Brother!
Hata waliyoikubali Quran na Mtume hawakuikubali kibubusa! Bali waliikubali Quran na mtume baada ya kufikiri kwa kina; aidha kwa hoja au kusikia kilichosemwa na Quran.
Tangu mababu zangu walisema haya masanamu ndiyo miungu. Muhammad anakuja na hoja zake anasema hawa si miungu bali kuna Mungu! Haya mambo yapoje!
Walitumia akili kwa usahihi si kwa mtindo wa logic. Logic ni fani pweke, ambayo msingi wake ni akili pekee, Sasa kwa uhalisia akili haiwezi kudiriki kila kitu. Hili jambo la kwanza. Sasa nitakuuliza hao maswahaba walitumia logic ? Kumbuka hapa tunaongelea logic kama fani na si kama matamko.
Sababu kila mtume alikuja baada ya kutanguliwa mitume wengine, ukirejea historia mitume utaona mitume wamekuja kujibu maswali ambayo akili imekoma. Walikuwa na nyenzo za kuwafanya watu waamini ikiwemo miujiza. Kingine kila mwanadamu ameumbwa na hali ya kumjua Allah yaani Fitrah.