Mimi naomba Mhe. Mbowe aeleze vyema wananchi kuhusu mkanganyiko ulipo sasa kuhusu
- Kususia kura ya maoni ya katiba pendekezwa
- Kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura
UKAWA wametangaza msimamo wao wa kususia kura ya maoni ya katiba pendekezwa. Ingawa mimi sikubaliani na msimamo huo wa UKAWA, kwasababu haileti MANTIKI/LOGIC kususia kupiga kura ya maoni ya katiba pendekezwa. Halafu on the other hand UKAWA ikaingia kwenye uchaguzi mkuu kwa kutumia KATIBA WALIOISUSIA. This is ILLOGICAL, lakini hii ni topic ya siku nyingine.
Point ya leo ni NEC imetangaza kuanza kuandikisha Watanzania wenye sifa katika daftari la kudumu la wapiga kura. Kutokana na tangazo la Judge Damian Lubavu zoezi litaanzia mkoa wa Njombe.
Daftari hilo la wapiga kura ndilo litatumika kwenye kura ya maoni ya katiba pendekezwa na pia ndilo litatumika kwenye uchaguzi mkuu wa october 2015.
UKAWA baada ya kutangaza msimamo wao wa kususia kura ya maoni ya katiba pendekezwa, CCM wanatumia mwanya huo kupotosha wananchi hasa wa vijinini ambao wanaunga na kushabikia upinzani (UKAWA).
CCM wanapita wanawadanganya Watanzania ambao wanaonekana ni mashabiki wa vyama vya upinzani kwamba, uandikishwaji wa watu kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, ni kwaajili tu ya wale ambao wataipigia kura ya NDIYO katiba pendekezwa.
CCM wanaambia wananchi kwamba wale ambao ni wafuasi wa UKAWA hawana haja ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, kwasababu viongozi wa UKAWA wameshasema kwamba watasusia kura ya maoni ya katiba pendekezwa.
Propaganda hizi za CCM zinalenga kuwafanya Watanzania wengi ambao ni wafuasi wa UKAWA wasijiandikishe kwenye daftari la kudumu la wapiga kura wakifikiri kwamba ni kwaajili ya kura ya maoni ya katiba pendekezwa tu. Kumbe daftari hili ndilo pia litatumika kwenye uchaguzi mkuu.
Matokeo yake ni kwamba ni wana-CCM tu na mashabiki wao ndio watakaojiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, hivyo wana-CCM kuweza kushiriki kwanza kupiga kura ya maoni ya katiba pendekezwa na pia kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani
Katika suala ambalo vyama vya upinzani vimekuwa vikifanya vibaya, KWANZA ni katika kuhamasisha Watanzania wote wenye sifa kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura. PILI ni katika kuhamasisha Watanzania kujitokeza kupiga kura siku ya uchaguzi mkuu.
Wote tunafahamu kwamba low voters registration na low voters turn out uwa ni advatange kwa CCM. Kwasababu CCM inao wanachama na mashababiki wachache. Lakini wanachama na mashabiki wa CCM pamoja na uchache wake wako VERY RESPONSIBLE to their party.
Wana-CCM wanajiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, Wana-CCM lazima wajitokeze siku ya kupiga kura kukipigia chama chao CCM na wagombea wake.
Lakini vyama vya upinzani i.e UKAWA wana wafuasi wengi, but MOST THEM VERY IRRESPONSIBLE. Wanachama wengi wa UKAWA kwanza hawajiandikishi kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Pili hata wale wachache wanaojiandikisha kwenye daftari la wapiga kura, ni wachache wanaojitokeza siku ya kupiga kura.
Bila UKAWA kuyafanyia kazi hayo mambo mawili makuu basi wasahaku kabisa kushika dola. Anecdotal inaonyesha kwamba katika maeneo ambayo yamekuwa high turn out siku ya kupiga kura CCM imeangukia pua au imeshinda kwa margin ndogo sana. Lakini katika maeneo ambayo kumekuwa na low voters turn out CCM imepata ushindi wa KIMBUNGA (REF Uchaguzi mkuu 2010, uchaguzi serikali za mitaa 2014)
Hivyo suala kujiandikisha KUPIGA kura na KUJITOKEZA siku ya kupiga kura kama litafanyika kwa mafanikio makubwa 80% - 90% ndiyo KABURI la CCM. Kama UKAWA wanafikiri kwamba serikali ya CCM ipo siku itataka ione kwamba Watanzania wengi wanajiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Na pia CCM eti wapende kuone Watanzania wengi wanajitokeza kupiga kura, kama yupo kiongozi wa UKAWA anafikiri hivyo, basi UKAWA haijawa tayari kushika dola.
Mfano mdogo tu wa kujiliuza. Hivi ni kwanini NEC huwa inaandikisha wanafunzi wa vyuo vikuu na vyuo vingine, pamoja na wanafunzi wa sekondari kwenye daftari la kudumu la wapiga kura wakati vyuo na sekondari vikiwa VIMEFUNGULIWA. Lakini siku ya uchaguzi mkuu hufanyika wakati vyuo na sekondari vikiwa VIMEFUNGWA?!
Kila uchaguzi mkuu hali ni hiyo, unafikiri hiyo ni coincidence? It is by design and its puporse is to disefranchise younger voters
UKAWA the ball is in your court, mki-bugi step katika zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapinga kura YOU ARE FINISH