Kosa kubwa ulilolisema katika swali lako ni kuwa pi ilijulikanaje zama za kabla ya sayansi? Nitakupa mfano, uhandisi wa majengo uliotumiwa kujenga mapiramidi ya Misri ulikuwa ni wa hali ya juu sana. Mapiramidi yalijengwa kabla ya Musa kwa sababu Musa baadaye ndiye aliwaondoa Wana wa Israel katika utumwa uliowafanya kujenga mapiramidi hayo. Na Musa ndiye aliyeandika vitabu vitano vya Agano la Kale (Mwanzo, Kutoka, Walawi, Hesabu na Kumbukumbu ya Torati).
Mimi Biblia yangu inasema hivi: Wana wa Israel waliondoka Misri 1520 BC. Na Mfalme Suleman alitawala 970 BC.
Sasa nikuulize, hiyo sayansi unayoizungumzia ilianza lini? Kama unazungumzia mwanzo wa sayansi iwe pale Bwana wetu Yesu Kristo alipopeleka Fadhila zake nchi za Magharibi, basi unazungumzia maugunduzi ya Wanasayansi wa leo wakiwemo Mathematicians na Physicists uliowasoma darasani. Baada ya Mwanakondoo aliyechinjwa kutawazwa kama ilivyo katika Ufunuo wa Yohana Aya ya 4, Aya ya 5 na Aya ya 6 ndipo dunia ikajaliwa sayansi na teknologia ya magari, treni na ndege na kuifanya dunia kuwa ndogo sana.
Lakini sayansi hii ilikuwa ni mwendelezo wa maarifa ambayo yalikuwepo tangu zama za kabla ya kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Kulikuwa na refinements kulingana na mahitaji makubwa ya kuenezwa kwa neno kutoka Ulaya kwenda dunia yooote zaidi ya Israel. Kina Vasco daGama, kina Marcopolo, sema wewe na hao wengine.
Kwa hiyo pi ilikuwepo kabla ya Yesu Kristo.