wanaukabidhi mwili uzikwe na manispaa,wafanyazi hao wa Mochwari walikubali ombi la mwandishi wa Mtandao huu na kuuhifadhi mwili huo hadi leo Machi 20,ikumbukwe mwili huo ulifikishwa kwenye chumbachi hicho machi 1 mwaka huu.

Majira ya saa moja na nusu asubuhi ya leo mwandishi wetu alipokea taarifa za uwepo la lori la Manispaa kwenye chumba hicho cha kuhifadhia maiti bila kuchelewa paparazi wetu alifika fasta na kushuhudia mwili wa maremo huyo uliokuwa ukitoa harufu kali ukitolewa kwenye majokofu ya Mochwari na kupakiwa kwenye Lori la manispaa.

Mtandao huu kwa kutumia usafiri wa pikipiki uliongozana na lori hilo hadi kwenye makaburi la Manispaa yaliopo eneo la Kolla na kushuhudia mrembo huyo akifukiwa bila kusaliwa.

Mbali na kushiriki mazishi hayo kwa kushika kole mwandisghi wetu pia alimsalia mrembo huyo sala ya dini zote mbili sambamba na kuweka alama kaburi hilo ambapo kama ndugu zake watajitokeza wakati wowote mwandishi wa mtandao huu atawaonyesha kaburi hilo ambalo alama iiyowekwa haiwezi kutoweka kwa kipindi cha miezi mitatu,hivyo mtu yoyote atakaye mtambu mrembo huyo kwa picha awasiliane na Mtandao huu kwa lengo la kuonyehswa kaburi na mepndwa wetu huyo aliyeuwawa kikatili na watu wasiojulikana.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro ACP Faustene Shilogile Mwili wa Mrembo huyo ambaye jina lake halikupatikana mara moja ulikutwa kwenye mashmba ya mkonge njia panda ya kueleka Tungi huku sehemu za siri zikiwa wazi na kwamba alipopekuliwa polisi walikuta tiketi ya basi iliyoonyesha mrembo huyo February 28 alipanda basi hilo akitokea Dar es salaam kuja mkoani hapa. na kwamba Mach 1 mwili wake uliokotwa kwenye mashamba hayo ya mkonge.
 
Daaaaaaaahhhhhh so sad aisee,
muwe mnatoka home mmeaga jamani maana siamini kama kuna mtu at that age akawa hana ndugu jamaa wala rafiki wa kumtafuta hasa anapoondoka mwa zaidi ya siku tatu nne
 
Du yaani hawa manispaa basi wangekuwa wanajaribu hata kuzika kwa heshima kidogo, mh si watenge fungu la mazishi kwa raia wanaokufa na kuokotwa kama huyu. Kodi tunalipa za kutosha mh, kweli mtu ukifa, nimesikia uchungu sana naona kawekwa juu ya matakataka !
 
Dah, inasikitisha sana, lakini Mungu atawalipa hao waliotenda huu Unyama hata kama sio leo basi kesho ahera. Na hawa Manispaa yaani wanamfukia mtu katika kashimo kadogo tena kafupi kama hako hata hawajali kua Mbwa anaweza kuja kufukua!, R.I.P Dada.
 
RIP mdada mwenzetu.

ila inasikitisha sana, sidhan hata kama kuna kuoshwa kulikofanyika, mweeeh! kazikwa na janaba la kubakwa jamaniiiiii
kuna watu wameandikiwa vifo vibya jamanii.
 
Duh, binadamu tumekuwa wakatili kuliko wanyama nowadays. Damu ya binti huyu itawahunt popote walipo washenzy wote waliohusika kwa namna moja ama nyingine ktk utekelezaji wa unyama huu.
 
Manispaa ya morogoro na uongozi mzima inabidi watambue kuwa haita maiti anastahili heshima. Kweli manispaa imeshindwa kutoa ambulance na kuweka maiti hiyo na kwenda kuizika.

Kweli watanzania tumefikia unyama wa aina hii.

Hela ya chai na vitafunio kila siku ipo, hela za tafrija kila wiki zipo. Hela za masurufu na posho zipo. Mmeona ugumu gani kuondoa angalau posho zenu za siku mmoja na mumuhifadhi marehemu kwa heshima ya kibinadamu inayostahili???

Mmekosea sana. Uongozi wa manispaa ombeni radhi kwa watanzania kwa kitendo mlichofanya!!!!!
 
Jamani yaani hao manispaa wameshindwa hata kumwaga kwanza takataka kabla ya kubeba mwili? Kwa kweli inasikitisha. Apumzike kwa amani mdada wa watu. Wabakaji na walipwe wanavyostahili.

hapo wanaposema mwili ulikuwa ukitoa harufu kali ndio sijapaelewa, mie najua wakiwekwa humu huwa wanachomwa masindano kuzuia mwili kuharibika au kwa mrembo ilikuwaje? maisha haya jamani, mweh
 
Pole kwa ndugu na jamaa waliopoteza mpendwa wao.Tuko kwenye nyakati za giza na watu wasipobadili mienendo mauti inawasubiri na tena inawatamani
 
Mungu aendelee kuwapa moyo huo huo watu wote walioshiriki kufanikisha kumpumzisha salama marehemu huyu aliyefanyiwa vibaya. Mungu aseme nao wote waliomfanyia vibaya huyu mdada wa watu sawasawa na uhusika wao.

RIP mdada wa watu.
 
Back
Top Bottom