Mwanajeshi mmoja ameamua kujitoa mhanga na yuko tayari kufukuzwa kwaajili ya CHADEMA maana amechoshwa na maisha magumu ya kwake binafsi na ndugu zake...
Lema, Nassari na mwanajeshi aliyeamua kusema yupo tayari kufukuzwa kwa ajili ya CDM LEO kwenye mkutano Mererani
Mkuu maisha ni magumu yaani wanajeshi wanatamani afadhali wawe wachimba msingi kuliko kutumikia jeshi..kuna polisi wengine ukiwaona hata mavazi yao utawahurumia...
Magwanda ya kijeshi yanauzwa kila uchochoro wa mitumba! sasa gwanda hilo halinishangazi maana tangu turuhusu mitumba sio shida tena kujipatia gwanda la jeshi!
Maisha yakiendelea kuwa magumu hivi mwaka 2015 CCM wakaleta uhuni kwenye matokeo watu hawatavumilia maana maisha yana wapiga wewe krismasi hii baba yako huko kijijini anakuomba umtumia hata 5000 huna ukipiga mahesabu january ndiyo hiyo inakuja ada za shule...kwanini usijilipue halafu mpumbavu kama Nape anasema kadi ya dr slaa ndiyo hoja ya nchi nzima...
Magwanda ya kijeshi yanauzwa kila uchochoro wa mitumba! sasa gwanda hilo halinishangazi maana tangu turuhusu mitumba sio shida tena kujipatia gwanda la jeshi!
Mtu aliyejitambulisha kuwa askari wa Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ),kambi ya Monduli,Arusha akiwa na wabunge wa Chadema,Godbless Lema (Arusha Mjini) na Joshua Nassari (Arumeru Mashariki) baada ya kumalizika kwa mkutano wa hadhara uliohutubiwa na wabunge hao katika Mji mdogo Mererani,Simanjiro mkoani Manyara jana.
Mtajipambambanua kwa njia nyingi lakini sawa na mwanaume asiye na kizazi ... Bado mtanunua hadi nguo za mgambo wa jiji,za manesi na madr alafu mpige nao picha.... Hata kwa macho tu mtoto mdogo anajua huyo kibaka tu kaokotwa mtaani kavalishwa nguo .