Aliyekua kada wa CHADEMA Philipo Mwakibinga amejiunga na chama cha ACT Wazalendo baada ya kushindwa kwenye kura za maoni huko jimbo la Lupa-Chunya. Sasa Mwakibinga atagombea ubunge jimbo hilo kupitia chama cha ACT.
Kwa maoni yangu Mwakibinga amekosea. Najua ni haki yake kujiunga na chama chochote cha siasa, najua pia ni haki yake kugombea ubunge. Lakini si kwa namna alivyofanya.
Nilitegemea Mwakibinga kama ilivyo kwangu na vijana wengine wa CHADEMA waliotangaza nia lakini hawakupitishwa, angetulia na kukisaidia CHADEMA kuiondoa serikali dhalimu ya CCM madarakani. Lakini ameamua kuondoka ili akatimize azma yake ya ubunge nje ya CHADEMA.
Nilimsoma Mwakibinga kwny group moja akisema "Huu ndio muda sahihi wa yeye kuwatumikia wananchi kama mbunge". Bila shaka alikuwa sahihi kuwaza hivyo. Lakini lazima aelewe kuwa CCM kuondoka madarakani ni muhimu zaidi kuliko yeye kuwa mbunge.
So angetulia ashirikiane na mgombea wa CHADEMA aliyepitishwa jimbo la Lupa ili chama kishinde. Ushindi wa CHADEMA Jimbo la Lupa ungekua ushindi kwa Mwakibinga pia. Chadema hatugawani vyeo tunagawana majukumu. Si lazima wote tuwe viongozi mwaka huu.
Mbona Julius S. Mtatiro alipokosa fursa Segerea hakuonesha kukereka? Hata alipoulizwa alijibu kwa hekima kuwa atamuunga mkono mgombea yeyote atakayepitishwa Segerea. Hii kilikua kiwango cha juu zaidi cha "matured politics".
Ni vizuri vijana tukajiandaa kisaikolojia tunapoamua kugombea nafasi za kisiasa. Tunaweza kuamini sisi ni bora zaidi ya wengine, tuna uwezo zaidi ya wagombea wengine lakini lazima tuheshimu maamuzi ya wananchi. Wakimpitisha mtu mwingine tofauti na sisi tusikasirike. Tumpe ushirikiano ili mradi awe amepitishwa kwa haki.
Pia ni muhimu tuelewe kuwa nafasi za kisiasa si ajira. Tusitegemee kufanya siasa kama sehemu ya ajira yetu. Ni muhimu wagombea wawe na ajira zao au njia zao nyingine za kuwaingizia kipato wakati wanagombea. Ili wasipopata nafasi wasione ndio mwisho wa maisha. Wasije kudhani hamna maisha nje ya siasa.
By the way namtakia kila la heri Mwakibinga huko alikoenda. Namtakia heri ktk mbio zake za ubunge jimbo la Lupa kupitia ACT (japo hatashinda). Pia nimtake ajiandae kisaikolojia kupokea matokeo ya ushindi wa CHADEMA jioni ya tar.25 October.!
ALL THE BEST MWAKIBINGA. Mwanajeshi mmoja akifa vitani, sio mwisho wa mapigano. Vita vinaendelea. Umetuacha vitani, tutapambana hadi dakika ya mwisho kuhakikisha CCM inaondoka madarakani. VIVA CHADEMA, VIVA UKAWA.!
View attachment 278559