tunalazimika
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 1,098
- 259
MWAKIBINGA KATIKA CHAMA KIPYA.
ANAYE UNGA MKONO KARIBU ANAYE PUUZA KWAKHERI.
Kama Mwakibinga nina maamuzi yangu na siendeshwi na hisia bali naendeshwa na dhamira yangu.
Nimepata marafiki wengi sihofu kuwapoteza kwa kusimamia ninacho kifia.
Nilijiunga na chadema mwaka 2009/01/23. Nikiwa kidato cha sita. Baada ya hapo niliendelea kuhakikisha chadema inaenea vyuo vikuu vya dodoma nilifanikiwa kueneza chadema lakini nimefukuzwa chuo zaidi ya mara mbili niliamini kwenye ukombozi na msimamo wa CHADEMA. Nimetumika sana sana katika chama hichi.
Nimekua afisa mafunzo Taifa.
Nimekua mwenyekiti chadema UDOM.
Nimekua Mjumbe wa kamati tendaji ya jimbo la lupa chunya chadema.
Nimekua mratibu wa vijana bavicha chadema chunya.
Nimekua mjumbe katika kamati ya ufundi ya chadema nyanda za juu kusini.
Nimetumikia idara ya usalama ya CHADEMA kazi maalumu chini ya Rwakatale sijui hata kama Mbowe anajua labda Dr slaa.
Pamoja na hayo yote nakumbuka nilichaguliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya chadema ni msingi kanada ya nyanda za juu kusini nikashinda Mbowe akasema nina hakili sana sifahi kuwa mwenyekiti ila niwe makamu nika kataa.
Niligombea bavicha taifa mbowe akaja usiku wa manane kumsafisha patrobas katambi wagombea wengine tuka hujumiwa.
Nimegombea ubunge chunya kila taarifa ilionesha uchaguzi haukuwa wa halali lakini amekatwa wa kwanza. Amepewa kasaka aliye ongoza jimbo kwa miaka 15 akashindwa 2005 akahamia chadema kabla hajazoea kahamia cuf kabla hajazoea kahamia ccm tena.
Nimejenga chunya kwa juhudi na mahalifa lakini siku ya siku analetwa KASAKA HATA KADI YA CHADEMA HANA.
Nimeitwa na viongozi wa chama nikaambiwa ni mwachie KASAKA lakini aliyeshika nafasi ya kwanza hajaitwa hata kuambiwa kama kumuheshimu tu MIRAJI HUSSEIN KAONEWA.
Huu ni udhalilishaji nimevumilia lakini leo mchana kata ya chokaa yaani nyumbani kabisa ambapo kuna makaburi ya babu na bibi mgombea aliye chukua nafasi ya kwanza kachukua na form karudisha lakini viongozi wa jimbo wame pora form ya mzee kabuje kwa mtendaji msimamizi wa uchaguzi mtendaji karipoti polisi lakini inaonekana agizo la kufukuzwa mzee kabuje limetoka juu yaani mkoa kanda na taifa.
Mbowe kauza jimbo letu kwa kasaka,
Kaamua na kuuza kata yetu No! Sitaki kuona chunya ina ujumiwa mimi chunya kwanza chama baadaye.
Nita hakikisha chunya ina kombolewa na nitapambana hadi nife siwezi kurudi nyuma
NINA MSIMAMO NA NIKO TAYARI KUUFIA. KAMA KUNA MTU YUPO TAYARI KUPOTEZA URAFIKI WANGU NAYE KWASABABU YA KUONANA NA KUACHANA CHADEMA BASI SEPA.
MWAKIBINGA NI YULE YULE NA SASA TUKUTANE CHUNYA MAHALI NILIPO ZALIWA.
HUJUMU KILA KITU ILA SIYO CHUNYA HAISEE
ACT WAZALENDO NDIYO CHAMA CHANGU KWASASA.
Mwakibinga II
0758 910403
Chagadema wahuni hao-mwenye akili na asiyekuwa opportunist hawez kukaa Chagadema. kadi yangu ni ya mwaka 2001 lkn mwaka 2009 niliichana