Phd ya Obama kutoka open university.

Phd ya Obama kutoka open university.

kimweri Jr

Senior Member
Joined
Jun 9, 2012
Posts
131
Reaction score
42
Wanajamvi kwa wale wenye taarifa za kutosha naomba kufahamishwa ile phd ya heshima aliyopangiwa kupewa Rais obama alipewa? na kama hakupewa ni kwann? Kwa mwenye taarifa wadau tafadhali.
 
obama apendi vya bure yeye tayari ni profesa na anayo phd aliyoifanyia kazi kuipata
 
wakati mkuu wa chuo cha open anasema atampa alisema kama ikitokea wanapata nafasi atampatia kama watakosa hapewi..
 
Wanajamvi kwa wale wenye taarifa za kutosha naomba kufahamishwa ile phd ya heshima aliyopangiwa kupewa Rais obama alipewa? na kama hakupewa ni kwann? Kwa mwenye taarifa wadau tafadhali.

yule "mnene wa sayari ya 3" hawezi kukubali UCHOKO kama ule tena kutoka chuo magumashi kama kile kwani jamaa wenda alikifananisha na shule ya kata ya huko USA , so haki deserve kumpa heshima kama hiyo. matokeo yake akachinjia baharini na ndo maana prof. MBWETE akasema kuwa warikurupuka" kusema kuwa watampa mnene hiyo Ph.D wakati jamaa hana hata taarifa, so akashitukia janja yao kuwa wantaka kuuza sura kwenye "cable newz network -CNN, BBC, AL-JAZEERA, VOA, REUTERS, bila kufuata vigezo .
 
Ha ha ha ha Mkuu vioja.. naomba ninukuu gazeti la Mwananchi la leo.

Mbwete: Mpango wetu kwa Obama uko pale pale

Makamu Mkuu wa chuo kikuu huria Tanzania Profesa Tolly Mbwete amesema kuwa walichelewa kufanya mawasiliano na vyombo vinavyohusika na ili kupata fursa ya kumkabidhi Raisi ya Marekani, Barack Obama Shahada ya Heshima ya Uzamivu kama walivyokuwa wamepanga.

Profesa Mbwete akizungumza kwa njia ya simu alisema kuwa, ingawa Raisi Obama ameondoka bado wana njia mbili za kuweza kumkabidhi cheti ikiwa ni ishara ya kumtunuku shahada hiyo.
"Yule ni mtu mkubwa bwana ingetakiwa tufanye mawasiliano ya kupata nafasi ya kumkabidhi kwa miezi mitatu kabla, hata hivyo hiyo shahada kwa maana halisi tulishampa kwa sababu Mkuu wa chuo ndo mwenye mamlaka ya kuitoa, kilichokuwa kinasuburiwa ni kumkabidhi cheti tu na yeye atoe hotuba ya kuikubali," alisema Profesa Mbwete.

Anasema kuwa, chuo hicho kitawasiliana na Ubalozi wa Marekani nchini ili kuona njia itakayotumiwa katika kumaliza mchakato huo.

Kwa sasa kuna njia mbili za kumkabidhi, sisi tunaweza kwenda ama kukituma cheti hicho kupitia ubalozi na yeye akatuma hotuba yake," alisema Profesa Mbwete.

​
 
Kushindwa kumpa phd huyo Rais Wa USA. Ni udhaifu Wa MKUU Wa chuo kushindwa kufanya maandalizi ya kutosha
Isingekuwa so easy Kwa vile anatembelea Tanzania then mnakurupuka!
I will soon present that little risala
 
Huenda maafisa usalama wake waliiona ni ya kizushi ndo maana wakaichomolea kuwekwa kwenye ratiba.
 
Kushindwa kumpa phd huyo Rais Wa USA. Ni udhaifu Wa MKUU Wa chuo kushindwa kufanya maandalizi ya kutosha
Isingekuwa so easy Kwa vile anatembelea Tanzania then mnakurupuka!
I will soon present that little risala
Sasa alisemaje watamtunuku wakati walikuwa hawajafanya mawasiliano? Kwanini hakusubiri mpaka wawe na uhakika? Nchi ya Tanzania ni maneno maneno maneno maneno!
 
yaani niwe na hold phd toka havard university then nikubali phd ya chuo huria cha tanzania? ni sawa umekula biliani then unashushia na kande.
Kaka umenikuna na comment yako. ni kweli kabisa ndg yangu
 
Na angeipokea angeichanolia mbali kabla ya kuingia kwenye ndege,PHD YA OPEN UNIVERSITY bora hata ya INDIA
 
Yaani ni aibu kwa prof kusema hwakuwa na mawsiliano ya mapema!!!!!!!

Halafu wanafundisha watoto communication skills!!!!
 
Back
Top Bottom