Picha:Hii ndio Mbeya Airport

Ngalikivembu

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
1,959
872
Sijawahi kuona uwanja wa Ndege mbaya na wenye hatari kubwa kwa maisha ya watumiaji wa viwanja vya ndege kama huu wa Mbeya uliopo katikati ya mji wa Mbeya.Nilistaajabia sana kuona mji mkubwa kama Mbeya bado ulikosa uwanja wa Ndege wenye hadhi kama huu.Kwa hakika uwanja wa ndege wa Songwe unapaswa uishe haraka sana na tena nasema serikali ilichelewa sana kujenga uwanja mwingine.Leo ninaposikia kuna ajali ya ndege katika uwanja huu sishangai tena.

Kwanza uwanja huu wananchi wanakatiza tu katikati ya uwanja kwa shughuli zao binafsi.Waendesha pikpiki wanapita hapo, magari yanakatiza tu kiholela, watu pia usiseme.Kutokana na uwanja huu kuwa katikati ya makazi ya watu imekuwa ni kawaida tu sasa hata kukaa na kupiga stori na wahusika wasichukue hatua zozote zile.

Barabara ya kurukia ndege ni hovyo na wala huwezi kuita ni runway.Mashimo ni mengi sana.Hapa ina maana ndege ikikosea ikaacha njia basi itaenda kupiga break kwenye makazi ya watu jambo ambalo ni la hatari. Wenyeji wanasema kama kuna ndege inataka kutua au kuruka basi itapigwa filimbi kuashiria kuna ndege hivyo watu watawanyike.Hii ni hatari mno,sijui kwa nini Mamlaka ya Anga Tanzania haiufungi uwanja huu.Tazama picha mbalimbali za uwanja huo.Kuna picha zingine hazijawa clear sana.
 

Attachments

  • AIRPORT MBEYA1.JPG
    AIRPORT MBEYA1.JPG
    82.4 KB · Views: 373
  • AIRPORT MBEYA2.JPG
    AIRPORT MBEYA2.JPG
    1.8 KB · Views: 1,551
  • AIRPORT MBEYA3.JPG
    AIRPORT MBEYA3.JPG
    95.8 KB · Views: 316
  • AIRPORT MBEYA4.JPG
    AIRPORT MBEYA4.JPG
    100.7 KB · Views: 399
  • AIRPORT MBEYA5.JPG
    AIRPORT MBEYA5.JPG
    80.9 KB · Views: 247
Ukipita kuanzia saa 1.30 usiku watu wanapeana uroda hapo usipime!
 
Ukipita kuanzia saa 1.30 usiku watu wanapeana uroda hapo usipime!

Sasa ukiwa na mpenzi wako wa siku nyingi unachagua tena sehemu ya kulia uroda?tatizo ni kuanza utapelekwa hata usikotegemea kwa gharama kubwa ukome ukomae!!
 
Sijawahi kuona uwanja wa Ndege mbaya na wenye hatari kubwa kwa maisha ya watumiaji wa viwanja vya ndege kama huu wa Mbeya uliopo katikati ya mji wa Mbeya.Nilistaajabia sana kuona mji mkubwa kama Mbeya bado ulikosa uwanja wa Ndege wenye hadhi kama huu.Kwa hakika uwanja wa ndege wa Songwe unapaswa uishe haraka sana na tena nasema serikali ilichelewa sana kujenga uwanja mwingine.Leo ninaposikia kuna ajali ya ndege katika uwanja huu sishangai tena.

Kwanza uwanja huu wananchi wanakatiza tu katikati ya uwanja kwa shughuli zao binafsi.Waendesha pikpiki wanapita hapo, magari yanakatiza tu kiholela, watu pia usiseme.Kutokana na uwanja huu kuwa katikati ya makazi ya watu imekuwa ni kawaida tu sasa hata kukaa na kupiga stori na wahusika wasichukue hatua zozote zile.

Barabara ya kurukia ndege ni hovyo na wala huwezi kuita ni runway.Mashimo ni mengi sana.Hapa ina maana ndege ikikosea ikaacha njia basi itaenda kupiga break kwenye makazi ya watu jambo ambalo ni la hatari. Wenyeji wanasema kama kuna ndege inataka kutua au kuruka basi itapigwa filimbi kuashiria kuna ndege hivyo watu watawanyike.Hii ni hatari mno,sijui kwa nini Mamlaka ya Anga Tanzania haiufungi uwanja huu.Tazama picha mbalimbali za uwanja huo.Kuna picha zingine hazijawa clear sana.

UMESAHAU KUONGEZA neno INTERNATIONAL...
 
Sasa hiyo itaitwa Mbeya Airport ama Mbeya Airstrip, kuna utofauti kati ya airport na airstrip kama kulivo na utofauti kati ya Airway na Airline sisi ndo wataalam wa kada hiyo kwa taarifa yako
 
Sijawahi kuona uwanja wa Ndege mbaya na wenye hatari kubwa kwa maisha ya watumiaji wa viwanja vya ndege kama huu wa Mbeya uliopo katikati ya mji wa Mbeya.Nilistaajabia sana kuona mji mkubwa kama Mbeya bado ulikosa uwanja wa Ndege wenye hadhi kama huu.Kwa hakika uwanja wa ndege wa Songwe unapaswa uishe haraka sana na tena nasema serikali ilichelewa sana kujenga uwanja mwingine.Leo ninaposikia kuna ajali ya ndege katika uwanja huu sishangai tena.

Kwanza uwanja huu wananchi wanakatiza tu katikati ya uwanja kwa shughuli zao binafsi.Waendesha pikpiki wanapita hapo, magari yanakatiza tu kiholela, watu pia usiseme.Kutokana na uwanja huu kuwa katikati ya makazi ya watu imekuwa ni kawaida tu sasa hata kukaa na kupiga stori na wahusika wasichukue hatua zozote zile.

Barabara ya kurukia ndege ni hovyo na wala huwezi kuita ni runway.Mashimo ni mengi sana.Hapa ina maana ndege ikikosea ikaacha njia basi itaenda kupiga break kwenye makazi ya watu jambo ambalo ni la hatari. Wenyeji wanasema kama kuna ndege inataka kutua au kuruka basi itapigwa filimbi kuashiria kuna ndege hivyo watu watawanyike.Hii ni hatari mno,sijui kwa nini Mamlaka ya Anga Tanzania haiufungi uwanja huu.Tazama picha mbalimbali za uwanja huo.Kuna picha zingine hazijawa clear sana.
Mkuu umeibiwa, hapo ni Airstrip ya toka enzi ya mkoloni.

Mambo yako Songwe International Airport, kama kilometa 20 toka hapo.
 
Sijawahi kuona uwanja wa Ndege mbaya na wenye hatari kubwa kwa maisha ya watumiaji wa viwanja vya ndege kama huu wa Mbeya uliopo katikati ya mji wa Mbeya.Nilistaajabia sana kuona mji mkubwa kama Mbeya bado ulikosa uwanja wa Ndege wenye hadhi kama huu.Kwa hakika uwanja wa ndege wa Songwe unapaswa uishe haraka sana na tena nasema serikali ilichelewa sana kujenga uwanja mwingine.Leo ninaposikia kuna ajali ya ndege katika uwanja huu sishangai tena.

Kwanza uwanja huu wananchi wanakatiza tu katikati ya uwanja kwa shughuli zao binafsi.Waendesha pikpiki wanapita hapo, magari yanakatiza tu kiholela, watu pia usiseme.Kutokana na uwanja huu kuwa katikati ya makazi ya watu imekuwa ni kawaida tu sasa hata kukaa na kupiga stori na wahusika wasichukue hatua zozote zile.

Barabara ya kurukia ndege ni hovyo na wala huwezi kuita ni runway.Mashimo ni mengi sana.Hapa ina maana ndege ikikosea ikaacha njia basi itaenda kupiga break kwenye makazi ya watu jambo ambalo ni la hatari. Wenyeji wanasema kama kuna ndege inataka kutua au kuruka basi itapigwa filimbi kuashiria kuna ndege hivyo watu watawanyike.Hii ni hatari mno,sijui kwa nini Mamlaka ya Anga Tanzania haiufungi uwanja huu.Tazama picha mbalimbali za uwanja huo.Kuna picha zingine hazijawa clear sana.

hivi kumbe mbeya ni jiji na hiyo ndio airport yao sio??
 
Mkuu umeibiwa, hapo ni Airstrip ya toka enzi ya mkoloni.

Mambo yako Songwe International Airport, kama kilometa 20 toka hapo.

Tunaomba picha za Songwe Intl kwa walionazo tafadhali, isije ikawa ndio Uwanja wa kufikirika wa kimataifa wa Songwe.
 
Tunaomba picha za Songwe Intl kwa walionazo tafadhali, isije ikawa ndio Uwanja wa kufikirika wa kimataifa wa Songwe.
58.jpg

Songwe-International-Airport.jpg






The construction of the passengers' lounge was underway and it was expected to be completed by the end of the year. Songwe airport is expected to be among the best airports in the country upon its completion and is said to be bigger that Mwalimu Julius Nyerere international airport in Dar es Salaam. Songwe's runway is 3.5 km long while Mwalimu Julius Nyerere's is only 3.0 Km. Source ippmedia.

e.
Songwe Int Airport under construction.
 
Ngalikivembu naamini huujui uwanja unaojengwa. Huo ni uwanja wa zamani, ambapo kila mji una wake. Sasa umewalisha watu sumu.
 
Last edited by a moderator:
nilikuwa singida jana nakufa mbavu zangu, sikujua kile ni choo cha walinzi au ofice ya wafanyakazi wa hicho kiwanja! sasa hii mpyaaaaa! lol
 
nilikuwa singida jana nakufa mbavu zangu, sikujua kile ni choo cha walinzi au ofice ya wafanyakazi wa hicho kiwanja! sasa hii mpyaaaaa! lol

Usishangae, airstrips nyingi za Tanzania ndivyo zilivyo.
 
Usishangae, airstrips nyingi za Tanzania ndivyo zilivyo.

Mkuu si watu wengi wenye ufahamu wa tofuti kati ya airstrips,airports na International airports.
Watu kwa vile ufahamu ni mdogo wanafikiri ndege lazima itue kwenye tarmaced landing area.

Mbaya zaidi si wengi wanaojua hata tofauti kati ya propelled aircrafts, turbo-propelled aircrafts na jet aircrafs.
Aina ya uwanja ndio inayoweza kudetermine aina ndege inayoweza kutua kiwanjani hapo.
 
Mkuu si watu wengi wenye ufahamu wa tofuti kati ya airstrips,airports na International airports.
Watu kwa vile ufahamu ni mdogo wanafikiri ndege lazima itue kwenye tarmaced landing area.

Mbaya zaidi si wengi wanaojua hata tofauti kati ya propelled aircrafts, turbo-propelled aircrafts na jet aircrafs.
Aina ya uwanja ndio inayoweza kudetermine aina ndege inayoweza kutua kiwanjani hapo.

Uko sahihi kabisa.
Kuna mkanganyiko mkubwa kutofautisha hivyo viwanja vya ndege na ndege zenyewe.
Labda nikuombe uanzishe thread yenye kuchanganua zaidi mambo hayo, naahidi nitachangia mawazo kwa kadri ninavyoelewa. Labda kwa ufupi, kama ulivyosema, ndege zenye Jet Engine haziwezi kutua viwanja vya vumbi (ambavyo ni vingi Tanzania), badala yake ndege zinazotumia turbo propelled engines (pangaboi) kama zilivyo ATR za Precision ndizo hutua kwenye viwanja vya vumbi. Ukubwa wa uwanja pia huamua ukubwa wa ndege ya kutua katika uwanja husika.
 
Wote mnaosema kwamba mtoa mada hajui anachoongea hebu rudini tena msome mada yake kwa umakini. Iwe ni AIRSTRIP au AIRPORT au chochote kile mradi tu kinahusika na kutua na kuruka ndege basi hakipaswi kuwa ktk mazingira hayo, kwamba uwanja uko ktk mazingira hatarishi kwa wakazi wa hapo na abiria pia. Watu wanakatiza tu katikati ya uwanja, magari ng'ombe n.k. hata hizo runway zenyewe zina mashimo balaa, je ndege ikikwama au ikakwepa shimo na kupitiliza kwenye makazi ya watu ni sawa? Tufikiri mara mbili kabla ya kushambulia, hata yeye ameweka wazi kwamba serikali imechelewa kuanza kujenga uwanja mpya hadi huu ukafikia hali hii. Uwanja mpya uendelee kujengwa ila hata huu wa zamani uwe ktk hali salama pia, hata kama hauna lami basi ndio kuwe na mashimo? Zinatua ndege ndogo lakini nazo zinahitaji usalama, hivi ukiwa unajenga nyumba mpya unaacha hiyo ya zamani ambayo bado unaishi iendele kuvuja, milango ing'oke, bati lidondoke ati kwasababu unajenga mpya utahamia? Tukubali ukweli uwanja umechakaa sana, hauna uzio hivyo ndio malisho ya mifugo na shortcut ya magari na watu kwenda makwao! hadi ajali itokee ndio tuanze kulaumu serikali?
 
Back
Top Bottom