[PICHA] CHADEMA Ndani ya Shinyanga

Kikwete anajua kuwa nyuma yake hana watu. Hii inamfanya aweweseke daima.
 
CHADEMA unatufaa sana.''CHADEMA your the only Option we have''.Eee MUNGU muumba mbingu na nchi ,uliyetuumba watanzania tujitwale kwa upendo,amani na mshikamano ,utusaidiye kuwapata viongozi wanaokuheshimu wewe.AMEN
 
WanaJF.

CHADEMA inaendelea na Maandamano Kanda ya Ziwa na leo tuko Mkoa wa Shinyanga.Maandamano ndio yameanza na watu ni wengi mno.Barabara zimefunga msafara unaenda kwa taabu sana.Karibu Pikipiki na Tax zote za Mjini hapa zipo kwenye maandamano kuelekea Uwanja wa Lubaga. Hakika mambo ni moto.

Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke

Kutoka kwenye Maandamano Shinyanga

Regia E Mtema
Waziri Kivuli-Kazi na Ajira

IVI REGIA. UNAJUA THAMANI YA UTULIVU? CHADEMA MNACHOFANYA SI SAWA KWA MTANZANIA MWENYE NIA SAFI NA NCHI HII. MOTO MNAOUCHOCHEA UTAWAKA, ILA SIDHANI MKISHA UWASHA KAMA MTAWEZA KUUZIMA, WOTE MTAJUTA KWA NIA HIYO MNAYOTAKA KUTUMIA. SIKU ZOTE MUNGU ANAMULAANI MTU ANAYEAMSHA HISIA ZILIZOLALA. MSIWATUMIA WATANZANIA KAMA TOOL ITAWACOST
 
kikwete anajua kuwa nyuma yake hana watu. Hii inamfanya aweweseke daima.

hili ndilo liliwafanya chadema wadhani kuwa watashinda kumbe watu huenda pale kusikiliza kinachozungumzwa na si kwamba ni washabiki kama unavyodhani. Chadema hutumia masela kuwin mass. Siku zote thamani ya kitu huwezi kuijua mpaka kikutoke. Kama unaweza nenda rwanda ukawaulize maaskofu walichokichochea na nini ilikuwa hatima yake kisha waulize wanyarwanda kama wako tayari kurudia ujinga ule? Chadema kama wanaipenda nchi watulie tusubiri mchakato ujao
 
Ingawa sina hela na mshahara wa mkwere mpaka leo haujatoka na sijui nitukula nini kuona hizo picha nimefarijika.
keep it up
 
hakuna hata mwenye sare, ingekuwa wale wenzetu!!
ingekuwa rangi fulani inawakaaaaaa!! nguo zote mpyaaa!!
Lakini hawa watu na baiskeli zao, na nguo zao za kawaida, kweli wamekerwa!
 
Hiyo mioto huwa inazimika siku zote.

Ulizimika Sarayevo, itakuwa wa Tanzania ukiwaka? Tanzania siyo Somalia ili moto usizimike.

Kwani unaona sisi ni Wala mirungi hadi tusizimishe moto?

Ila kabla haujazima, Chenge, Lowassa, Kikwete, Mkapa, Mramba, Rostam Azziz, Manji, Makamba, Shimbo, Tendwa, ET EL... tutahakikisha kwanza wametunzwa maeneo wanayotakiwa kuwa na mali zao zimetaifishwa.

Tukishafanya hilo, na kubadili katiba, watu wataanza kufanya kazi kwenye nchi ya kawaida duniani.

Niliongea na Mwana CCM ambaye anakiri kabisa kuwa "Tanzania tumekuwa kama Minyama kwenye mbunga......"
IVI REGIA. UNAJUA THAMANI YA UTULIVU? CHADEMA MNACHOFANYA SI SAWA KWA MTANZANIA MWENYE NIA SAFI NA NCHI HII. MOTO MNAOUCHOCHEA UTAWAKA, ILA SIDHANI MKISHA UWASHA KAMA MTAWEZA KUUZIMA, WOTE MTAJUTA KWA NIA HIYO MNAYOTAKA KUTUMIA. SIKU ZOTE MUNGU ANAMULAANI MTU ANAYEAMSHA HISIA ZILIZOLALA. MSIWATUMIA WATANZANIA KAMA TOOL ITAWACOST
 
Back
Top Bottom