Napata shida kuweza kutambua adhma ya walioko kwenye dola dhidi ya wananchi wanao ongozwa.
Katika hali tulionayo hivi sasa ya matukio ya kutisha, naona haja ya dola kuboresha na kuimarisha mahusiano na wananchi wake ili kuweza kupambana vyema na matukio ya sasa. Ila cha kushangaza inaonekana kuna vitu vinafanyika kwa lengo l kukomoa wengine bila kujua kuwa yanatengeneza chuki baina ya pande mbili.
Nini mantiki ya haya ya ziada ikiwa mtu amekili kosa na taratibu za kisheria zipo?
Mbona serikali inajidhalilisha yenyewe nila kutambua,maana hata wenzetu nchi Jirani wakiona wanajua kabisa nchi yetu haifuati utawala wa sheria,ndio maana wananchi wanaandika mabango ili kudai haki,